Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Je, Kiwanda cha Sukari Kagera tangu kimepata mwekezaji mpya baada ya kile cha mwanzo kushindwa kuendelea na uzalishaji kimetoa mchango gani kwa Wilaya ya Misenyi, Mkoa wa Kagera na Taifa kwa ujumla?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri yaliyotolewa na Mheshimiwa Waziri ambayo na mimi nakubaliana nayo, lakini mafanikio haya yapo hatarini kupotea kabisa ama wafanyabiashara wasio waaminifu wataendelea kungiza sukari nchini kama wanavyofanya hivi sasa na kufanya repackaging ya sukari hiyo kwenye mifuko wakisingizia kwamba imezalishwa hapa nchini wakati sio. Na hivyo kusababisha viwanda kukosa soko kama ambavyo inatokea kwa Kagera Sugar hivi sasa wamezalisha sukari, imejaa kwenye maghala, hawana sehemu ya kuiuza. Je, Serikali inalitambua hilo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kama Serikali inalitambua hilo ni hatua zipi inazichukua kuhakikisha usemi wa kwamba Tanzania tunajenga Tanzania ya viwanda, tujenge kweli Tanzania ya viwanda kwa kulinda viwanda vyetu, lakini si kusema tunasema tunajenga ya viwanda huku tukiruhusu wafanyabiashara wasio waaminifu wanaingiza sukari ndani ya nchi, na wanafanya repackaging wanaua viwanda vyetu?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunayo sukari nyingi kwenye viwanda vyetu. Kiwanda cha Kagera Sugar kina sukari na imerundikana nje kama ambavyo mmeona kwenye vyombo vya habari. Hali ni hiyo hiyo Kilombero na TPC. Kwa majibu ya swali la kwanza na la pili Serikali tunatambua na kikosi maalum cha Serikali kinafuatilia na kwa ruhusa yako ningeomba nisiende zaidi kwa sababu katika kinachofanyika kuna jinai ndani yake na vyombo vya dola vinafuatilia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuwambia wawekezaji wote wa viwanda vyetu Serikali inawafuatilia na itawalinda na wale wanaochezea viwanda vyetu nataka niwahakikishie uchunguzi ukikamilika tutachukua hatua kali. Fair Competition wako kazini, TFDA wako kazi, TAKUKURU wako kazini na watu wa TRA wako kazini. Ni timu makini na niwaeleze kwa utangulizi hili suala lina jinai na anayehusika atakiona cha moto. (Makofi)

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Je, Kiwanda cha Sukari Kagera tangu kimepata mwekezaji mpya baada ya kile cha mwanzo kushindwa kuendelea na uzalishaji kimetoa mchango gani kwa Wilaya ya Misenyi, Mkoa wa Kagera na Taifa kwa ujumla?

Supplementary Question 2

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni muunganiko wa nchi mbili na unapotaja viwanda vya Tanzania huwezi kuvitenga viwanda vilivyoko Zanzibar. Nataka kujua ni sababu ipi ya msingi inayoifanya Kiwanda cha Sukari cha Mahonda – Zanzibar kisiruhusiwe kuingiza sukari yake katika soko la Tanzania Bara, sababu ya msingi hasa ni ipi?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili swali limekuwa likijirudia mara kwa mara, lakini niseme tu kwamba pamoja na kwamba Tanzania ni moja, suala la ulinzi wa viwanda lipo kila mahali na kama ulivyoona hata Tanzania Bara imerundikana sukari ya kutosha. Kwa hiyo, pengine badala ya kutaka nyingine iingie tushughulikie kwanza hii hali mbaya ya kuingiza sukari ya magendo inayoendelea.

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Je, Kiwanda cha Sukari Kagera tangu kimepata mwekezaji mpya baada ya kile cha mwanzo kushindwa kuendelea na uzalishaji kimetoa mchango gani kwa Wilaya ya Misenyi, Mkoa wa Kagera na Taifa kwa ujumla?

