Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA (K.n.y. MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI) aliuliza:- (a) Je, Mfuko wa Bima ya Afya una wanachama wangapi na ni asilimia ngapi ya Watanzania wamejiunga na bima hiyo? (b) Je, kwa nini baadhi ya hospitali, hasa za binafsi, hazikubali malipo kwa kutumia kadi hizo za Bima ya Afya? (c) Je, Mfuko wa Bima ya Afya umefikia malengo ya kuanzishwa kwake?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini nina swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu zinaonesha kwamba, bado asilimia ni ndogo sana ya watumizi wa mfuko huu. Je, Serikali ina mikakati gani ya kuwaelimisha Wananchi, ili aweze kujiunga na mfuko huu?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunatambua kwamba bado idadi kubwa sana ya Watanzania hawajafikiwa na huduma ya bima ya afya, lakini tunatambua vilevile gharama za matibabu zinazidi kuongezeka. Kwa hiyo, sisi kama Serikali tunaendelea kupanua wigo wa vifurushi vyetu ili kuhakikisha kwamba tunaweza kuwafikia Watanzania wengi zaidi, lakini sambamba na hilo tunaendelea kuboresha vifurushi, lakini tunaboresha vilevile utaratibu wa wananchi kuweza kuchangia na moja ya mkakati tunaoufikiria ndani ya Serikali ni utaratibu wa jipimie, ambapo mwananchi atakuwa anachangia kadiri kipato chake kinavyoruhusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mkakati wa muda mrefu ambao tunaendelea kuufanyia kazi, dunia ya sasa imeelekea katika Mpango wa Bima ya Afya kwa wananchi wote na sisi kama Tanzania tumeridhia azimio hilo la kidunia na sasa hivi tuko katika mchakato wa kuandaa muswada wa sheria ambao utafanya bima ya afya kuwa ni kwa lazima kwa Watanzania wote.

Name

Saada Salum Mkuya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA (K.n.y. MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI) aliuliza:- (a) Je, Mfuko wa Bima ya Afya una wanachama wangapi na ni asilimia ngapi ya Watanzania wamejiunga na bima hiyo? (b) Je, kwa nini baadhi ya hospitali, hasa za binafsi, hazikubali malipo kwa kutumia kadi hizo za Bima ya Afya? (c) Je, Mfuko wa Bima ya Afya umefikia malengo ya kuanzishwa kwake?

