Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa wakulima 435 wa kahawa waliodhulumiwa katika Jimbo la Buhigwe?

Supplementary Question 1

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri wa Kilimo kwa majibu mazuri na kihakika kama Wizara wanaonesha wanalitambua suala hili vizuri. Kwa hilo, nawapongeza sana kwa majibu haya.
Mheshimiwa Spika, kuanzia 2011 - 2018 ni miaka saba sasa, hawa wakulima 435 wanaodai zaidi ya milioni 150 au Dola 74,000 bado wanadai. Kwa kuwa Bodi ya Kahawa ilifanya makosa kumlipa mtu mwingine na Mheshimiwa Waziri amekiri kwenye majibu yako kwamba iko kwa Mwanasheria, wakulima hawa wanataabika na hii ni Serikali ya wakulima, ni lini fedha hizo zitapatikana na Mwanasheria ataweza kuliharakisha suala hili?
Mheshimiwa Spika, la pili kwa kuwa hii inatokana na matatizo ya soko hili la kahawa, ni mkakati gani uliopo wa bei na masoko ya kahawa kwa wakulima wetu? Wananchi wanataka kusikia. Nakushukuru.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nichukue fursa hii nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia sana suala zima la zao hili la kahawa katika jimbo lake. Kwenye maswali yake madogo mawili ya nyongeza, mimi nimejibu kwenye majibu yangu ya msingi kwamba hili suala liko Mahakamani na jambo linapokuwa Mahakamani, sisi kama Serikali tunaviachia vyombo vya sheria viweze kuchukua mkondo wake na ukizingatia pia Mwanasheria Mkuu ndiyo in charge katika suala zima hili.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili la nyongeza, ni kwamba, kama Serikali hata zao la kahawa tumejipanga na tumesema tunafufua, tunaimarisha Vyama vya Ushirika kuhakikisha kwamba wakulima wetu wa Kitanzania hawaonewi na wanakuwa na strong bargaining power kupitia Vyama vya Ushirika ili bei zao ziwe nzuri na mazao yaweze kuwa bora. Nashukuru.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa wakulima 435 wa kahawa waliodhulumiwa katika Jimbo la Buhigwe?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kutokana na swali la msingi, naomba kuuliza Wizara ya Kilimo hapo. Kwa kuwa wakulima wa kahawa ni sawasawa na wakulima wa pamba. Wakulima wa pamba wamewaruhusu waliofanya biashara ya mkataba waweze kuendelea na shughuli hiyo, lakini wakulima wa kahawa katika nchi wa mkataba hawazidi watano mpaka sita. Kwa nini Wizara inakuwa double standard, msimu umeanza sasa hivi wiki ya pili watu hawa hawataki kuwapa kibali cha kuweza kukusanya kahawa kwa sababu ni biashara yao. Naomba tujue hawa haki yao wanaipata wapi?

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, utaratibu tuliouweka sasa hivi lengo lake la kwanza ni kuhakikisha kwamba wakulima wanapata malipo stahiki kwa jasho lao. Mfumo tuliokuwa nao sasa hivi kwa kiwango kikubwa ulikuwa hautoi malipo stahiki kwa jasho la wakulima na moja ya njia zilizotumika kuwanyima haki wakulima ilikuwa ni mfumo wa kununua kahawa kwa kulipa advance kutoka kwa wafanyabiashara na hasa katika Mkoa ambako Mheshimiwa Bulembo anatoka maarufu kwa jina la Butura. Ili kukabiliana na Butura, lazima kuweka mfumo unaofafana maeneo yote.
Mheshimiwa Spika, jana nilisema hapa ndani wakati nachangia hoja ya Bajeti Kuu ya Serikali kwamba pale ambapo mikataba hiyo iliingiwa officially kwamba kuna mkataba na mamlaka za Serikali zinatambua mikataba hiyo kama ilivyo kwenye pamba, pamba mtu haingii mkataba mtu na mtu mmoja, mikataba hiyo inaingiwa kupitia mamlaka za Serikali, kama wako wakulima wa kahawa ambao wameingia mikataba kwa njia hiyo, nilielekeza kwamba wapeleke habari hiyo haraka Bodi ya Kahawa ili waweze kupata utaratibu wa kuuza kahawa kwa mtu waliyeingia naye mkataba.
Mheshimiwa Spika, ile mikataba ya kuingia kienyeji ndiyo utaratibu uliokuwa unasababisha watu kupoteza haki yao na jasho lao kwa kuuza kwa watu ambao wanawapa malipo kidogo kwa kahawa ya bei kubwa.

