Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Kilimo cha umwagiliaji katika Mji wa Bunda kimekuwa kikitengewa fedha kidogo sana kiasi cha kutokidhi mahitaji kazi husika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuiwezesha Ofisi ya Umwagiliaji ya Wilaya ili kufanya kilimo kuwa cha kisasa, endelevu na chenye kuleta tija kwa wananchi wa Bunda?

Supplementary Question 1

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Waziri katika majibu yake wataalam wanajibu kana kwamba bado Halmashauri ni moja lakini tuna Halmashauri mbili; Halmashauri ya Wilaya ina majimbo mawili ya Mwibara kwa Mheshimiwa Kangi na Bunda kwa Mheshimiwa Boniphace; Halmashauri ya Mji ina Jimbo moja tu la Ester Bulaya, Bunda Mjini. Sasa haya majibu waliyompa ni ya enzi zile za babu, za Wasira, sio kipindi hiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nauliza maswali yangu mawili ya nyongeza. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu alipofanya ziara kwenye Jimbo langu la Bunda alitembelea Kikundi cha Igebesabo kilichopo Kata ya Nyatwali ambacho kina mradi mkubwa wa umwagiliaji uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 700. Pale wana changamoto ya mashine kubwa ya kusukuma maji ambayo yanatoka Ziwa Viktoria aliwaahidi atawasaidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini ahadi hii itatekelezwa kwa sababu pia katika hicho kikundi kuna vijana kama wewe Mheshimiwa Waziri?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Idara ya Umwagiliaji ina changamoto nyingi ikiwepo ya bajeti na vitu vingine, lakini kwa sasa hivi hawana gari la kuweza kufanya patrol katika miradi mbalimbali ya umwagiliaji katika Wilaya nzima ya Bunda. Ni lini sasa watawapatiwa gari ili sasa kilimo cha umwagiliaji Bunda kiweze kushamiri na vijana wengi graduates sasa hivi wamejiajiri wenyewe kwenye shughuli za umwagiliaji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze kwa maswali mazuri lakini kubwa ambalo nataka nimhakikishie, ahadi ni deni. Kwa kuwa hii ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo katika kuhakikisha tunaitimiza kwa wakati ili wananchi wake, kwa maana ya kile kikundi, waweze kupata mashine hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu suala zima la gari, ili mradi uwe bora na wenye tija kwa wananchi lazima kuwe na usimamizi na ufuatiliaji wa karibu. Kwa hiyo suala la gari ni jambo la muhimu sana. Niagize wataalam wetu wa Bunda kufuatilia kitendea kazi hiki na sisi kama Wizara ya Maji tutatoa ushirikiano wa dhati kabisa katika kuhakikisha kinapatikana.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Kilimo cha umwagiliaji katika Mji wa Bunda kimekuwa kikitengewa fedha kidogo sana kiasi cha kutokidhi mahitaji kazi husika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuiwezesha Ofisi ya Umwagiliaji ya Wilaya ili kufanya kilimo kuwa cha kisasa, endelevu na chenye kuleta tija kwa wananchi wa Bunda?

Supplementary Question 2

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Skimu ya Mwakijembe ambayo imetumia fedha nyingi kujengwa, zaidi ya shilingi bilioni moja, mpaka leo hii haijakamilika kwa kukosa mifereji ya umwagiliaji lakini vilevile kukosa bwawa na sasa tunashuhudia maeneo ya wananchi yakichukuliwa na Jeshi bila fidia yoyote. Je, Waziri yuko tayari kuja kufanya ziara mahsusi Jimboni Mkinga ajionee hali hii ili kuweza kutatua tatizo linaloikabili skimu ile?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie kaka yangu, Mheshimiwa Dunstan Kitandula, mimi kama Naibu Waziri wa Maji nipo tayari.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Kilimo cha umwagiliaji katika Mji wa Bunda kimekuwa kikitengewa fedha kidogo sana kiasi cha kutokidhi mahitaji kazi husika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuiwezesha Ofisi ya Umwagiliaji ya Wilaya ili kufanya kilimo kuwa cha kisasa, endelevu na chenye kuleta tija kwa wananchi wa Bunda?

Supplementary Question 3

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wakulima wa mbogamboga wa Wilaya ya Lushoto wanachimba vidimbwi vidogovidogo kwa ajili tu ya kunyeshea mazao yao. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha kwa kuwajengea mifereji hasa wakulima wa mabondeni hasa Mabonde ya Boheloi, Mshizii, Kwai, Milungui, Ubiri, Kwekanga, Mazumbai, Mlola, Mboi hadi Makanya?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, kaka yangu, Mheshimiwa Shekilindi (Bosnia), kwa kazi nzuri anazozifanya katika Jimbo lake la Lushoto. Kubwa ambacho nataka nimwambie ni kwamba nchi yetu sasa hivi tunakwenda katika uchumi wa kati, tumeona haja sasa ya kulima kilimo cha umwagiliaji. Nimhakikishie kwamba sisi Wizara yetu ya Maji tumetenga shilingi bilioni 29.767 katika kuhakikisha tunawekeza katika kilimo cha umwagiliaji. Niwaombe tu wataalam wetu wa Lushoto wasilale, wamsaidie Mheshimiwa Mbunge katika kuhakikisha jambo lake linatimilika kwa wakati.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Kilimo cha umwagiliaji katika Mji wa Bunda kimekuwa kikitengewa fedha kidogo sana kiasi cha kutokidhi mahitaji kazi husika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuiwezesha Ofisi ya Umwagiliaji ya Wilaya ili kufanya kilimo kuwa cha kisasa, endelevu na chenye kuleta tija kwa wananchi wa Bunda?

Supplementary Question 4

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya Mawaziri wa Wizara hii kutembelea chanzo cha maji cha Mto Qangded kule Karatu ambacho kinatumiwa na wananchi katika kilimo cha umwagiliaji zaidi ya vijiji sita. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, yuko tayari sasa kutimiza ahadi yake ya kutembelea eneo hilo ili kutatua changamoto ambazo wakulima wa eneo hilo wanakumbana nazo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nilihakikishie Bunge lako niliahidi kwenda kutembelea Jimbo la Karatu lakini kutokana na changamoto sikuweza kufanikisha ahadi ile. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kabla ya Bunge la Novemba tutatimiza ahadi ile kwa kuhakikisha tunatembelea miradi katika jimbo lake.