Supplementary Question 2

MHE. SAADA SALUM MKUYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana kwa kuniona na mimi nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri na ya ufasaha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba kwa upande wa Zanzibar majimbo mengi tulijikusanya na tukawa tumewalipia bima ya afya watu mbalimbali, lakini baadae Mfuko huu wa NHIF ukasitisha kile kifurushi. Na sasa hivi nadhani karibu miaka miwili tunaambiwa assessment inaendelea ili kuona kwamba tunapata alternative ya ile bima ya afya ambayo ilikuwa imesitishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mpaka lini au lini sasa hii assessment itakamilika ili tuje na mpango mpya tuweze kuwahudumia wananchi wetu katika majimbo yetu ambao wanahitaji hii huduma ya afya kupitia Bima ya Afya?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kulikuwa kuna utaratibu wa kutoa bima ya afya kupitia vikundi, lakini kusudio lile naomba labda nianze kutoa maelezo ya awali ili Waheshimiwa Wabunge nanyi mnielewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mara nyingi tunapokuwa tunazungumzia suala la bima tunwataka watu wanaojiunga ni wale ambao hawana magonjwa pale wanapokuwa wanaanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni sawasawa unataka kukata bima wakati gari lako limepata ajali. Sasa baadhi ya watu kilichotokea ni kwamba kuna vikundi vilikuwa vinajikusanya ambavyo tayari wana magonjwa makubwa na ya muda mrefu wanatengeneza vikundi, wanalipa hela ndogo shilingi 70,000 halafu wanaenda sasa hospitalini wanapata huduma kubwa, kwa utaratibu huo tungeweza tukaufilisi mfuko.
Kwa hiyo, baada ya kubaini kwamba, kulikuwa na changamoto hiyo, tulisitisha hilo fao, ili kuweza kupitia taratibu nzuri za kutengeneza vile vikundi na vigezo vya kuzingatia kwa hiyo, bado hiyo kazi inaendelea kufanyika na tutakapokamilisha tutautangaza upya utaratibu mpya wa kujiunga na vikundi hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suluhu ya kudumu, sisi kama Serikali tuko katika hatua ya mwisho ya kuandaa muswada na utakapokamilika ndani ya Serikali tutauleta hapa Bungeni na mimi niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge mtuunge mkono katika muswada huo.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA (K.n.y. MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI) aliuliza:- (a) Je, Mfuko wa Bima ya Afya una wanachama wangapi na ni asilimia ngapi ya Watanzania wamejiunga na bima hiyo? (b) Je, kwa nini baadhi ya hospitali, hasa za binafsi, hazikubali malipo kwa kutumia kadi hizo za Bima ya Afya? (c) Je, Mfuko wa Bima ya Afya umefikia malengo ya kuanzishwa kwake?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na niseme wazi nimeyaelewa sana majibu ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na majibu hayo mazuri na ufafanuzi huo, wanawake wa Mkoa wa Kilimanjaro wamehamasika sana kwenye SACCOS na sio vikundi vya ambao wameshapata maradhi tayari, bali ni vikundi vya akinamama ambao wanafundishana mambo mengi ikiwemo ujasiriamali, scheme za elimu pamoja hiyo kujiunga na NHIF. Ni muda mrefu sasa toka mwaka jana wameandikiwa barua kusitisha zoezi hilo, lakini kwao imekuwa ni usumbufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Naibu Waziri haoni kwamba itakuwa sasa ni usumbufu wale akinamama kurudi kuanza upya, badala ya kuweka muendelezo kwamba walikuwepo kwenye NHIF na waendelee?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa sina maelezezo kamili kuhusiana na hivi vikundi vya Mkoa wa Kilimanjaro ambavyo Mheshimiwa Mbunge anaviongelea, mimi nimuombe sana Mama Shally Raymond baada ya Kipindi cha Maswali na Majibu tuonane anipe maelezo na mimi nimtume Meneja wangu wa NHIF Mkoa wa Kilimanjaro aende akavitembelee na kuvikagua vikundi, kwa sababu tunapozungumzia vikundi vya washirika na vikundi hivi vya SACCOS ni vikundi ambavyo na sisi tumekuwa tunavihamasisha vijiunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichotaka tuweze kupata maelezo kidogo tuweze kubaini changamoto zilizopo na tuweze kuchukua hatua kwa haraka zaidi.

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA (K.n.y. MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI) aliuliza:- (a) Je, Mfuko wa Bima ya Afya una wanachama wangapi na ni asilimia ngapi ya Watanzania wamejiunga na bima hiyo? (b) Je, kwa nini baadhi ya hospitali, hasa za binafsi, hazikubali malipo kwa kutumia kadi hizo za Bima ya Afya? (c) Je, Mfuko wa Bima ya Afya umefikia malengo ya kuanzishwa kwake?

Supplementary Question 4

MHE. NURU AWADHI BAFADHIL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kuwa wananchi wengi wamehamasika katika kujiunga na bima ya afya, wananchi hawa wanapofika hospitalini daktari anaweza akamuandikia dawa moja paracetamol nyingine anaambiwa akanunue. Je, Serikali inatwambiaje kuhusu hawa Wananchi wanaoambiwa wakanunue wakati wao wamejiunga na Bima ya Afya, ili waepuke makali ya maisha? Ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano imeongeza bajeti ya dawa kutoka shilingi bilioni 30 hadi shilingi bilioni 270 katika bajeti ambayo tumeipitisha mwezi Julai mwaka huu; hali ya upatikanaji wa dawa nchini sasa hivi ni zaidi ya 90%; lakini sambamba na hilo mwezi Februari tulitoa mwongozo wa utoaji huduma za afya na aina za dawa ambazo zitatumika katika kila ngazi kwa aina ya ugonjwa na orodha hii tumejaribu kuihuisha pamoja na wenzetu wa Bima ya Afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo tumeanzisha utaratibu wa maduka ya dawa muhimu ambazo haziko katika orodha yetu ya dawa zile muhimu ambazo ni 167 ili yale maduka yaweze kutoa dawa zile ambazo ziko nje ya utaratibu wetu wa hizi standard treatment guideline lakini zinahitajika katika utaratibu wa bima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe na nimhakikishie Mbunge kuwa tunaendelea kuboresha mfumo huu kuhakikisha kwamba dawa zote ikiwa na zile ambazo zilikuwa zinahitajika kwa wagonjwa wa bima zinapatikana katika hospitali zetu za umma.