Name

Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa wakulima 435 wa kahawa waliodhulumiwa katika Jimbo la Buhigwe?

Supplementary Question 3

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwanza KACOFA iko kwenye Kata yangu, Organic iko Kalinze ambako ni Kata yangu. Kwa masikitiko makubwa Waziri anasema kesi iko Mahakamani, si kweli hakuna kesi Mahakamani.
Mheshimiwa Spika, kilichotokea, KACOFA walipeleka Kahawa na hawa Organic-Kalinze walipeleka Kahawa. Kile kiwanda kilipouza Kahawa ile kikawalipa KACOFA, hakikuwalipa Kalinze Organic. Kalinze Organic walipoanza kufuatilia pesa zao wamefanya usuluhishi Wizarani na Bodi ya Kahawa mwisho wake Kiwanda kikasema kitawalipa, naomba nitoe maelezo haya; kitawalipa Organic taratibu.
Mheshimiwa Spika, toka mwaka 2011 kiwanda kile ambacho kilikubali kuanza kuwalipa watu wa Kalinze Organic, kwamba tutawalipa taratibu mpaka leo hakijalipa. Waziri anakuja leo hapa anasema suala lipo kwa Attorney General wakati wameshakubaliana waanze kuwalipa taratibu.
Mheshimiwa Spika, swali langu; naomba Wizara isimamie watu wa Kalinze Organic waweze kulipwa fedha zao kwa sababu makosa haya yamefanywa na kiwanda kile cha Moshi.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jinsi alivyojibu hili swali la msingi la Mheshimiwa Albert Obama. Jambo hili ni la siku nyingi na hatua za awali kama anavyozisema Mheshimiwa Serukamba ni kweli zilichukuliwa namna hiyo. Kosa lililofanyika ni ku-identify nani anatakiwa kulipwa baada ya yule kupeleka ile kahawa kule mnadani.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Bodi ya Kahawa ilivyopokea yale malipo ikapeleka kwa mtu ambaye alitajwa na mtu aliyeleta kahawa kwamba ndiye beneficiary wa hiyo kahawa; kwa hivyo wakamlipa na wale watu wakapokea pesa isiyo yao na wakaitumia.
Mheshimiwa Spika, baadaye ilipoonekana kwamba wamepokea pesa isiyo yao na wametumia, kwanza wakatakiwa wasuluhishwe tu amicably, wakaitwa, wakakiri kwamba watalipa msimu utakaofuata, kwamba watakapouza kahawa msimu unaofuata watalipa hilo deni. Wale waliokuwa wanadai Mheshimiwa Serukamba wakakubaliana na hiyo position, kwamba watapewa pesa yao msimu utakaofuata.
Mheshimiwa Spika, msimu uliofuata wale mabwana wa KACOFA hawakupeleka kahawa, kwa hivyo sasa kukawa na default ya makubaliano hayo; na baada ya hapo ndipo taratibu zikaanza. Nikiri tu kwamba jambo hili lilienda polepole lakini sisi safari hii tulichokifanya tumelipeleka kwenye vyombo vya uchunguzi kwanza tujiridhishe kwa nini walitumia hela ambayo si yao at a time wakati ya kwao walishalipwa? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, humu ndani kuna jinai katikati ya hili jambo, kwamba mtu amekuta benki fedha ambayo si kwake lakini bila kuuliza benki hela hii imetoka wapi, ameitumia, Sheria za Fedha ziko wazi, umeona! Sasa katika hatua hiyo ndiyo Mwanasheria Mkuu wa Serikali atatushauri sasa hivi tuendelee na hatua gani.
Mheshimiwa Spika, kama atatushauri tuwapeleke Mahakamani ili wale viongozi wa ule Ushirika waweze kuchukuliwa hatua wachukuliwe hatua, kwa sababu as we speak hawa hela ya kuwalipa wale wenzao mara moja, kwamba tungewaambia leteni hizi pesa tuwalipe wale ambao wanastahiki ya kupata hizo pesa.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa wakulima 435 wa kahawa waliodhulumiwa katika Jimbo la Buhigwe?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Sasa hivi ni kipindi cha msimu wa kahawa. Vyama vya Ushirika vimeshindwa kuwahudumia wananchi kupata maturubai ya kuvunia Kahawa na hii kahawa inaendelea kukaukia Mashambani, wananchi wamekosa msaada. Hata hivyo, hata wale ambao wamepata maturubai, maturubai haya hayana viwango yanachanika hovyo. Ni hatua zipi za dharura ambazo zitachukuliwa ili kunusuru zao hili na mkulima aweze kulifaidi? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ni kweli tumekuwa na matatizo sana katika suala zima la Vyama vyetu vya Msingi na Vyama Vikuu vya Ushirika na ndiyo maana kama Serikali tunasema kwamba, tuko katika mikakati ya kuhakikisha tunafufua, tunaimarisha na kuboresha Vyama vya Ushirika.
Mheshimiwa Spika, kwa maana hiyo kutokana na swali lake hili la msingi katika Jimbo lake la Kyerwa, kwamba mpaka sasa hivi kunasuasua, naomba nichukue fursa hii kuagiza Chama Kikuu cha Ushirika cha Kyerwa kuanzia leo wahakikishe kabisa kwamba, zoezi zima la mazao ya kahawa katika Jimbo la Kyerwa wanafanya kazi yao kwa ubunifu, wanafanya kazi yao kwa utii, wanafanyakazi yao kwa weledi, wanafanyakazi yao kwa uhakika.
Mheshimiwa Spika, lakini na mimi kama Naibu Waziri nikitoka hapa Bungeni ninaahidi kuwapigia Vyama Vikuu vya Ushirika vile AMCOS pale Kyerwa nikishirikiana na Mrajisi wangu kuhakikisha kwamba jambo hili halijirudii na linaweza kufanikiwa kwa uhakika. Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa wakulima 435 wa kahawa waliodhulumiwa katika Jimbo la Buhigwe?

