Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete iliahidi kujenga kwa lami barabara ya kutoka Kimara Mwisho kupitia Mavulunza – Bonyokwa Segerea hadi kuungana na barabara ya Nyerere yenye urefu wa Kilomita 4.7 na ambayo imekasimiwa kwa TANROADS:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo kwa lami kama ambavyo iliahidiwa miaka mitano iliyopita? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara hiyo ili kupunguza tatizo la foleni?

Supplementary Question 1

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Swali la kwanza, ukiangalia majibu ya Mheshimiwa Waziri anasema kwamba baada ya kukamilika barabara ya Kinyerezi - Mbezi ndipo wanapotegemea kuanza ujenzi wa barabara hii inayoongelewa hapa na Mheshimiwa Kubenea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimkumbushe Mheshimiwa Waziri kwamba hizi ni barabara mbili tofauti na mahitaji ya wananchi wale ni tofauti. Tunataka kufahamu ni lini Serikali specifically itaanza ujenzi wa barabara inayotajwa iliyoahidiwa miaka mitano iliyopita? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, suala lililopo Jimbo la Ubungo linafanana moja kwa moja na masuala yaliyopo katika Jimbo la Ndanda, Mkoa wa Mtwara kwamba Serikali iliahidi kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mtwara Mjini – Nanyamba – Tandahimba – Newala - Masasi mpaka Nachingwea kuja kutokea Nanganga. Sasa tunataka kufahamu pamoja na mkandarasi kuwepo pale ambaye anasuasua kwenye kazi hii, ni lini Serikali specifically itaanza ujenzi wa barabara inayotokea Masasi kwenda Nachingwea kuja kutokea Nanganga?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba katika barabara ambazo nimezitaja awali ndiyo zilikuwa na matatizo makubwa na ndiyo zilikuwa kipaumbele. Niseme tu kwamba nafahamu maeneo haya ambayo Mheshimiwa Mbunge anayazungumzia ni korofi na kama nilivyosema tutaendelea kuyashughulikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yako maeneo matatu ambayo tulikuwa tunaendelea nayo kuhakikisha kwamba barabara hii inatoa huduma iliyokusudiwa wakati sasa tukikamilisha hii barabara ni fursa tosha kuja kuijenga barabara hii. Yako maeneo pale Kwa Bichwa, Kwa Mahita na eneo la Makange Sekondari ndiyo zilikuwa sehemu korofi. Alikuwepo mkandarasi anaendelea kurekebisha maeneo yale lakini kutokana na mvua nyingi zilizonyesha amesimama kidogo ili hali ya hewa ikiwa nzuri hii barabara tuiimarishe halafu baadaye sasa wakati barabara hizi zinakamilika ni fursa tosha kuja kuijenga hii barabara kama ahadi ilivyokuwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Ndanda kuja Nachingwea kupitia Nanganga kama tulivyoizungumza katika bajeti tumetenga fedha kwa ajili ya kutengeneza kipande hiki kutoka Nachingwea - Nanganga na Nachingwea – Ruangwa – Nanganga. Mheshimiwa Mbunge anafahamu pia liko daraja katika Mto Lukuledi tunaendelea kulijenga na hii ni sehemu ya kukamilisha barabara hii anayoitaja ili sasa tuweze kuunganisha kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimsihi tu Mheshimiwa Mbunge avute subira na wananchi wa Ndanda wategemee kwamba barabara hii tunaenda kuikamilisha ili waendelee kupata huduma kama wananchi wengine katika maeneo ya Tanzania.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete iliahidi kujenga kwa lami barabara ya kutoka Kimara Mwisho kupitia Mavulunza – Bonyokwa Segerea hadi kuungana na barabara ya Nyerere yenye urefu wa Kilomita 4.7 na ambayo imekasimiwa kwa TANROADS:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo kwa lami kama ambavyo iliahidiwa miaka mitano iliyopita? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara hiyo ili kupunguza tatizo la foleni?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Pamoja na juhudi za Serikali za kuweka barabara nyingi za kupunguza msongamano katika Jiji la Dar es Salaam hatua ambayo naipongeza, lakini ninalo swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Nzasa - Kilungule kuungana na Buza ni muhimu sana kwa wakazi wa Mbagala katika kuondoa msongamano. Je, Serikali lini itaanza ujenzi wa barabara hiyo? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa amekuwa akifuatilia barabara nyingi lakini nimhakikishie kwamba katika harakati za kukwamua msongamano katika Jiji la Dar es Salaam barabara 12 zimekamilika. Ziko barabara 10 ambazo mpaka kufikia mwezi Aprili tunaendelea nazo lakini ziko barabara nyingine ambazo tutazishughulikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba Serikali iko committed kuhakikisha Jiji la Dar es Salaam linafunguka. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge hii barabara anayoizungumza kutoka Nzasa – Kilungule - Jeti Kona itashughulikiwa na mradi wa DMDP. Nitajaribu kufuatilia baada ya mkutano wa leo ili nione hatua ilivyo na nitampa mrejesho lakini niombe tu tuendelee kushirikiana na kupeana taarifa kwa sababu lengo la Serikali ni kurekebisha maeneo mbalimbali ili yaweze kupitika vizuri.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete iliahidi kujenga kwa lami barabara ya kutoka Kimara Mwisho kupitia Mavulunza – Bonyokwa Segerea hadi kuungana na barabara ya Nyerere yenye urefu wa Kilomita 4.7 na ambayo imekasimiwa kwa TANROADS:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo kwa lami kama ambavyo iliahidiwa miaka mitano iliyopita? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara hiyo ili kupunguza tatizo la foleni?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami naomba nimuulize Naibu Waziri swali ndogo la nyongeza. Kwa kuwa hizi barabara zimekuwa zikijengwa kwa gharama kubwa sana, halafu zinaharibika kwa muda mfupi, je, Serikali ina mikakati gani kuhakikisha wakandarasi wote wanaojenga barabara hizi wanachukuliwa hatua na kurudia ujenzi ili kuepusha kutumika tena gharama nyingine ya Serikali?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni kweli kuna baadhi ya maeneo baada ya barabara kutengenezwa zinaharibika, lakini ni hali ya kawaida kwa sababu ziko sababu nyingi ambazo zinaweza kusababisha miundombinu hii kuharibika. Ndiyo maana baada ya ujenzi wa barabara katika kipindi cha maisha ya barabara tunatenga fedha kwa ajili ya kufanya rehabilitation na baada ya miaka 20 tunafanya matengenezo makubwa kwa maana kwamba ule muda wa maisha ya barabara unakuwa umekwisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi kama Serikali…

