Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Halmashauri ya Busokelo ina utajiri mkubwa wa madini na gesi asilia aina ya carbon dioxide:- Je, ni lini Serikali itaenda kufanya utafiti wa kutosha kwenye Kata ya Lufilyo ambapo kuna madini aina ya marble (marumaru)?

Supplementary Question 1

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, napenda kuweka kumbukumbu sahihi kwamba mimi ni Mbunge wa Jimbo la Busokelo na si Rungwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Halmashauri ya Busokelo ina utajiri mkubwa sana wa madini aina ya marble pamoja na carbondioxide gas. Serikali imekiri hapa kwamba madini ya marble yanapatikana katika Kijiji cha Kipangamansi, Kata ya Lufilyo. Je, ni lini Serikali itakuja kufanya tafiti katika milima ya safu za Livingstone kwani inasadikika pia kuwa kuna madini aina ya dhahabu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Waziri tumekuwa tukiongea mara nyingi kwamba atutembelee Halmashauri ya Jimbo la Busokelo ili apate kushuhudia wananchi wangu wanaojishughulisha na hizo shughuli za marble. Ni lini Waziri atakuja kuwatembelea wananchi wa Jimbo langu na kuona shughuli hizo za madini? (Makofi)

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwakibete, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu namuomba radhi kidogo Mheshimiwa Mbunge kwa kukosea kutaja jina lake. Nieleze tu kwamba Mheshimiwa Mwakibete ni miongoni mwa Wabunge ambao kwa kweli katika kufuatilia masuala ya madini kwenye Jimbo lake amekuwa mstari wa mbele. Kama alivyoeleza hapa, mara nyingi amekuwa akitualika Wizara twende kwenye Jimbo lake na mara ya mwisho tulizungumza tukakubaliana tutakwenda. Nataka nimuhakikishie kwamba tutakwenda mara baada ya kukamilisha Bunge la Bajeti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni lini tutafanya utafiti kwenye Milima ya Livingstone, naomba nimjulishe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Taasisi yetu ya GST inaendelea kufanya tafiti mbalimbali kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini ili kubaini maeneo yenye madini ikiwemo eneo la Busokelo na Lufilyo kama alivyoomba.

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Halmashauri ya Busokelo ina utajiri mkubwa wa madini na gesi asilia aina ya carbon dioxide:- Je, ni lini Serikali itaenda kufanya utafiti wa kutosha kwenye Kata ya Lufilyo ambapo kuna madini aina ya marble (marumaru)?

Supplementary Question 2

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika nchi yetu kuna madini ya aina mbalimbali kama vile ruby, sapphire blue, ulanga na tin katika Mkoa wa Kagera, Wilaya ya Karagwe. Je, Serikali ina mkakati gani wa kutangaza madini haya katika soko la dunia kama inavyotangaza tanzanite, dhahabu na almasi? Ahsante. (Makofi)

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kahigi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, madini yote ambayo tunayachimba hapa nchini ni wajibu wetu kama Serikali kuyatangaza kwamba yapo ndani ya nchi na kuwavutia wawekezaji waje kuwekeza katika madini hayo. Madini ya tin na madini mengine aliyoyataja tunaendelea na mkakati huo wa kuyatangaza duniani kote na ndiyo maana ataona hata leo akienda hapo nje atakuta tuna maonyesho mbalimbali. Baada ya bajeti hii tutakuwa na vipindi mbalimbali vya redio, televisheni, magazeti na machapisho mbalimbali kwa ajili ya kutangaza utajiri tulionao ndani ya nchi yetu yakiwemo madini ya tin na haya mengine ya vito aliyoyataja. (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Halmashauri ya Busokelo ina utajiri mkubwa wa madini na gesi asilia aina ya carbon dioxide:- Je, ni lini Serikali itaenda kufanya utafiti wa kutosha kwenye Kata ya Lufilyo ambapo kuna madini aina ya marble (marumaru)?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza kwa niaba ya wananchi wa Longido ambao pia nina furaha kwamba Madiwani wao karibu wote leo wapo hapa kama wageni wa Bunge hili Tukufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido sawa na Busokelo, kwamba tuna utajiri mkubwa wa madini ya rubi. Kwa kuwa madini ya rubi ukiyakata ili kuyaongezea thamani kulingana na utaratibu uliotolewa na Serikali yanasagika. Kwa kuwa Mawaziri walishatembelea na wakajua changamoto hiyo, wanatuambia ni lini utaratibu huo utakamilika ili wananchi waweze kuyauza mawe haya waendelee kunufaika?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kiruswa, Mbunge wa Longido, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba mimi pamoja na Naibu Waziri mwenzangu, Mheshimiwa Nyongo tulikwenda Longido na hasa kwenye eneo la Mundarara anbako kuna machimbo ya rubi. Wananchi wa kule wanajihusisha na shughuli hiyo na changamoto aliyoizungumza Mheshimiwa Mbunge walitueleza kwenye mazungumzo yetu na wao. Jambo ambalo linapaswa lieleweke hapa ni kwamba Sheria yetu mpya ya Madini imezuia kabisa usafirishaji wa madini ghafi kwenda nje ya nchi. Lengo ni kwamba tunataka teknolojia na ajira zibaki ndani ya nchi kuliko kuzisafirisha kwenda nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo madini ambayo yana upekee wa aina yake katika ukataji. Serikali kupitia Wizara ya Madini na Tume ya Madini tunaandaa mwongozo wa namna bora zaidi ya kuwasaidia wananchi ili waweze kupata fursa ya kuuza madini haya.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Halmashauri ya Busokelo ina utajiri mkubwa wa madini na gesi asilia aina ya carbon dioxide:- Je, ni lini Serikali itaenda kufanya utafiti wa kutosha kwenye Kata ya Lufilyo ambapo kuna madini aina ya marble (marumaru)?

