Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Augustino Manyanda Masele
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbogwe
Primary Question
MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Visima virefu vimechimbwa katika Vijiji vya Lugunga na Kabanga (Mkweni) na maji yakapatikana lakini shughuli za ulazaji mabomba na ukamilishaji imekwama. Je, Serikali iko tayari kutoa utaalam na fedha kukamilisha miradi hii?
Supplementary Question 1
MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba sasa nimuulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, tatizo kubwa hapa ni uhaba wa wataalam. Naomba kujua sasa Serikali itatupatia lini wataalam wa kuweza kutusaidia katika kurahisisha ukamilishaji wa hii miradi ya maji inayoendelea huko Mbogwe? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba sasa kujua time frame, ni lini miradi hii itakamilishwa? Ahsante.
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyowatetea wananchi wake lakini kikubwa maji hayana mbadala na uhitaji wa maji ni mkubwa sana. Sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo, kubwa nimwombe Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane ili tuwape watalaam wetu wa Wizara waweze kumsaidia katika kuhakikisha wananchi wake wanapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala zima la fedha na ni lini miradi hii itakamilika, kikubwa nimwombe sasa Mhandisi wa Maji katika Jimbo lake ahakikishe kwamba anatengeneza certificate ili sisi kama Wizara tutawalipa kwa wakati ili wananchi wake waweze kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.
Name
Edwin Mgante Sannda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kondoa Mjini
Primary Question
MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Visima virefu vimechimbwa katika Vijiji vya Lugunga na Kabanga (Mkweni) na maji yakapatikana lakini shughuli za ulazaji mabomba na ukamilishaji imekwama. Je, Serikali iko tayari kutoa utaalam na fedha kukamilisha miradi hii?
Supplementary Question 2
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kondoa Mjini tulichimba visima kumi, tumepata usambazaji wa visima vitano, lakini bila ya ukarabati wa miundombinu ya maji pale mjini, hizi gharama zilizotumika kusambaza visima vitano ni sawa na bure.
Je, ni lini Serikali itatuletea fedha kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya maji mjini ambayo pia ni ahadi ya Waziri Mkuu? Ahsante.
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Spika, nikushukuru lakini kikubwa nataka nimpongeze kaka yangu Mheshimiwa Sannda kwa jitihada anazozifanya, sisi kama Wizara ya Maji lazima tumuunge mkono. Kikubwa nimuombe Mhandisi wa Halmashauri ya Kondoa asilale, fedha tumeshapitishiwa na Bunge a-rise certificate na sisi tutamlipa kwa wakati mkandarasi atakayetekeleza mradi huo katika kuhakikisha tunaondoa tatizo la maji.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved