Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Wakati wa ziara ya Kampeni za Uchaguzi Mheshimiwa Rais aliahidi kujenga daraja la kuunganisha Tarafa tatu za Luoimbo, Suba na Nyancha na tayari Halmashauri imeshapeleka makadirio Wizarani:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo?

Supplementary Question 1

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Swali la kwanza, Tarafa za Luoimbo, Suba na Nyancha ni tarafa zinazounganika, watu wanapita sehemu hiyo na Mheshimiwa Rais alitoa ahadi na muda wa ahadi za Rais kweli zitatekelezwa zote, je, imo ndani ya bajeti inayokuja kwamba inaanza kutengenezwa hata kama haitaisha kwa mwaka huu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni lini wananchi wa Rorya wataweza kuwa na matumaini kwamba Serikali yao inawakumbuka katika kilio chao hiki cha mafuriko ya kila mwaka?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdallah Bulembo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kwamba ipo kwenye bajeti ya mwaka huu, naomba anipe muda tupitie bajeti ya mwaka huu tutaangalia kama ipo. Cha muhimu ni kwamba mimi nilienda Rorya, nimefanya ziara ya kikazi, ni miongoni mwa wilaya za mwanzo kabisa nimezitembelea. Nimeenda Luoimbo, Suba na hii ni wilaya moja ilikuwa Tarime na Rorya imegawanywa hivi karibuni na imekuja na changamoto. Naomba wananchi wa Rorya, Mara na Watanzania wote waendelee kuiamini Serikali ya Chama cha Mapinduzi, ahadi hizi zote zitatekelezwa kabla ya uchaguzi wa mwaka wa fedha ujao. Tathmini imeshafanyika, tunahitaji shilingi bilioni 1.15 ya kukamilisha kazi hii. Ahsante.

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Wakati wa ziara ya Kampeni za Uchaguzi Mheshimiwa Rais aliahidi kujenga daraja la kuunganisha Tarafa tatu za Luoimbo, Suba na Nyancha na tayari Halmashauri imeshapeleka makadirio Wizarani:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo?

Supplementary Question 2

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kazi kubwa inayofanywa na TARURA inapunguzwa faida au kufifishwa faida yake kutokana na ukosefu wa fedha za kujenga madaraja muhimu. Wananchi wa Korogwe wamekuwa wakipata shida ya muda mrefu ya Madaraja yao ya Mbagai, Makondeko na Mswaha. Serikali haioni kwamba iko haja ya kuweka jicho maalum kwenye bajeti inayokuja kwa ajili ya madaraja kwenye barabara ambazo zinatengenezwa na TARURA?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Korogwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge, ni Mbunge mpya lakini anafanya kazi kubwa sana ya kutetea wananchi wake wa Korogwe. Jambo la pili ni kwamba huu mpango mkakati ni wa kudumu na ndiyo maana imeanzishwa TARURA ili wataalam wetu hawa wakilala, wakiamka wafikirie barabara zetu za vijijini na mijini. Kwa hiyo, naomba tu aamini kwamba kazi hii inaendelea kufanyika vizuri na huu ni mwaka wa bajeti na bajeti ya barabara hizi inabidi ianzie katika vikao vyao vya ndani kuanzia kwenye mtaa, kijiji, halmashauri yao na hatimaye hapa Bungeni. Sisi kama Serikali tupo tayari kushirikiana na wananchi wa Korogwe na Mheshimiwa Mbunge wao ili kuhakikisha kazi hii inafanyika vizuri na kuondoa kero zilizopo pale.