Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:- Jimbo la Kigoma Kusini lenye ukubwa wa kilometa za mraba 10,178 lina jiografia mbaya na idadi ya wakazi wake ni kubwa sana:- a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuligawa jimbo hilo na kuanzisha halmashauri nyingine ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za kijamii kiurahisi? b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo katika Tarafa ya Nguruka?

Supplementary Question 1

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Natambua kwamba Jimbo la Kigoma Kusini linakidhi vigezo vyote vya kugawanywa na kuwa majimbo mawili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivi kwa sababu kwa mfano, Mkoa wa Katavi una kilometa za mraba 45,000 population 564,000. Jimbo hili la Kigoma Kusini lina vigezo vyote na tayari tulishafanya vikao kuanzia kwenye Vijiji, Kata, Baraza la Madiwani, DCC, vikao vikaenda mpaka kikao cha Mkoa kwa maana ya RCC na tayari tulipeleka Wizara ya TAMISEMI. Tume ya Uchaguzi mwaka 2015 waliliweka kwenye website yao kuonesha kwamba wako tayari sasa kuligawa, kama taratibu zote zilishafanyika na tulishawasilisha kwenye Wizara ya TAMISEMI, kwa nini walipotangaza majimbo mengine 2015 hawakuligawa jimbo hili?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Nguruka ilishafuata taratibu zote za kisheria na vigezo vyote inavyo kwa maana tuna kata nne na vigezo vya kisheria vinasema lazima tuwe na kata tatu. Je, kwa nini sasa Wizara ya TAMISEMI wasiamue tu rasmi kutangaza kwamba Mamlaka ya Mji wa Ngaruka sasa tayari inaweza kuanzishwa rasmi? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza, nina wasiwasi aliposema kwamba ana uhakika Jimbo la Kigoma Kusini limekidhi vigezo vyote, lakini nilipokuwa najibu swali la msingi nilizungumza kigezo kimojawapo ni ukubwa wa ukumbi wa Bunge. Sasa sijaelewa kama kigezo hicho nacho tayari kimefikiwa kwa kuangalia ukubwa na viti vilivyomo ndani ya Bunge kama kweli vinaweza vikakidhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nimhakikishie tu kwamba kwa mawasiliano zaidi na kuwapa uhakika wananchi wa Kigoma Kusini tutapeleka barua Tume ya Taifa Uchaguzi ili kusudi watupe mrejesho mzuri zaidi wa hatua ambayo imefikiwa mpaka sasa hivi. Nina uhakika 2020 bado iko mbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu Nguruka kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo, naomba sana arejee jibu langu la msingi nimesema kwamba vikao vinatakiwa vianzie kwenye Serikali ya Kijiji, Halmashauri ya Kijiji ikae ipeleke kwenye Mkutano Mkuu wa Kijiji upitishe, upeleke kwenye Kamati ya Maendeleo ya Kata iende kwenye Halmashauri, iende Mkoani ndio ije kwetu kwa ajili ya kumshauri Waziri mwenye dhamana na Waziri mwenye dhamana ni Rais. Kwa hiyo, itakapofika kwetu tutatoa ushauri, naomba sana awe na subira.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:- Jimbo la Kigoma Kusini lenye ukubwa wa kilometa za mraba 10,178 lina jiografia mbaya na idadi ya wakazi wake ni kubwa sana:- a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuligawa jimbo hilo na kuanzisha halmashauri nyingine ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za kijamii kiurahisi? b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo katika Tarafa ya Nguruka?

Supplementary Question 2

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Wilaya ya Tunduru ni miongoni mwa wilaya kubwa ina kilometa za mraba 18,786 sawa na Mkoa wa Mtwara wenye wilaya sita. Je, Serikali haioni wakati sasa umefika wa kugawa wilaya hiyo kulingana na majimbo yaliyopo, kuna Jimbo la Tunduru Kusini na Jimbo la Tunduru Kaskazini maeneo hayo sasa yakapata wilaya? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpe taarifa tu kwamba Jimbo la Sikonge ambako mimi natoka lina kilometa za mraba 27,873 sasa yeye kilometa za mraba 18,786 anaweza akasubiri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwape comfort wananchi wa Tunduru kwamba maeneo haya Serikali inafahamu kwamba ni makubwa, lakini kwa sasa hivi mzigo uliopo kwa Serikali ni kuhakikisha kwamba inaziwezesha wilaya mpya ambazo zimeanzishwa hivi karibuni, tuna wilaya kama sita ambazo zimeanzishwa hivi karibuni zipate majengo, vifaa vya uendeshaji, zipate watumishi, huo mzigo bado ni mkubwa sana na halmashauri mpya vilevile. Kwa hiyo, tukimaliza kuziwezesha hizi halmashauri mpya na wilaya mpya zikapata vifaa na majengo yakakamilika kabisa hapo ndiyo tutakuja kwa awamu nyingine sasa ya kuanzisha wilaya mpya na halmashauri mpya.

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:- Jimbo la Kigoma Kusini lenye ukubwa wa kilometa za mraba 10,178 lina jiografia mbaya na idadi ya wakazi wake ni kubwa sana:- a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuligawa jimbo hilo na kuanzisha halmashauri nyingine ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za kijamii kiurahisi? b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo katika Tarafa ya Nguruka?

Supplementary Question 3

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Wananchi wa Kata za Isaka, Mwalugulu, Isakajana pamoja na Mwakata walishakamilisha mchakato wa kuanzisha Halmashauri au Mamlaka ya Mji Mdogo wa Isaka na taratibu zote ambazo Mheshimiwa Naibu Waziri amezielezea hata hapa hadi kufika hatua ya kufika kwenye ofisi ya Waziri mhusika wameshafikia. Nataka kujua tu ni lini sasa hatimaye Mamlaka ya Mji Mdogo wa Isaka itaanzishwa?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Ezekiel Maige kwamba maombi ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Isaka yameshapokelewa, yanafanyiwa kazi, lakini tunawaomba wananchi wasubiri pale ambapo tutakuwa tayari mara moja tutatangaza.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:- Jimbo la Kigoma Kusini lenye ukubwa wa kilometa za mraba 10,178 lina jiografia mbaya na idadi ya wakazi wake ni kubwa sana:- a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuligawa jimbo hilo na kuanzisha halmashauri nyingine ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za kijamii kiurahisi? b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo katika Tarafa ya Nguruka?

Supplementary Question 4

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Manispaa ya Moshi Mjini tayari imekidhi vigezo vyote na kikubwa zaidi ina Mlima Kilimanjaro ambayo ni highest pick in Africa. Nataka kujua process inaendelea vipi mpaka sasa hivi bado hatujapata majibu?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, sijamwelewa vizuri Mheshimiwa Susan Lyimo kwa sababu Moshi tayari ni Manispaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, okay kuipandisha kuwa jiji. Pamoja na alivyosema kwamba imekidhi vigezo lakini bado hatujapata maombi rasmi kutoka kwenye vikao vinavyohusika kwa hivi karibuni….
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda kama anazungumzia maombi ya zamani lakini ya hivi karibuni hatujapata.