Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Wafungwa wakimbizi toka nchi za Burundi na DRC wamekuwa wakijaza mahabusu na magereza yetu:- (a) Je, kwa nini Serikali isikubaliane na nchi za Burundi na DRC kubadilishana wafungwa ili wakimbizi hao wafungwe katika nchi zao? (b) Je, wafungwa wa aina hiyo wanapokuwa mahabusu na magereza, Shirika la UNHCR linachangia gharama kwa kiasi gani? (c) Je, UNHCR imechangia fedha kiasi gani kwa wafungwa wakimbizi waliofungwa au kuwekwa mahabusu nchini kuanzia mwaka 2017/2018?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na maelezo ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, msingi wa hoja ni Serikali ianze mchakato wa kimkataba wa makubaliano, ndiyo msingi wa hoja. Kama kubadilishana wafungwa kunaongozwa na mkataba, ni lini Serikali yetu itaanza mchakato huo kati ya nchi ya DRC na Burundi ambazo zina wafungwa wengi Kasulu na Kigoma?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri anataka kuniambia wale wafungwa wa Kongo na Burundi waliopo Kibondo, Kasulu na Kigoma kwa ujumla wanatoka Taifa gani kama siyo wakimbizi toka nchi hizo nilizozisema?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daniel Nsanzungwanko, Mbunge wa Kasulu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza ni ushauri ambao tumeuchukuwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ni kweli wale ni wakimbizi lakini kwa maana ya tafsiri ya kisheria wamefanya makosa wamekuwa ni wafungwa. Kwa hiyo, kimsingi kwa tafsiri ya kisheria wale ni wafungwa.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Wafungwa wakimbizi toka nchi za Burundi na DRC wamekuwa wakijaza mahabusu na magereza yetu:- (a) Je, kwa nini Serikali isikubaliane na nchi za Burundi na DRC kubadilishana wafungwa ili wakimbizi hao wafungwe katika nchi zao? (b) Je, wafungwa wa aina hiyo wanapokuwa mahabusu na magereza, Shirika la UNHCR linachangia gharama kwa kiasi gani? (c) Je, UNHCR imechangia fedha kiasi gani kwa wafungwa wakimbizi waliofungwa au kuwekwa mahabusu nchini kuanzia mwaka 2017/2018?

Supplementary Question 2

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa kumekuwa na operesheni ambayo inafanywa na Jeshi la Polisi ya kusaka watu ambao wanasema hawana kazi mtaani. Cha ajabu hawa watu wanakamatwa kipindi kile cha jioni tayari wamesharudi makazini wakiwa wamepumzika barazani huko Dar es Salaam na maeneo mengine ya Tanzania hali ambayo inapelekea kujaza mahabusu zetu katika maeneo mengi ya nchi hii. Serikali inatoa tamko gani kuhusu operesheni hii inayofanywa na Jeshi la Polisi ambayo inapelekea kujaza mahabusu bila sababu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maftaha, Mbunge wa Mtwara Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina taarifa ya maelezo ambayo ametoa Mheshimiwa Mbunge kwamba Polisi wanachukuwa mtu yeyote. Nachojua katika utaratibu wa kawaida wa Jeshi la Polisi ni kufanya doria na pale wanapoona watu wanaojihusisha na uhalifu ama wana viashiria vya uhalifu kuwachukuwa na kufanya uchunguzi wao ili hatua zaidi zichukuliwe. Taarifa za ziada kwamba kuna watu ambao anadhani yeye hawakupaswa kuchukuliwa na Jeshi la Polisi kutokana na shughuli hiyo, labda angetupatia taarifa mahsusi ili tuweze kuzifanyia kazi.

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Wafungwa wakimbizi toka nchi za Burundi na DRC wamekuwa wakijaza mahabusu na magereza yetu:- (a) Je, kwa nini Serikali isikubaliane na nchi za Burundi na DRC kubadilishana wafungwa ili wakimbizi hao wafungwe katika nchi zao? (b) Je, wafungwa wa aina hiyo wanapokuwa mahabusu na magereza, Shirika la UNHCR linachangia gharama kwa kiasi gani? (c) Je, UNHCR imechangia fedha kiasi gani kwa wafungwa wakimbizi waliofungwa au kuwekwa mahabusu nchini kuanzia mwaka 2017/2018?

Supplementary Question 3

MHE. KABWE Z.R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ukienda Segerea utakuta idadi ya mahabusu ni wengi zaidi kuliko watu ambao wameshahukumiwa na hii inatokana na sheria kandamizi ambazo zinanyima watu dhamana kama zilivyonyima dhamana Wabunge wetu wawili; Mheshimiwa Mbowe na Mheshimiwa Matiko na Sheria ya Anti Money Laundering ambayo makosa yanawekwa tu ili kuweza kuwaweka ndani watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haioni kwamba imefikia wakati kwa watu ambao umri wao ni kuanzia miaka 75 na kuendelea kama ilivyokuwa kwa Mheshimiwa William Shelukindo ambaye aliwekwa kwenye Gereza la Maweni kwa kukosa dhamana tu, kuweka utaratibu watu hawa wawe wanafungwa kifungo cha nyumbani kwao badala ya kuwajaza magerezani bila sababu kutokana na umri wao kama ambavyo nchi nchi nyingine wanafanya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Zitto amezungumza vitu viwili kwa pamoja suala la mahabusu na wafungwa. Suala la wafungwa siku zote nimekuwa nikieleza mikakati ya Serikali ya jinsi ya kupunguza msongamano kwenye magereza kupitia njia mbalimbali. Tumeona Mheshimiwa Rais akitoa msamaha kwa wafungwa, tuna sheria za parole, sheria za huduma za jamii na nyinginezo. Pia tunafanya jitihada ya kujenga magereza ili kupunguza ule msongamano. Kwa hiyo, kimsingi kwa wafungwa huo ndiyo mkakati wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la mahabusu ni suala la kisheria zaidi, kumchukua mahabusu na kumpa kifungo cha nje anakuwa bado hajahukumiwa. Kwa hiyo, cha msingi ni kufuata sheria za dhamana ili aweze kupata dhamana wakati huo huo sisi tukifanya jitihada za kuboresha mahabusu zetu ili kuepusha msongamano na madhara yanayoweza kujitokeza.