Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Kituo cha Afya cha Palestina kilichopo Kata ya Sinza alitangaza kukipandisha hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, bado Serikali inaendelea kuipatia fedha hospitali hiyo kama Kituo cha Afya. Je, ni lini Serikali itaitambua hospitali hiyo kama Hospitali ya Wilaya kwa kuipa fedha na vitendea kazi vinavyofanana na hadhi yake?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mara nyingi Mawaziri wetu hapa Bungeni wamekuwa wakituambia kwamba ahadi ya Rais ni sheria na lazima itekelezwe. Sasa kupandisha hadhi Kituo cha Afya cha Palestina kuwa Hospitali ni ahadi na agizo la Mheshimiwa Rais. Sasa ni kwa sababu gani badala ya Serikali kutekeleza ahadi hii, inafanya maboresho?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Kituo cha Afya cha Tarakea katika Wilaya ya Rombo kinachukua wagonjwa wengi sana kutokana na eneo kubwa na wagonjwa wengine kutoka nchi jirani ya Kenya, lakini hakina incinerator, hakina mortuary, vilevile kilikuwa hakina uzio lakini Mbunge akajitahidi kwa fedha za Mfuko wa Jimbo kujenga uzio.
Sasa je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufika Rombo kutembelea kituo kile ili tushauriane naye namna ya kukiboresha kiweze kuhimili idadi kubwa ya wagonjwa ambao wanakwenda kwenye kile kituo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi, Serikali tunakiri juu ya umuhimu wa Kituo cha Afya cha Sinza pale Palestina, lakini ni ukweli usiopingika kwamba ili Kituo cha Afya kiwe Hospitali ya Wilaya kuna suala zima la eneo ambalo katika jibu langu la msingi nimemwambia kwamba tunahitaji ekari 25. Sasa ukienda katika kile Kituo cha Afya cha Palestina, eneo hilo halipo na ndiyo maana katika maboresho ambayo yanaendelea ni pamoja na kutenga shilingi milioni 160 ili kuweza kuwa na hadhi ya kufanana na Kituo cha Afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli usiopingika kwamba tunapata changamoto katika Vituo vya Afya vilivyo Mijini, kitu ambacho kinakosekana ni jina lipi tutumie? Kwa sababu vinakuwa na hadhi zaidi ya Vituo vya Afya, lakini vinakuwa havijafikia kuwa Hospitali za Wilaya. Ndiyo maana nimesema kwamba ni vizuri Manispaa wakatenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Kwa hiyo, kama Serikali tuko tayari na wala hatupingani na kile ambacho Mheshimiwa Rais alielekeza kwa wakati ule, lakini changamoto ya ardhi ndiyo inayotusababisha tuseme kwamba ni vizuri likatengwa eneo lingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili, Mheshimiwa Selasini anataka utayari wangu kwenda kutazama Kituo cha Afya Tarakea. Naomba nimhakikishie, kama ambavyo nimefanya ziara kwenda Kituo cha Afya cha Kiaseri kule, niko tayari kufika hata Tarakea kwa kadri muda unavyokuwa umeruhusu.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Kituo cha Afya cha Palestina kilichopo Kata ya Sinza alitangaza kukipandisha hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, bado Serikali inaendelea kuipatia fedha hospitali hiyo kama Kituo cha Afya. Je, ni lini Serikali itaitambua hospitali hiyo kama Hospitali ya Wilaya kwa kuipa fedha na vitendea kazi vinavyofanana na hadhi yake?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto iliyopo Ubungo inafanana kabisa na changamoto iliyopo Jimbo la Mbulu Vijijini. Tuna kituo kimoja tu cha afya Jimbo zima; je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutuongezea angalau kituo kimoja ili katika huduma za afya jimboni, pakawa na hali ya kuwasaidia wananchi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto iliyopo kwenye Kituo cha Afya katika swali la msingi, ni suala la eneo, lakini kwake yeye eneo siyo tatizo kama ambavyo iko Sinza, Palestina pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba kwa dhati kabisa ya moyo wangu nimpongeze Mheshimiwa Flatei Massay kwa jinsi ambavyo amekuwa akilipigania Jimbo lake, amehakikisha kwamba Halmashauri inajengwa lakini pia ni miongoni mwa maeneo ambayo yanakwenda kujengewa Hospitali za Wilaya. Naomba nimhakikishie kwa dhati hiyo hiyo ambayo Serikali imeonesha kuhakikisha kwamba tunajenga Hospitali za Wilaya, ni azma yetu pia kuhakikisha kwamba tunajenga Vituo vya Afya vya kutosha na kwa kadri bajeti itakavyokuwa imeruhusu hakika hatutasahau eneo la kwake. (Makofi)

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Kituo cha Afya cha Palestina kilichopo Kata ya Sinza alitangaza kukipandisha hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, bado Serikali inaendelea kuipatia fedha hospitali hiyo kama Kituo cha Afya. Je, ni lini Serikali itaitambua hospitali hiyo kama Hospitali ya Wilaya kwa kuipa fedha na vitendea kazi vinavyofanana na hadhi yake?

