Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Serikali kupitia Mradi wa Mfuko wa Benjamin Mkapa ilidhamiria kujenga na kukamilisha huduma ya upasuaji kwenye Kituo cha Afya cha Kata ya Kala na baada ya mfuko huo kuacha shughuli zake hakuna juhudi inayoendelea. (a) Je, kuna mpango wowote kuendeleza nia hiyo njema? (b) Kwa kuwa kituo hicho kina upungufu mkubwa wa wataalam; je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi wakiwepo wauguzi?

Supplementary Question 1

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kunipa nafasi pamoja na majibu ya Serikali, naomba nieleze kwamba gari lililopo Kituo cha Afya Kala ni bovu sana na halifanyi kazi na Kala ipo umbali wa kilometa 150; hakuna mawasiliano yoyote ya simu wala barabara haifai. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza kwenye huduma za afya zinazotolewa kwenye vituo vyenye udau wa Serikali na wadau wengine, wananchi wa Kala wameamua kujenga kituo cha afya kwenye Kijiji cha King’ombe wao wenyewe, lakini vilevile wako wananchi wengine wameamua kujenga kutoka kwenye kata zao, Kata ya Ninde, Kata Kate na Kata ya Nkandasi. Je, Serikali iko tayari kuunga mkono juhudi hizi za wananchi?
Swali la pili Waziri wa Afya alipotembelea kwetu alituahidi kutupata shilingi milioni 400 kwenye Kituo cha Afya cha Wampembe na mpaka sasa sijaona fedha hiyo zimeonekana katika vitabu mbalimbali, lakini pia hatujazipokea; je, Serikali bado ina mpango huo wa kutupatia pesa katika Kituo hicho cha Wampembe? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue fursa hii kuwapongeza wananchi kwa dhati kwa moyo wao wa kujitoa kuhakikisha kwamba vinajengwa vituo vya afya baada ya kuona kwamba changamoto ya kuwa katika hivi vya ubia inawakabili. Katika Serikali kuunga jitihada za wananchi naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika pesa ambayo inatarajiwa kupatikana muda si mrefu Kituo cha Afya Kasu nacho ni miongozi mwa vituo vya afya ambavyo vinaenda kupatiwa fedha ili viweze kujengwa na kuweza kutoa huduma ambazo wananchi wanatarajia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili ameniambia kwamba Mheshimiwa Waziri wa Afya alivyoenda baada ya kuona changamoto kwa wananchi wa Wampembe aliahidi kituo hicho kingeweza kupatiwa jumla ya shilingi milioni 400 ili kiweze kupanuliwa. Naomba nimhakikishie kwamba ahadi hiyo bado ni thabiti ni suala la tu la muda, pesa ikipatikana hatutasahau.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwa ujumla wake naomba uniruhusu, unajua unapokuwa na Waheshimiwa Wabunge ambao wako kwenye Halmashauri moja na majimbo yako mawili ni sawa na ambavyo unapokuwa na watoto mapacha. Ni wajibu wako kuhakikisha kwamba unakuwa na balancing ambalo kama Serikali tunaenda kulifanya. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Serikali kupitia Mradi wa Mfuko wa Benjamin Mkapa ilidhamiria kujenga na kukamilisha huduma ya upasuaji kwenye Kituo cha Afya cha Kata ya Kala na baada ya mfuko huo kuacha shughuli zake hakuna juhudi inayoendelea. (a) Je, kuna mpango wowote kuendeleza nia hiyo njema? (b) Kwa kuwa kituo hicho kina upungufu mkubwa wa wataalam; je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi wakiwepo wauguzi?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetoa waraka wa kusitisha taratibu wa upandishwaji wa baadhi ya zahanati kwenda vituo vituo vya afya ikitaka vituo vya afya vijengwe kwenye kila kata, lakini kwamba Halmashauri zetu hazina fedha za uhakika za kujenga lakini hata wananchi wenyewe hali ya uchumi ni ngumu kuweza kujenga vituo hivyo vya afya.
Je, Serikali kwa nini msifikirie kwa upya kubatilisha uamuzi huo na kuangalia zile zahanati ambazo kwa kweli zinakidhi haja ziweze kupandishwa kuwa vituo vya afya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya suala zima la kupandisha zahanati kuwa vituo vya afya, kwanza naomba tukubaliane, zahanati zina ramani zake na vituo vya afya vina ramani zake. Hoja ya msingi ni kwamba tungependa wananchi wapate huduma ya afya jirani sana, naomba kwa sababu mpaka sasa hivi tulikuwa tunaongelea tuna asilimia 12 tu ya vituo vya afya na bado na uhitaji wa zahanati bado uhitaji ni mkubwa.
Naomba azma hiyo ya Serikali yakuhakikisha kwamba kila kijiji kinakuwa na zahanati na kila Kata kunakuwa na kituo cha afya bado ndio msimamo wa Serikali na wananchi waendelee kushiriki ili tuhakikishe kwamba huduma hii ina inawasogelea wananchi kwa karibu.