Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. KHATIB SAID HAJI aliuliza:- Viwango vya riba katika benki hapa nchini ni vikubwa na vimekuwa ni kikwazo kwa Watanzania wengi kuweza kukopa na kufanya biashara:- Je, Serikali inachukua hatua gani ili Benki ziweze kupunguza viwango hivyo vya riba?

Supplementary Question 1

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza katika hili napenda kwa dhati kabisa kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa juhudi zake katika kuhakikisha benki zinaendelea kupunguza riba za mikopo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, ni kweli benki zimeanza kuitikia wito huu na kipekee niipongeze Benki ya CRDB kwa kuwa wa kwanza kuitikia wito huu. Hata hivyo, inaonekana mikopo ambayo inapewa unafuu wa riba na kwa haraka ni ya wafanyakazi na watumishi wa umma lakini mikopo ya kibiashara bado mabenki yanaonekana kusuasua katika kufikia lengo hilo. Je, Serikali inatoa kauli gani ya kuzitaka benki kushusha riba kwa mikopo ya kibiashara?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mara nyingi tu katika Bunge hili nimekuwa nikisema kwamba kiwango kikubwa cha riba katika benki kinatokana na kiwango cha T-Bills ambacho kinapangwa na Serikali BOT. Je, Serikali inatoa kauli gani kuwa riba zinazotozwa na microfinances ambazo ndiyo kimbilio kubwa la wananchi wa kawaida? Ahsante.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Khatib Said Haji, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, Serikali kwa nia thabiti kabisa imechukua hatua za kisera na benki zetu za kibiashara kwa kuanza wameanza na mikopo hii ya watumishi. Ni imani yetu kama Serikali benki zitashusha riba kwa wakopaji wote wakiwemo wakopaji wanaokopa kwa ajili ya biashara zao kwa kuzingatia watu hawa wanapatikana wapi na nini wanadhamiria kukifanya. Cha msingi nachotaka kuwaomba wafanyabiashara wetu ni kuwa na mipango thabiti wakati wanachukua mikopo hii ili kuhakikisha pesa wanazokopa zinaweza kurejeshwa na hivyo kuleta imani kwa benki zetu kwa wafanyabiashara wetu kwamba ni wakopaji wa uhakika na ni imani ya Serikali yetu kwamba riba zitaendelea kupungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, napenda kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba kwa kutambua umuhimu wa wajasiriamali wadogo, kwa kutambua umuhimu wa Watanzania wanaokwenda kukopa katika microfinances, Serikali yetu ya Awamu ya Tano ilizindua Sera ya Taifa ya Huduma Ndogo ya Fedha Desemba, 2017. Dhamira kubwa ya sera hii ni kuhakikisha kwanza tunawatambua wakopeshaji kwenye huduma ndogo za kifedha lakini pia kuhakikisha tunawalinda wakopaji kwenye sekta hii ya huduma ddogo za fedha ili wawe na uhakika wanakopa nini na sheria, taratibu na kanuni za utawala bora ziweze kufuatwa hata kwenye sekta hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba Serikali yetu inatambua mchango wa bei ya T-Bills. Sasa hivi tumeweza kupunguza bei ya T-Bills kwa kiwango kikubwa ili kuhakikisha pia bei ya fedha zinazokopeshwa inakuwa ndogo.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. KHATIB SAID HAJI aliuliza:- Viwango vya riba katika benki hapa nchini ni vikubwa na vimekuwa ni kikwazo kwa Watanzania wengi kuweza kukopa na kufanya biashara:- Je, Serikali inachukua hatua gani ili Benki ziweze kupunguza viwango hivyo vya riba?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa fursa hii na nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kujibu vizuri na Serikali kuwa na mkakati mzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza deposit rate, maana watu wengi hawaweki fedha benki kwa sababu riba ni ndogo sana na riba ya kukopesha ni kubwa sana. Kama mkakati huu ukitekelezwa benki itakuwa na fedha nyingi ya kukopesha kwa riba ndogo. Naomba jibu, je, Serikali ina mkakati gani kuhusu suala hili?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali moja la nyongeza la mtani wangu, Mheshimiwa Dkt. Mary Michael Nagu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, Serikali inashughulika na Sera ya Sekta ya Fedha na nimeainisha hatua mbalimbali tulizozichukua. Moja katika taratibu zilizopunguzwa ni statutory minimum reserve rates za mabenki yetu. Tumeona sasa, kama nilivyosema tangu awali, riba zinapungua na hivyo hata deposit rate nayo itaweza kuongezeka ili kuona kwamba Watanzania wanaweza kuweka fedha zao katika benki zetu.