Supplementary Question 4

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Njombe kuna wananchi wengi sana wameomba leseni kwa ajili ya utafiti na uchimbaji wa makaa ya mawe. Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini wananchi hawa mtawapa leseni hizo ili tuweze kuinua uchumi wa Mkoa wetu wa Njombe?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Neema William Mgaya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Neema Mgaya yuko mstari wa mbele kuwapigania wananchi wa Mkoa wa Njombe na hususan wanawake. Naomba nichukue nafasi hii nimpongeze kwamba juhudi zake si bure, wananchi na wanawake wa Mkoa wa Njombe wanaziona na sisi kama Serikali tutamuunga mkono kwa hatua alizonazo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo la lini tutaanza kuwapa leseni, naomba nimpe taarifa njema Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Serikali kupitia Tume yetu ya Madini ambayo imeteuliwa hivi karibuni, tumeanza kutoa leseni kwa wachimbaji wadogo zote ambazo zilikuwa zimeombwa na tunapitia maombi mengi ambayo yapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa kwamba mpaka sasa kuna jumla ya zaidi ya leseni 5,000 tunazitoa nchini kote. Wananchi wa Mkoa wa Njombe ambao wapo kwenye maombi hayo na wao watahudumiwa kama wengine. Nashukuru.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Halmashauri ya Busokelo ina utajiri mkubwa wa madini na gesi asilia aina ya carbon dioxide:- Je, ni lini Serikali itaenda kufanya utafiti wa kutosha kwenye Kata ya Lufilyo ambapo kuna madini aina ya marble (marumaru)?

Supplementary Question 5

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliahidi kusaidia wachimbaji wadogo wadogo. Jimboni kwangu wapo wachimbaji wadogo wadogo wa Kata ya Katuma ambao wanajishughulisha na uchimbaji wa dhahabu. Je, Serikali inachukua hatua ipi ya kusaidia wachimbaji wadogo waweze kufanya shughuli zao?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Moshi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya Serikali ni kuwasaidia wachimbaji wadogo na kuwainua ili watoke kwenye uchimbaji mdogo waje kwenye uchimbaji wa kati, na walio kwenye uchimbaji wa kati waende kwenye uchimbaji mkubwa. Kazi ya Serikali, hatua ya kwanza ya kuwasaidia wachimbaji wadogo ni kuwarasimisha. Kila mahali ambapo tunakuta kuna wachimbaji wadogo ambao hawapo rasmi tunawarasimisha kwa kuwaweka kwenye vikundi na baadaye kuwapatia leseni wawe na uhalali wa kuweza kuchimba. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya pili ni kuwapatia mafunzo ya namna bora ya uchimbaji kwa kuzingatia sheria lakini vile vile utunzaji wa mazingira. Kazi hizi zote Mheshimiwa Mbunge ataziona baada ya bajeti hii kwa sababu hii ni Wizara mpya, tutakuwa na progamu maalum ya kuwasaidia wachimbaji wadogo wakiwemo wachimbaji wake wa Kata ya Katama.