Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KABWE R. Z. ZITTO aliuliza:- (a) Je, ni kwa nini Serikali ya Tanzania inazuia wawekezaji wa uvuvi kuvua kwa kutumia purseiner katika Ziwa Tanganyika ilhali nchi za Burundi, Zambia na DRC zinazopakana na ziwa hilo huruhusu uvuvi huo? (b) Je, kwa nini Serikali inawaelekeza wawekezaji wa uvuvi katika Ziwa Tanganyika kuhamisha uwekezaji wao na kuupeleka mahali pengine nchini na je, huu sio makakati wa kukwamisha maendeleo ya Mkoa wa Kigoma na watu wake?

Supplementary Question 1

MHE. KABWE R. Z. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini sasa Serikali itafanya utafiti iweze kutoa kanuni za kuwezesha uvuvi wa kisasa na viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi katika Mkoa wa Kigoma kuweza kufanyika? Lini utafiti huo utaweza kufanyika kwa sababu sio wajibu wa wananchi ni wajibu wa Serikali kufanya huo utafiti na miaka 21 imepita bila huo utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sasa hivi kumekuwa na leseni nyingi sana za uvuvi. Mvuvi mmoja yaani kwa chombo kimoja kinahitaji leseni takribani tisa na hivyo kuongeza gharama kubwa sana kwa wavuvi wa Ziwa Tanganyika. Vilevile gharama za kuuza mazao ya uvuvi nje zimeongezeka kutoka senti 0.5 ya dola ya Marekani mpaka dola 1.5 kitu ambacho kinatufanya wavuvi wa Mkoa wa Kigoma kutokushindana vizuri na wenzetu wa Burundi na Congo kwa sababu wao hawana tozo hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni lini Serikali itahusianisha hizo tozo na kuzishusha ili tueweze kuendeleza export tunayoifanya sasa hivi ya mazao yetu kutoka Ziwa Tanganyika?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali linalouliza kuwa ni lini Serikali itafanya utafiti. Kupita taasisi yetu ya TAFIRI tumeanza hatua za awali za kufanya utafiti katika maji yetu ya Ziwa Victoria, lakini vile vile tunacho kituo cha TAFIRI pale Kigoma. Kwa hivyo hatua za mwanzo za utafiti huu kwa kushirikiana na nchi zinazozunguka Ziwa hili Tanganyika kupitia taasisi inayotuunganisha tutafanya utafiti pia wa kujiridhisha ya stock assessment na hatua za kuweza kuwaruhusu wawekezaji wakubwa, wakati na wadogo ziweze kuendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la ni juu ya leseni nyingi zilizopo. Uwepo wa leseni katika tasnia ya uvuvi
ni jambo la matakwa la kisheria lakini vilevile ya kitaalam. Kwa sababu inatusaidia hata kujua idadi ya wavuvi tulionao.

Naomba nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge juu ya tozo tunazozitoza kuonekana kuwa ni nyingi na kubwa na kutufanya tusiwe na ushindaji sahihi na wenzetu. Jambo hili ndani ya mamlaka yetu, tupo tayari kukaa na wadau kuweza kushaurina ili kuweza kufanya tasnia ya uvuvi iweze kuwa na manufaa kwa Taifa letu.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. KABWE R. Z. ZITTO aliuliza:- (a) Je, ni kwa nini Serikali ya Tanzania inazuia wawekezaji wa uvuvi kuvua kwa kutumia purseiner katika Ziwa Tanganyika ilhali nchi za Burundi, Zambia na DRC zinazopakana na ziwa hilo huruhusu uvuvi huo? (b) Je, kwa nini Serikali inawaelekeza wawekezaji wa uvuvi katika Ziwa Tanganyika kuhamisha uwekezaji wao na kuupeleka mahali pengine nchini na je, huu sio makakati wa kukwamisha maendeleo ya Mkoa wa Kigoma na watu wake?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimwia Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri. Kwa sababu makatazo yaliyokuwa yamefanyika Ziwa Tanzanyika yamemefanyika pia Ziwa Victoria hasa kwa kuzuia matumizi ya taa za solar kwenye shughuli ya uvuvi wa dagaa. Kwa sababu juzi Mheshimiwa Waziri niliona anatoa tamko kule Ferry, ni nini sasa kauli thabiti kwa wavuvi wa Ziwa Victoria ili waendee kutumia taa za solar mpaka pale utaratibu utakapo kamili?

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimwa Mabula kwa swali lake.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba baada ya kutafakari sana malalamiko ya wavuvi wetu katika maziwa mbalimbali juu ya leseni nyingi, matumizi ya jenereta pamoja na matumizi ya taa za solar; na kwa mamlaka niliyonayo nikaamua kwamba sasa matumizi ya solar na jenereta yaruhusiwe na wananchi wasikamatwe kwa kutokuwa na leseni hivi sasa wakati tunatatua tatizo hili la kuwa na leseni nyingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ninachotaka kuwambia wavuvi wote na Mheshimiwa Mbunge ni kwamba nimeruhusu rasmi matumizi ya taa za solar na jenereta mpaka tarehe 1 Julai. Hata hivyo Serikali haikusudii kuzuia wananchi kutumia solar isipokuwa ni kuwa-guide kwamba ni solar zenye watts kiasi gani ambazo zitahitajika kutumika, hapo ndio tutatoa hizo guidelines tarehe 1 Julai.