Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:- Zipo benki zinazotoa mikopo ya kilimo hususan Benki ya Kilimo Tanzania:- Je, kwa upande wa Zanzibar ni wananchi wangapi wanaofaidika na mikopo ya kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na maswali mawili ya nyongeza.
Je, Serikali inatumia vigezo gani kwa wananchi kupata hiyo mikopo?
Swali la pili, atakubaliana na mimi Mheshimiwa Naibu Waziri akiongozana na watalaam wake waende Jimboni kwangu kwenda kutoa elimu na kwa sababu wananchi wanataka kukopa fedha hizi ili wananchi na wao waondokane na umaskini. Je, Serikali lini watakwenda Jimboni kwangu Bububu ili kwenda kutoa mikopo? Ahsante.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lako la kwanza kuhusu vigezo, kigezo kikubwa ambacho benki yetu ya kilimo inaangalia ili iweze kumkopesha mkulima ni kuangalia kama mradi ule unaotekelezwa na mkulima unaweza kukopesheka yaani valuable agricultural activity ambayo inaweza akawekeza na akapata faida yake na akaweza kurejesha mkopo huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakatika hili ndio maana Benki Kuu imetoa maelekezo kwa mabenki yetu yote kuhakikisha kwamba wakopeshwaji ambao wanaomba mikopo wanakuwa ni wale ambao taarifa zao zinaonesha wameweza kukopa na wakarejesha mikopo ili kuondokana na tatizo la mikopo chechefu ambayo mabenki yetu mengi yanapambana nayo. Serikali yetu ya Awamu ya Tano imepanga kuhakikisha wakulima wetu wanafikiwa na mikopo hii ya benki ya kilimo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, namuahidi Mheshimiwa Mwantakaje baada ya Bunge hili mimi na watalaam wangu wa Benki yetu ya Kilimo tutakuja Jimboni kwako Bububu kuja kuwatembelea wakulima wa Bububu. (Makofi)