Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:- Jimbo la Masasi lina shule moja tu ya sekondari kwa kiwango cha Kidato cha Tano na Sita ambayo ni Sekondari ya Wasichana Masasi nayo imekuwa haitoshelezi kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaofaulu:- (a) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi Shule za Sekondari za Mwenge Mtapika na Anna Abdallah ili ziweze kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita? (b) Je, ni lini Serikali itaajiri Walimu katika Jimbo la Masasi ikiwa ikama ya Walimu wa Sayansi katika Shule za Sekondari tisa zilizopo ni Walimu 84 lakini waliopo ni 24 tu?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID M. CHUACHUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Sasa naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Masasi imeandika andiko hilo TEA katika kipindi cha takriban miaka miwili iliyopita na mpaka sasa hakuna majibu yoyote au matumaini yoyote ya kupatikana kwa fedha, je, ni lini sasa Serikali kupitaia TEA itatoa fedha hizo ili kuboresha miundombinu ya shule hizo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tangu tulipoambiwa Serikali ina mpango wa kuajiri Walimu 5,000 ni muda sasa umepita, lini sasa Serikali itatoa kauli ya kuajiri Walimu hao rasmi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dkt. Rashid Mohamed Chuachua, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza anauliza juu ya Halmashauri kupeleka maombi TEA na kwamba mpaka sasa hivi bado majibu hayajaja kwa ajili ya upatikanaji wa fedha na miundombinu iweze kuboreshwa ili Form Five na Six zianze kufanya kazi katika Halmashauri ya Masasi. Ni ukweli usiopingika kwamba ili tuweze kuchukua vijana wa Form Five na Form Six ni lazima miundombinu ambayo inatakiwa iwe imakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimsihi Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na Halmashauri yake, hivi karibuni Ofisi ya Rais, TAMISEMI iliwaita Wakurugenzi wote pamoja na Wenyeviti ili waweze kuweka vipaumbele katika maeneo ambayo wanaenda kuboresha katika suala zima la elimu na afya. Ni matumaini yangu makubwa kwamba pamoja na ombi ambalo limepelekwa TEA kwa vile priority yao ni suala la elimu watakuwa wameweka kama kipaumbele ili tuweze kukamilisha miundombinu ya shule hizo mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala zima la kuajiri Walimu, bahati nzuri Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana wakati anahitimisha bajeti yake alisema hapa nasi sote tukiwa mashuhuda. Naomba Mheshimiwa Mbunge awe na imani kama ambavyo tulisema kwamba vibali vitapatikana kwa ajili ya watumishi wa afya na tayari kazi zilishatangazwa, hatua itakayofuata ni hao Walimu ambao Serikali imeahidi kuajiri.

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:- Jimbo la Masasi lina shule moja tu ya sekondari kwa kiwango cha Kidato cha Tano na Sita ambayo ni Sekondari ya Wasichana Masasi nayo imekuwa haitoshelezi kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaofaulu:- (a) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi Shule za Sekondari za Mwenge Mtapika na Anna Abdallah ili ziweze kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita? (b) Je, ni lini Serikali itaajiri Walimu katika Jimbo la Masasi ikiwa ikama ya Walimu wa Sayansi katika Shule za Sekondari tisa zilizopo ni Walimu 84 lakini waliopo ni 24 tu?

Supplementary Question 2

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Changamoto ya Walimu wa Sayansi iliyoko Masasi pia inaukumba Mkoa wangu wa Iringa. Nataka commitment ya Mheshimiwa Waziri kwamba watakapopewa vibali vya kuajiri Walimu wa Sayansi mtaupa kipaumbele Mkoa wa Iringa? Nilitoa mfano last time kuwa Shule ya Lukosi ina watoto 700 na tuna Mwalimu mmoja tu wa Sayansi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rose Tweve, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba maeneo yale yote ambayo yana upungufu mkubwa wa Walimu wa Sayansi ndiyo hayo ambayo hasa yanaanza kupelekewa Walimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niutake Mkoa wa Iringa kwa ujumla wake watupe stock, maeneo ambayo yana upungufu mkubwa hayo ndiyo yawe ya kwanza katika kuhakikisha kwamba walimu wanapelekwa kwa ajili ya kwenda kuziba pengo hilo. Naamini na Iringa nao watafanya hivyo.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:- Jimbo la Masasi lina shule moja tu ya sekondari kwa kiwango cha Kidato cha Tano na Sita ambayo ni Sekondari ya Wasichana Masasi nayo imekuwa haitoshelezi kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaofaulu:- (a) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi Shule za Sekondari za Mwenge Mtapika na Anna Abdallah ili ziweze kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita? (b) Je, ni lini Serikali itaajiri Walimu katika Jimbo la Masasi ikiwa ikama ya Walimu wa Sayansi katika Shule za Sekondari tisa zilizopo ni Walimu 84 lakini waliopo ni 24 tu?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa maswali ya Shule za Sekondari za Wasichana katika eneo la Masasi linafanana kabisa na Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mpanda iliyoko Mpanda Mjini na tumeshaleta maoni kwa Waziri wa Elimu pamoja na Waziri wa TAMISEMI kwamba shule ile ilikuwa inachukua kuanzia Form One mpaka Form Four na ikabadilishwa ikawa Form Five mpaka Form Six. Je, ni lini sasa Serikali itakuja na mpango wa kuhakikisha shule ile inachukua wasichana kuanzia Kidato cha Kwanza mpaka cha Sita kwa kuwa tuna shule moja tu Mkoa wa Katavi ya boarding? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pudenciana Kikwembe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Kikwembe kwa sababu ni miongoni mwa Wabunge wachache ambao huwa wakiwa katika maeneo yao ya Jimbo ambao ni Walimu huwa wanaenda kushika chaki kwa ajili ya kusaidia watoto wetu. Naye ni Mwalimu mzuri wa masomo ya Sayansi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika swali langu la msingi kwamba ni wajibu kuhakikisha kwamba miundombinu yote inayohusika katika uanzishaji wa ‘A’ Level inakamilika, lakini pia ithibati iweze kupatikana na Kamishna wa Elimu aweze kutoa kibali, hapo ndipo tunaposajili shule yetu kwa ajili ya kuanzisha Form Five. Kwa hiyo, naamini na shule anayoitaja Mheshimiwa Mbunge, pindi miundombinu itakavyokuwa imekamilika, Serikali haitasita kwa sababu uhitaji wa ‘A’ Level ni suala ambalo hatuna ubishi katika hilo.