Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- Kuna mgogoro wa ardhi wa muda mrefu kati ya wananchi wa kijiji cha Mkwaya na mwekezaji Durbali:- Je, ni lini mgogoro huo utapatiwa ufumbuzi?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa Serikali imekiri kwamba mgogoro upo katika eneo hili, je, haioni haja ya kuharakisha kufuta eneo hili ili wananchi wale wapate maeneo ya kulima?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa wananchi wale wana mahitaji makubwa ya ardhi, Serikali haioni haja sasa kupitia mipaka ya eneo lile ili kuongeza eneo la kijiji?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mpakate, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika swali langu la msingi atakubaliana na mimi kwamba hukumu ndiyo imepatikana Februari, 2018 na bado kuna tetesi kwamba huyu ambaye ameshindwa ni kama vile tayari ametuma application kwa ajili ya kukata rufaa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wale ambao wanahitaji eneo wanapatiwa lakini kwa kufuata sheria. Naomba tuvute subira taratibu zote zifuatwe ili wananchi wapate haki lakini na yule mwingine ambaye alikuwa anamiliki asije akasema kwamba haki yake imeporwa.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- Kuna mgogoro wa ardhi wa muda mrefu kati ya wananchi wa kijiji cha Mkwaya na mwekezaji Durbali:- Je, ni lini mgogoro huo utapatiwa ufumbuzi?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wakati wananchi wa Mkwaya hawajajua mmiliki halali wa eneo hili ni nani kwa kuwa kulikuwa na mgogoro baina ya Serikali na mwekezaji, wakati fulani Machi, 2017 wananchi waliamua…
Ahsante. Kuna watu wameshtakiwa wakati wanaomba hili eneo liweze kuchukuliwa na bado kesi ziko mahakamani lakini Serikali imeshinda kesi. Sasa Mheshimiwa Waziri, anasemaje kuhusu hawa watu walioshtakiwa wakati wanalipigania eneo hili? Ni hatua gani Serikali itachukua ili kuwasaidia wale watu? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bobali, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anajua historia ya mgogoro huu kwamba inaanzia miaka ya 1995 na kwamba kuna wakati ambapo wananchi walivamia maeneo yale ya mwekezaji wakachukua ndizi na wengine wakaenda kutikisa mikorosho. Kwa hiyo, haiwezekani tukasema kwamba sasa hao ambao walivunja sheria Serikali iwatetee, ni vizuri sheria ikafuata mkondo wake.