Supplementary Question 5

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru mimi nina swali dogo la nyongeza. Tarafa ya Herujuu huko Kasulu tunalima Kahawa nyingi na hasa Kata ya Herujuu, Kata ya Muhunga na Kata ya Muganza lakini eneo hilo halina Chama cha Ushirika na Chama cha Ushirika kiko Buhigwe kilometa 45. Ni kwa nini Mheshimiwa Waziri asitoe ruhusa sasa wakulima hawa wakauza kwa watu binafsi?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, hatuwezi kuwaruhusu kuuza kwa watu binafsi kwa sababu tutakuwa tume-distort mfumo tunaojaribu kuujenga. Tunajaribu kujenga mfumo hapa ambao tukiruhusu hicho anachokisema tutakuwa tumeuvuruga tena wenyewe wakati tunajaribu kutengeneza.
Mheshimiwa Spika, mimi binafsi Jimboni kwangu tunalima kahawa, lakini wale wakulima wa kwangu tumewaunganisha na vyama vingine ambavyo vina uwezo wa kufika sokoni na sisi tunaendelea tu kumshauri Mheshimiwa Nsanzugwanko kufanya namna hiyo. Jambo muhimu hapa ni kuangalia uwezekano wa wao wenyewe kuwa na AMCOS yao; na AMCOS zinaruhusiwa kufikisha Kahawa kwenye soko kule Moshi.