Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Halmashauri ya Geita DC ina Majimbo mawili ya Geita Viijini na Busanda ambayo kiutawala husababisha usumbufu na hali tete kwa wananchi kijiografia na mkoa ulishapitisha kuomba Serikali iigawe kuwa na Halmashauri ya Busanda:- Je, ni lini Serikali itaridhia ombi hilo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwana naomba niweke kumbukumbu sawa. Mimi ni Mbunge wa Geita, siyo Geita Vijijini. Hakuna Jimbo la Geita Vijijini.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Geita DC ina population ya takribani watu 1,200,000 kwa sensa ya mwaka 2012/2013. Sasa kwa majibu ya Serikali, inavyoonekana, bado tutakwenda hata uchaguzi ujao tukiwa bado tunakaa Halmashauri moja. Je, Serikali inatoa kauli gani ya uharaka kwa ajili ya kuharakisha hizo taasisi zilizobaki ili tuweze kupata mgawanyo wa Halmashauri mbili?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba Mheshimiwa Waziri atamke kitu kwamba kulingana na ukubwa na wingi wa watu wa Halmashauri ya Geita DC, Serikali inaona umuhimu gani wa kutuongezea ceiling ya bajeti kwa wingi wa watu tulionao?

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi ni kwamba suala la kugawa Mamlaka za Serikali za Mitaa linatakiwa lianzishwe na mamlaka yenyewe kwenye eneo hilo. Nimesema tayari jambo hili limejadiliwa kwenye Halmashauri yao ya Wilaya ya Geita. Sasa ni wajibu wao kupeleka mjadala huo kwenye ngazi ya Wilaya na ngazi ya Mkoa, nasi tupo tayari kupokea mapendekezo yao na tuangalie uharaka na ulazima wa kufanya maamuzi ya kugawa Halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Spika, jibu la swali la pili ni kwamba bajeti ya Serikali inategemea na uwezo uliopo. Nia ya Serikali ni njema kabisa kwamba bajeti iongezeke na kila mtu angeweza kupata mgao ambao angehitaji. Hili nalo linategemea pia uwezo wa Serikali, kadri itakavyoruhusu basi bajeti itaongezeka ili huduma iweze kupelekwa kwa wananchi wa Geita na maeneo mengine ya nchi. Ahsante.

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Halmashauri ya Geita DC ina Majimbo mawili ya Geita Viijini na Busanda ambayo kiutawala husababisha usumbufu na hali tete kwa wananchi kijiografia na mkoa ulishapitisha kuomba Serikali iigawe kuwa na Halmashauri ya Busanda:- Je, ni lini Serikali itaridhia ombi hilo?

Supplementary Question 2

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili nami niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro ambao una population kubwa sana: Je, Serikali inaonaje sasa hii mamlaka ya mji mdogo iwe mamlaka kamili ya mji?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kama nilivyosema, mchakato huu wauanzishe wenyewe watu wa Geita na hususan Busanda; nasi Ofisi ya Rais TAMISEMI tutapokea mapendekezo yao na tutawahisha jambo hili kadri itakavyohitajika kulingana na ukubwa wa bajeti na upatikanaji wa fedha.