Supplementary Question 3

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Katika mwaka wa fedha unaokuja, Serikali imetenga fedha za kujenga Hospitali za Wilaya kwenye maeneo 67, lakini pia ni wazi zipo Wilaya nyingi ambazo bado hazina Hospitali ya Wilaya ikiwemo Wilaya yangu ya Karatu. Ni lini sasa wananchi wa Karatu wategemee kujengewa Hospitali ya Wilaya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimekuwa nikijibu hapa, kuanza na Hospitali za Wilaya 67 tafsiri yake ni kwamba zikikamilika hizo tutakwenda kujenga nyingine. Ni azma ya Serikali inayoongozwa na CCM kuhakikisha kwamba Wilaya zote ambazo hazina Hospitali za Wilaya baada ya kumaliza hizi 67 tutakwenda hatua nyingine ya kwenda kuzijengea.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira, bajeti ndiyo imepita, tumwombe Mwenyezi Mungu makusanyo yetu yaende vizuri, tukimaliza 67 tutakwenda hatua ya pili.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Kituo cha Afya cha Palestina kilichopo Kata ya Sinza alitangaza kukipandisha hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, bado Serikali inaendelea kuipatia fedha hospitali hiyo kama Kituo cha Afya. Je, ni lini Serikali itaitambua hospitali hiyo kama Hospitali ya Wilaya kwa kuipa fedha na vitendea kazi vinavyofanana na hadhi yake?

Supplementary Question 4

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne, mwaka 2014 alipotembelea Jimbo la Tunduru Kusini alitembelea katika Kijiji cha Mbesa ambapo kuna Hospitali ya Mission pale. Hospitali ile inatoa huduma kubwa kuliko Hospitali ya Wilaya na Mheshimiwa Rais aliahidi kuipandisha daraja hospitali ile kuwa Hospitali Teule. Je, ni lini hospitali ile itapewa hadhi ya kuwa Hospitali Teule ili iweze kuendelea kutoa huduma vizuri?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni Hospitali ya Mission ya Mbesa.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimekuwa nikijibu na ambavyo nimejibu leo, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba maeneo ambayo hakuna Hospitali za Wilaya zinakwenda kujengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia ni azma ya Serikali kwa kushirikiana na Taasisi za Dini na Mashirika mengine pale ambapo sasa hivi hatuna Hospitali Teule, tunatumia zile ambazo zipo ili zifanye kazi kwa muda tu kama Hospitali Teule. Ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba tunakuwa na hospitali zetu za Serikali na zile za Mashirika ya Dini pale ambapo tutakuwa tumejenga za Serikali wabaki wakiendesha kwao na sisi Serikali tuwe na za kwetu tukifanya kazi kama Serikali. (Makofi)

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka tu kumshauri Mheshimiwa Mpakate, ili hospitali binafsi au ya Shirika la Dini ifanywe kuwa DDH sasa hivi tumeshusha madaraka haya kwenye Halmashauri husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Halmashauri ndiyo itafanya majadiliano na makubaliano na hospitali ile na tumeelekeza kuwe na mkataba wa muda maalum, kwamba Halmashauri ya Tunduru inaamua kuingia makubaliano na hospitali hii ili iwe Hospitali Teule ya Halmashauri na mkishakubaliana ndiyo mnaleta taarifa hizi TAMISEMI na Wizara ya Afya. Kwa hiyo, tutazitambua rasmi sasa kuwa ni Hospitali Teule ya Halmashauri husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, niseme tunatoka kwenye Hospitali za Wilaya, tunakwenda kwenye Hospitali ya Halmashauri. Kwa hiyo, sasa hivi kila Halmashauri itakuwa na Hospitali badala ya kuwa Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama kuna Wilaya zina Halmashauri mbili, zote zinapaswa kuwa na Hospitali ya Halmashauri ambayo ni ngazi ya kwanza ya Hospitali. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)