Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA (K.n.y. MHE. EDWIN M. SANNDA) aliuliza:- Mtandao wa miundombinu ya usambazaji wa maji toka chanzo kikuu cha maji ya chemchem katika Jimbo la Kondoa Mjini ni ya zamani na chakavu. Katika ziara yake mwaka jana, Mheshimiwa Waziri Mkuu aliahidi kutupatia fedha za ukarabati wa miundombinu hiyo:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, kwanza tunaishukuru Serikali kwamba tumechimbiwa visima vinne kupitia Halmashauri ya Mji wa Kondoa. Pamoja na visima hivyo ambavyo vimechimbwa bila ukarabati wa miundombinu ya maji, uchimbaji wa visima hivi havitawasaidia sana wananchi wa Kondoa Mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo katika bajeti iliyopita tuliomba fedha kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu hiyo. Naomba kujua Serikali imetenga fedha kiasi gani kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya zamani ukizingatia kwamba maeneo kama Kwapakacha, Kilimani na Bicha katika uchimbaji wa visima hivyo kuna maeneo watatumia miundombinu ya zamani? Je, Serikali iko tayari kujenga baadhi ya miundombinu ili wananchi wa Kondoa Mjini wapate maji? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa ahadi ya ukarabati wa miundombinu ya maji katika Mji wa Kondoa ni ya ahadi ya viongozi wa Kitaifa na hasa waliotembelea Kondoa Mjini mwaka jana akiwemo Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, ahadi hizo zitatekelezwa lini? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ninavyosema mara nyingi, nia ya Serikali ni kuhakikisha kila eneo tunapeleka maji safi na salama. Kwa upande wa Kondoa Mjini sasa hivi tuna mradi ambao utahakikisha kwamba tunapeleka maji kila eneo la Kondoa Mjini ambapo kama nilivyosema kwenye swali la msingi kwamba sasa hivi tunajenga miundombinu ya kilomita 9.12, tunajenga miundombinu ya kusambaza maji kilomita 30.172 kwa sababu kuchimba visima ni jambo lingine na kuweka miundombinu ni jambo linguine. Kwa kulijua hilo, Serikali tunaendelea sasa hivi kujenga miundombinu hiyo tuhakikishe mwananchi kila eneo anapata maji safi na salama. Tunategemea mradi huu utamalizika hivi karibuni na wananchi watapata maji hayo.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA (K.n.y. MHE. EDWIN M. SANNDA) aliuliza:- Mtandao wa miundombinu ya usambazaji wa maji toka chanzo kikuu cha maji ya chemchem katika Jimbo la Kondoa Mjini ni ya zamani na chakavu. Katika ziara yake mwaka jana, Mheshimiwa Waziri Mkuu aliahidi kutupatia fedha za ukarabati wa miundombinu hiyo:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mji wa Kasulu ni kati ya miji ambayo inasubiri kwa hamu sana fedha za mkopo wa India katika ile miji 17. Hii ni kwa sababu Mji wa Kasulu unakabiliwa na tatizo la maji na hata machache yaliyopo ni machafu, kwa hiyo, kutibu tatizo hilo ni fedha za Mfuko wa India. Sasa niapenda kujua miradi hiyo 17 inaanza lini ikiwa ni pamoja na Mji wa Kasulu?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kasulu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tuna mradi mkubwa wa India ambapo siyo miji 17 sasa itakuwa miji 25 na mradi huo utagharimu shilingi za Kitanzania trilioni 1.2. Tenda ya kwanza ilitangazwa tarehe 17 Agosti, kwa ajili ya pre- qualification na consultancy na itafunguliwa tarehe 17 Septemba. Kwa Mheshimiwa Mbunge yeyote anayehitaji kujua information za mradi huu anaweza kupata kwenye website ya Benki ya Exim ya India. (Makofi)

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA (K.n.y. MHE. EDWIN M. SANNDA) aliuliza:- Mtandao wa miundombinu ya usambazaji wa maji toka chanzo kikuu cha maji ya chemchem katika Jimbo la Kondoa Mjini ni ya zamani na chakavu. Katika ziara yake mwaka jana, Mheshimiwa Waziri Mkuu aliahidi kutupatia fedha za ukarabati wa miundombinu hiyo:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Moshi Vijijini hali iko kama Kondoa, miundombinu mingi imejengwa siku nyingi na imechakaa. Kwa kutambua hilo, Mamlaka ya Maji (MUWSA) imefanya kazi kubwa ya kukarabati miundombinu hiyo katika Kata mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana kulikuwepo na mradi mmoja katika Kata ya Mabogini ambao ilikuwa inahusu vijiji vinne na Wizara ilipokuja kuzindua kwa kuona kazi kubwa iliyofanywa na MUWSA katika Kata zingine iliahidi kutoa shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya kuendelea kusambaza maji kwenye vijiji vingine vitano vya Mvulei, Muungano na Msarikia. Nataka kujua ni lini fedha hizo zitapelekwa MUWSA ili waweze kutekeleza ahadi hiyo?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Komu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakubaliana na yeye kwamba MUWSA inafanya kazi nzuri na tunawapongeza sana na tumewapa miradi mingi kwa ajili ya Moshi Vijijini na wanafanya kazi kubwa. Serikali tuko tayari wakati wowote wakituletea, kwa sababu tumeshawapa kibali cha kupeleka mkandarasi kuanza kufanya kazi hiyo na wakati wowote watakapoleta certificate kwa ajili ya malipo ya mkandarasi sisi tumejipanga vizuri na tutaweza kuwalipa ili kazi hiyo iendelee. Mheshimiwa Mbunge naomba uwasiliane na MUWSA kujua wamefikia wapi lakini sisi tuko tayari fedha tunayo wakati wowote tutaweza kuwalipa waendelee na kufanya kazi hiyo.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA (K.n.y. MHE. EDWIN M. SANNDA) aliuliza:- Mtandao wa miundombinu ya usambazaji wa maji toka chanzo kikuu cha maji ya chemchem katika Jimbo la Kondoa Mjini ni ya zamani na chakavu. Katika ziara yake mwaka jana, Mheshimiwa Waziri Mkuu aliahidi kutupatia fedha za ukarabati wa miundombinu hiyo:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. MAFTAH A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mtwara Mjini kuna Mradi wa Maji ambao unatekelezwa na Serikali kutoa maji Kijiji cha Lwelu kuelekea Kata za Ufukoni, Magomeni na maeneo mengine ya Mtwara Mjini lakini mkandarasi yule anasuasua sana na tayari kasha-rise certificate Wizara bado haijamlipa na mradi umesimama. Je, Serikali inatoa kauli gani ili kuhakikisha mkandarasi yule analipwa na mradi ule unaendelea haraka ili wananchi wa Mtwara Mjini wapate maji? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Mtwara Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuna miradi mingi hapa nchini inaendelea na huu mradi wa Mtwara tunaufahamu vizuri na kila mwezi sisi tunaendelea kulipa, hata leo tunafanya malipo kwa wakandarasi. Tutahakikisha kwamba na mkandarasi huyo tunamlipa ili aweze kuendelea kumaliza kazi hiyo ili wananchi wa Mtwara Mjini waweze kupata maji safi na salama. (Makofi)