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHATIB SAID HAJI aliuliza:- Viwango vya riba katika benki hapa nchini ni vikubwa na vimekuwa ni kikwazo kwa Watanzania wengi kuweza kukopa na kufanya biashara:- Je, Serikali inachukua hatua gani ili Benki ziweze kupunguza viwango hivyo vya riba?

Supplementary Question 3

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niungane na Mheshimiwa Mbunge aliyeuliza swali la msingi kumpongeza Rais kwa kupigania kupunguza riba kwenye benki, lakini kwenye taasisi ndogo ndogo, kwa mfano PRIDE, FINCA, Tunakopesha mpaka navyoongea sasa hivi riba inafika asilimia 33. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwadhibiti hawa watu wanaofikisha riba mpaka asilimia 33 na kusababisha akina mama kunyang’anywa vitu vyao kila siku? Maana yake pesa ile sasa inakuwa haizai kazi yake ni kurudisha riba inapofikia miezi sita mama yule anaanza kunyang’anywa vitu vya ndani. Mheshimiwa Waziri ana mkakati gani wa kukomesha tabia ya kufikisha riba asilimia 33?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali moja la nyongeza la dada yangu, Mheshimiwa Munde, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, tumepitisha Sera ya Taifa ya Huduma Ndogo ya Fedha na moja ya malengo yake ni kuhakikisha kunakuwa na uzingatiaji wa kanuni za utawala bora kwenye taasisi zinazotoa huduma kwenye sekta ndogo ya fedha. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba Sheria ya Huduma Ndogo ya Fedha iko katika hatua za mwisho na ni imani yangu ndani ya mwaka huu sheria hii itapitishwa ili kuwalinda wakopaji wadogo katika sekta ndogo ya fedha. Naamini itakuwa ndiyo mkakati wetu na suluhisho la kuwalinda watu wetu.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. KHATIB SAID HAJI aliuliza:- Viwango vya riba katika benki hapa nchini ni vikubwa na vimekuwa ni kikwazo kwa Watanzania wengi kuweza kukopa na kufanya biashara:- Je, Serikali inachukua hatua gani ili Benki ziweze kupunguza viwango hivyo vya riba?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nami naomba niulize swali moja tu. Kwa kuwa benki zote ziko chini ya Wizara ya Fedha na kwa kuwa CRDB wameanza kupunguza riba, je, kwa nini benki nyingine zisipunguze riba ili wananchi na wafanyabiashara waweze kupata mikopo kuliko hali ilivyo sasa?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali moja la nyongeza la kaka yangu Mheshimiwa George Lubeleje, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema kwenye jibu langu la msingi na nizipongeze Benki ya CRDB, NMB na ABC, benki zote hizi zimeshusha riba yao kutoka zaidi ya asilimia 20 mpaka asilimia 17. Ni imani ya Serikali kwamba benki zote zitafuata mwanzo huu mzuri ulioanzwa na benki hizi tatu nilizozitaja kama njia mojawapo ya kuakisi jitihada njema za Serikali ya Awamu ya Awamu ya Tano na Mheshimiwa Rais wetu dhamira yake ya kuhakikisha Watanzania wanapata fedha za mitaji kwa bei iliyo chini kabisa.