Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi zake ikiwemo ya Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni za kutoa maji Mto Zigi kwenda Muheza na Vijiji vyake? (b) Je, Serikali ina mpango gani zaidi ya huo wa kuwaletea maji wananchi wa Muheza?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI ADADI. M.RAJABU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza: Kwanza napenda kuwapongeza sana Mawaziri wote yeye Naibu Waziri ameshafika Muheza pamoja na Waziri mwenyewe wiki iliyopita Ijumaa alikuwa Muheza na ameonesha ishara kwamba kweli Muheza inakaribia kupata maji. Isitoshe pia Mwewe katika kipindi cha Clouds TV imesema kwamba Muheza itapata maji hivi karibuni.
Mheshimiwa Spika, mradi huu wa Zigi kutoa maji kutoka Mto Zigi mpaka Mjini Muheza ni kati ya miradi 17 ambayo tunategemea kupata mkopo wa Serikali ya India ya dola milioni 500. Nataka kujua mradi huu utaanza lini?
Mheshimiwa Spika, la pili, pale Muheza Halmashauri ya Wilaya imenunua mtambo wa kuchimba visima, lakini mtambo huu tunashindwa kuutumia kikamilifu kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Kwenye bajeti hii ya wakati huu tumepangiwa zaidi ya bilioni moja na tuna mpango wa kuchimba zaidi ya visima 50, Halmashauri imekwishapitisha.
Mheshimiwa Spika, nataka Waziri awahakikishie wananchi wa Muheza kwamba Urasimu utaondolewa, tunataka kuchukua kiasi cha fedha kutoka kwenye hiyo bilioni ambayo tumepangiwa ili tuweze kutumia mtambo huu ili tuweze kuchimba visima. Nataka Mheshimiwa Waziri awahakikishie wananchi kwamba urasimu huo utaondolewa na utasaidia ku-facilitate mipango hii iweze kuendelea.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri, lakini niwahakikishie wananchi wa Muheza wana Mbunge mfuatiliaji.
Mheshimiwa Spika, kwa kudhamiria kwa kutatua tatizo la maji kabisa katika Mji wa Muheza tumeona haja ya kuwekeza mradi mkubwa wa maji kati ya miradi ile 17 na utekelezaji wa maji inategemea na upatikanaji wa fedha. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mpaka sasa Serikali imeshasaini mkataba na ile Serikali ya India mradi wa mkopo wa milioni 500 katika kuhakikisha kwamba tunatatua tatizo la maji.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie yeye pamoja na wananchi wa Muheza wakati wowote mradi ule utaanza mara moja. Sisi kama Wizara ya Maji tutasimamia na kufuatilia fedha zile mradi uanze mara moja na kwa wakati katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili, kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo lakini tuwapongeze kwa kununua mtambo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge leo saa saba tukutane na Katibu Mkuu wa Maji ili katika kuhakikisha namna gani tunaweza tukawasaidia wananchi wa Muheza waondokane na tatizo hilo la maji katika kuhakikisha tunawaunga mkono. Ahsante sana. (Makofi)