Supplementary Question 3

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimuombe tu Mheshimiwa Naibu Waziri anisikilize kwa makini kabisa, ninachokizungumza ni Kiswahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri, Muungano wetu huu tumeungana watu nchi mbili, Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Watu wa Tanganyika ndiyo maana jina likapatikana likaitwa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenkiti, kati ya mambo waliyokubaliana yalikuwa ni biashara na viwanda na swali la msingi linahusu viwanda vilevile. Nataka sababu za msingi nijue Kiwanda cha Sukari cha Mahonda hata Wabunge tungesimama mara nyingi mjue kuwa hili suala limetukwaza ndani ya moyo wetu. Bidhaa zinazotoka Tanzania Bara zinakwenda Zanzibar bila kigugumizi, leo viwanda vya Zanzibar kuzalisha na hii Jamhuri inaitwa Tanzania hebu tuelezeni ukweli Kiswahili tuweze kufahamu kwa nini maziwa ya Bakhresa hayawezi kufika hapa yanakwama na huku tukishuhudia wakati mwingine sukari inatoka nje mnaacha kununua kutoka Zanzibar. sababu gani zinasababisha bishaa hizo kupata kigugumizi. Za Tanzania Bara zinaingia Zanzibar, za Zanzibar kuja huku imekuwa kitendawili? (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo Kamati kati ya Waziri wa Biashara wa Tanzania (mimi) na mwenzangu wa Zanzibar. Yamekuwepo malalamiko ya wafanyabiashara na kupitia vikao hivyo tunakaa chini na kujadili suala la Kiwanda cha Maziwa cha Bakhresa kilichopo Zanzibar mimi mwenyewe nimekwenda nikakiangalia. Nikakitembelea kiwanda kile, nikaangalia uzalishaji wao ni mzuri na maziwa yamekuwa yanaingia. Tulichokubaliana ni kwamba mtu anapopata tatizo la kukwazwa na watendaji ilitolewa namba maalum na kikao cha Mawaziri wawili kwamba anayekwamishwa awasiliane na mamlaka. Kama kuna tatizo kuhusu maziwa mnijulishe mimi kusudi mimi niende kuwa-task wale wanaohusika. Lakini hao wawekezaji wenye viwanda napenda nikiri kwamba ninashughulika nao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije kwenye Kiwanda cha Sukari cha Mahonda. Serikali imeamua kusimamia Sekta ya Sukari kwa sababu kupitia sukari tunataka kuzalisha ajira. Kwa sababu ya nia ya kuzalisha ajira na kwa sababu ya fursa ya ajira katika sekta ya sukari hii sukari ni classified product na sasa hiyo Tume ninayowaeleza ikimaliza kazi ndiyo mtakuja kujua maana ya classified product kwamba sukari inakuwa classified. Kiwanda cha Mahonda wake wa kuzalisha ni tani 4,000 mahitaji ya Zanzibar ni tani 20,000. Mimi nawasiliana na watu wa Zanzibar, Waziri wa Zanzibar kwamba azalishe 4,000 auze kwao. Ndiyo!
…ninachozungumza ndiyo…, ngoja niwaeleze…
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Waheshimiwa Wabunge wanataka kujua ninachokisema.
Ningeomba muwape fursa wale wanaotaka kunisikiliza niwaeleze suala la Mahonda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niku-address wewe Mahonda inazalisha tani 4,000. Itakapokuwa imezalisha tani 4,000 inataka kuziuza katika soko la Tanzania Bara haitazuiliwa, tutakaa chini tuzungumze, lakini huwezo kuwa unazalisha tani 4,000 lakini wewe soko lako ni tani 20,000 halafu wewe unakwenda kuuza tani 4,000 nje hizi nyingine unazipata wapi? Kwa hiyo, ndiyo utaratibu huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa taarifa katika Bunge, tunataka ku-classify sukari. Mafuta ya kula ni classified, sukari itakuwa classified kwa sababu tunataka ajira. Niko tayari kulisimamia hilo mpaka nitakapoambiwa vinginevyo. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:- Je, Kiwanda cha Sukari Kagera tangu kimepata mwekezaji mpya baada ya kile cha mwanzo kushindwa kuendelea na uzalishaji kimetoa mchango gani kwa Wilaya ya Misenyi, Mkoa wa Kagera na Taifa kwa ujumla?

Supplementary Question 4

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Nashukuru kwa majibu ya Wizara kwa maswali yote yaliyopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapata miaka kadhaa sasa bidhaa hii ya sukari nchini inapanda bei kila inapofika mwezi wa tatu na inampa wakati mgumu mlaji katika gharama kulingana na hali ya uchumi ya Mtanzania wa chini.
Je, ni kwa nini Serikali isitazame namna ya kuzalisha sukari hii ikamudu katika ule muda wa sukari kupanda kila mwaka kuanzia mwezi wa tatu ili kila Mtanzania kwa wakati mmoja aweze kupata bidhaa hii kwa bei nafuu? (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba wawekezaji au wazalishaji wa sukari ni wafanyabiashara binafsi na Serikali imekuwa haiwaingilii sana katika upangaji wa bei, lakini tunawaomba fursa hii wanayoipata ya kulindwa wasiitumie vibaya. Tumefanya hivyo kwa viwnada vya saruji, tumeelewana vizuri na ninatoa rai kwao iwe ni mwiko kupandisha sukari kiholela.