Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH O. MBILINYI aliuliza:- Katika bajeti ya mwaka 2017/2018 Wizara ya Afya iliomba na kutengewa shilingi bilioni tano kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la maabara na ununuzi wa vipimo vya kisasa kama CT Scan na MRI Scan katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya. (a) Je, ni kiasi gani cha fedha kimeshatolewa mpaka sasa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo? (b) Kwa kuwa bajeti inayohitajika imeshatengwa; je, ni lini ujenzi huo utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ili kuondoa ile dhana kwamba hatupongezi kila kitu, naomba niseme kwamba naipongeza Wizara na hasa Katibu Mkuu aliyepita Dkt. Mpoki, kwa kutoa ushirikiano kwa Mbunge katika hili mpaka hapo tulipofika na jengo kukamilika na CT-Scan kupatikana. Swali la kwanza, ningependa kujua sasa, hiyo MRI chini ya huo Mradi wa ORIO itafika lini ili jengo lile lianze kazi? Kwa sababu tunalifuatilia na kwa taarifa tulizonazo ndani ya wiki mbili litaanza kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, vipi kuhusu wataalam (specialists), maana tunafanikiwa kwenye majengo ila mara nyingi tunakuwa na uhaba mkubwa wa specialists. Binafsi, kama ningeweza kumshauri Mheshimiwa Rais, ningemshauri huyu Dkt. Mpoki aliyekuwa Katibu Mkuu kuliko kupelekwa Ubalozini angeletwa hata kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwa sababu ule utaalam wake ni muhimu sana kwa Taifa na wako Madaktari wachache sana wenye utaalam ule. Kwa hiyo, kumpeleka mbali, ni kupeleka huduma mbali kutoka kwa Taifa. Ahsante sana.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa kwa kuipongeza Serikali, nami nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufanya ufuatiliaji wa karibu katika suala hili la ujenzi wa jengo la radiolojia katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na ni lini Serikali itapeleka mashine ya MRI; kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, ni kwamba sasa hivi Serikali kupitia Mradi wa ORIO ambao tunashirikiana na Serikali ya Uholanzi, ina kusudio la kupeleka mashine za radiolojia kwa maana ya X-Ray, Digital X-Ray, mashine za fluoroscopy, CT-Scan pamoja na MRI. Kwa hiyo, mchakato huo unaendelea. Tunategemea katikati au mwishoni mwa mwaka huu, utaratibu huo utakuwa umekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake la pili, Madaktari bingwa katika eneo hili; mkakati ambao tunakwenda nao sisi kama Wizara kwa sasa hususan katika wataalam wa Sekta ya Radiolojia, tumeamua kwamba tutumie ubunifu na teknolojia ya kisasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunavyoongea, huko duniani X-Rays zinazopigwa mathalan katika nchi ya Marekani, nyingine hazisomwi Marekani, zinasomwa katika nchi nyingine kwa kutumia teknolojia. Hizi mashine za Digital X-Ray ambazo tunazifunga sasa hivi, sisi kama Wizara tumeamua kuweka kituo chetu pale katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambapo tutaunganisha na mtandao wa fibre- optic, kutakuwa na screen pale ili picha ambazo zitakuwa zinapigwa Tanzania nzima kwa teknolojia hii, ndani ya dakika tano picha umepata. Tunaweza tukatuma kwa njia ya mtandao, zitasomwa Dar es Salaam na majibu ndani ya dakika 15 kurudishwa katika eneo husika. Kwa hiyo, tumejipanga vizuri sana katika eneo hilo.

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH O. MBILINYI aliuliza:- Katika bajeti ya mwaka 2017/2018 Wizara ya Afya iliomba na kutengewa shilingi bilioni tano kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la maabara na ununuzi wa vipimo vya kisasa kama CT Scan na MRI Scan katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya. (a) Je, ni kiasi gani cha fedha kimeshatolewa mpaka sasa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo? (b) Kwa kuwa bajeti inayohitajika imeshatengwa; je, ni lini ujenzi huo utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Hospitali ya Bombo katika Jiji la Tanga ndiyo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa; na kwa kuwa hospitali hiyo haina lift kiasi kwamba wanawake wazazi wanatengenezewa theater kule kule kwa ajili ya kuwasaidia wasipate taabu ya kubebwa na mabaunsa: Je, ni lini Hospitali ya Bombo itapatiwa lift?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nuru kuhusiana na suala la Hospitali ya Bombo. Nikiri ni kweli Hospitali ya Bombo, jengo la akina mama na watoto halina lift. Nami bahati nzuri nilipata fursa ya kwenda kulitembelea, nimeiona hiyo adha, nasi kama Serikali tumeingiza katika mipango yetu ya bajeti ili tuweze kukarabati hiyo lift.