Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Wananchi wanaoishi katika maeneo yanayopakana na hifadhi za misitu katika Wilaya ya Urambo wamepitia migogoro mingi ya mipaka na hata kuchomewa nyumba na mali:- Je, ni lini Serikali itamaliza migogoro ya mipaka katika Kata za Nsenda, Uyumbu na Ukondamayo ili wananchi waendelee na kilimo pamoja na shughuli nyingine za kuwaletea maendeleo?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARETH S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Awali ya yote namshukuru Naibu Waziri alifika mwenyewe na kujionea utata uliopo, kati ya mipaka iliyowekwa. Kuna mipaka miwili, wa zamani na wa sasa, ambayo imesababisha wananchi kutolewa kwa nguvu na hata kupoteza mali zao. Swali la kwanza; kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alifika yeye mwenyewe na kujionea utata uliopo anasemaje kuhusu utata ambao aliuona?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufuatana na mimi kwenda kukaa kumaliza kabisa utata uliopo pale ili wananchi waendelee na shughuli zao?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi kumpongeza sana Mheshimiwa Margaret Sitta kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya katika kuhakikisha kwamba anasimamia uchangishaji wa fedha kwa ajili ya vyoo vya mfano katika shule zetu katika majimbo yote. Nakupongeza sana mama yangu kwa kazi nzuri ambayo umekuwa ukiifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nitumie nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akilifuatilia hili suala kwa muda mrefu. Nakumbuka mimi mwenyewe nilifika katika lile eneo kweli, tuliangalia utata wa mipaka iliyopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia agizo la Bunge la mwezi wa Sita katika kipindi cha bajeti tulikubaliana kwamba mipaka yote lazima iwekwe kwa ushirikishwaji wa wananchi, viongozi, Wizara ya Ardhi pamoja na Maliasili. Kwa hiyo, nasema tu kwamba, tuko tayari tutashirikiana na Wizara zinazohusika na wadau mbalimbali kuhakikisha utata wa migogoro ya mipaka iliyopo unatatuliwa mara moja na wananchi wanaendelea kufanya kazi zao kwa amani na utulivu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, niko tayari kabisa kufuatana naye lakini wakati nitakapofuatana naye nitaomba kwamba twende pamoja na Waziri wa Ardhi ili tuweze kuhakikisha kwamba wote tunajionea uhalisia uliopo katika eneo hilo.

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Wananchi wanaoishi katika maeneo yanayopakana na hifadhi za misitu katika Wilaya ya Urambo wamepitia migogoro mingi ya mipaka na hata kuchomewa nyumba na mali:- Je, ni lini Serikali itamaliza migogoro ya mipaka katika Kata za Nsenda, Uyumbu na Ukondamayo ili wananchi waendelee na kilimo pamoja na shughuli nyingine za kuwaletea maendeleo?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza napenda kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri, alifanya ziara Mkoa wetu wa Lindi kuja kumaliza mgogoro wa mpaka wa Kikulyungu Wilaya ya Liwale lakini na mpaka wa Selous na Wilaya ya Kilwa. Kwa bahati mbaya sana kwa dharura iliyojitokeza Mheshimiwa Naibu Waziri alishindwa kukamilisha ile kazi. Sasa ningependa kujua ni lini Serikali itakuja sasa kumaliza ule mgogoro ili wananchi wa Kikulyungu na wananchi wa Wilaya ya Kilwa waendelee kufanya shughuli zao? Ahsante sana.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabla ya kujibu naomba niseme kweli kwamba nilikuwa nimeenda kwenye lile eneo hasa katika Wilaya ya Liwale kwa ajili ya kushughulikia ule mgogoro ambao upo katika Kijiji cha Kikulyungu. Bahati mbaya siku ile wakati tunajipanga kuelekea kule ndiyo siku ambapo Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii alipata ajali kwa hiyo nikalazimika kuahirisha ile safari ndiyo maana sikuweza kufika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na Maafisa mbalimbali wa kutoka Wizara ya Ardhi na Wizara ya Maliasili walienda katika eneo husika walikaa na wananchi wakatoa elimu na wananchi wakawapokea na wakawa sasa kwamba wako tayari sasa kushirikiana kwa pamoja ili kuweza kubaini mpaka uliopo na kuondoa huo mgogoro ambao umedumu kwa miaka mingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie nafasi hii kusema kwamba, sasa tuko tayari wakati wowote tena tutarudi kuhakikisha kwamba sasa tunashirikiana na wananchi katika kuonesha mipaka ya eneo hilo husika na Mheshimiwa Mbunge utashirikishwa kikamilifu katika hilo suala.