Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Visima virefu vimechimbwa katika Vijiji vya Lugunga na Kabanga (Mkweni) na maji yakapatikana lakini shughuli za ulazaji mabomba na ukamilishaji imekwama. Je, Serikali iko tayari kutoa utaalam na fedha kukamilisha miradi hii?

Supplementary Question 1

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba sasa nimuulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, tatizo kubwa hapa ni uhaba wa wataalam. Naomba kujua sasa Serikali itatupatia lini wataalam wa kuweza kutusaidia katika kurahisisha ukamilishaji wa hii miradi ya maji inayoendelea huko Mbogwe? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba sasa kujua time frame, ni lini miradi hii itakamilishwa? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyowatetea wananchi wake lakini kikubwa maji hayana mbadala na uhitaji wa maji ni mkubwa sana. Sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo, kubwa nimwombe Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane ili tuwape watalaam wetu wa Wizara waweze kumsaidia katika kuhakikisha wananchi wake wanapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala zima la fedha na ni lini miradi hii itakamilika, kikubwa nimwombe sasa Mhandisi wa Maji katika Jimbo lake ahakikishe kwamba anatengeneza certificate ili sisi kama Wizara tutawalipa kwa wakati ili wananchi wake waweze kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Visima virefu vimechimbwa katika Vijiji vya Lugunga na Kabanga (Mkweni) na maji yakapatikana lakini shughuli za ulazaji mabomba na ukamilishaji imekwama. Je, Serikali iko tayari kutoa utaalam na fedha kukamilisha miradi hii?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kondoa Mjini tulichimba visima kumi, tumepata usambazaji wa visima vitano, lakini bila ya ukarabati wa miundombinu ya maji pale mjini, hizi gharama zilizotumika kusambaza visima vitano ni sawa na bure.
Je, ni lini Serikali itatuletea fedha kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya maji mjini ambayo pia ni ahadi ya Waziri Mkuu? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Spika, nikushukuru lakini kikubwa nataka nimpongeze kaka yangu Mheshimiwa Sannda kwa jitihada anazozifanya, sisi kama Wizara ya Maji lazima tumuunge mkono. Kikubwa nimuombe Mhandisi wa Halmashauri ya Kondoa asilale, fedha tumeshapitishiwa na Bunge a-rise certificate na sisi tutamlipa kwa wakati mkandarasi atakayetekeleza mradi huo katika kuhakikisha tunaondoa tatizo la maji.