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete iliahidi kujenga kwa lami barabara ya kutoka Kimara Mwisho kupitia Mavulunza – Bonyokwa Segerea hadi kuungana na barabara ya Nyerere yenye urefu wa Kilomita 4.7 na ambayo imekasimiwa kwa TANROADS:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo kwa lami kama ambavyo iliahidiwa miaka mitano iliyopita? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara hiyo ili kupunguza tatizo la foleni?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete alikuja jimboni na akaahidi ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kahama – Nyang’olongo – Bukwimba - Kalumwa - Busolwa hadi Busisi Sengerema na Rais wa Awamu ya Tano pia aliahidi hivyo hivyo. Je, Serikali ni lini itatenga fedha ya upembuzi yakinifu ili kuanza kuijenga barabara hiyo? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua hii barabara Mheshimiwa Mbunge tumezungumza mara nyingi, ni barabara ambayo inaenda kuunganisha pia katika Jimbo la Msalala kuja Kahama Mjini. Kwa hiyo, kama tulivyozungumza tutaangalia sasa namna nzuri tuweze kuiingiza kwenye usanifu, kwa sababu zile barabara ambazo zinakwenda kuunganishwa na barabara hii Mheshimiwa Mbunge, unajua ile barabara inayokwenda Geita ni muhimu sana kwamba tutaweza kuwa na kipande cha kwenda Sengerema. Ni kipande kifupi Mheshimiwa Mbunge kinahitaji commitment ya fedha siyo nyingi sana. Kwa hiyo, azidi kuvuta subira tutaendelea kutazama kwenye bajeti zinazokuja.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete iliahidi kujenga kwa lami barabara ya kutoka Kimara Mwisho kupitia Mavulunza – Bonyokwa Segerea hadi kuungana na barabara ya Nyerere yenye urefu wa Kilomita 4.7 na ambayo imekasimiwa kwa TANROADS:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo kwa lami kama ambavyo iliahidiwa miaka mitano iliyopita? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara hiyo ili kupunguza tatizo la foleni?

Supplementary Question 5

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana. Naomba nimuulize swali dogo Mheshimiwa Naibu Waziri. Barabara ya Kitunda – Kivule - Msongora mkandarasi yupo site kwa zaidi ya mwaka mzima sasa, lakini hajatekeleza kazi ile hata zaidi ya asilimia 20, amechimbachimba na kuiharibu. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kwenda Kivule ili akaangalie usumbufu ambao wananchi wanapata na kulazimisha ujenzi ufanyike haraka ili watu wapate barabara ya kupita?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niko tayari na inawezekana kesho pia…