Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:- Moja ya majukumu makubwa ya Serikali ni kulinda raia na mali zao kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama ikiwemo Polisi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukirejesha Kituo cha Polisi katika Tarafa ya Kipatimu Wilayani Kilwa ambacho kilihamishwa?

Supplementary Question 1

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nimeyasikia na naomba anisikilize kwa makini.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba eneo hilo la Tarafa ya Kipatimu lina zaidi ya wakazi 60,000, hatuna kituo cha Polisi, jitihada hizo zimefanywa na wananchi, nikiwemo na Mbunge, nimetoa mifuko 100 ya saruji ku-support na wananchi tayari wamefyatua matofali, tunayo matofali, lakini shida kubwa tunayopata ni ushirikiano kutoka kwa ofisi yake ya Mkoa ambayo mpaka sasa tumehitaji kupata ramani imekuwa shida, tumehitaji kupata mchanganuo imekuwa shida. Je, sasa Mheshimiwa Waziri yuko tayari kunipatia ramani na mchanganuo wa ujenzi ule ili ujenzi uweze kuendelea kwa sababu wananchi wana ari kubwa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza kwa mchango wake katika kufanikisha ujenzi wa kituo hicho.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na ramani na ushirikiano mwingine nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba atapata. Naomba tu baada ya maswali tukutane ili niweze kumpa utaratibu huo namna gani ambavyo anaweza akapata ushirikiano huo, naamini kabisa inawezekana tu tatizo ni mawasiliano.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kawaida Vyombo vyetu vya Dola, kwa maana ya Jeshi la Polisi, vimekuwa vikipenda sana kufanya kazi karibu na wadau mbalimbali ikiwemo Wabunge na wamekuwa wakitoa ushirikiano wa haraka. Kwa hiyo, nadhani kama kulikuwa na changamoto ya mawasiliano, basi baada ya maswali nitakuwa tayari kumsaidia kufanikisha hilo kwa haraka. (Makofi)

Name

Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:- Moja ya majukumu makubwa ya Serikali ni kulinda raia na mali zao kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama ikiwemo Polisi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukirejesha Kituo cha Polisi katika Tarafa ya Kipatimu Wilayani Kilwa ambacho kilihamishwa?

Supplementary Question 2

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na Kituo cha Kipatimo ambacho amesema Mbunge mwenzangu wa Kilwa Kaskazini, Mbunge wa Kilwa Kusini kuna kituo cha Polisi ambacho kimejengwa na wananchi lakini bado kumalizika kule Kijiji cha Nanjilinji. Je, Mheshimiwa Waziri, unaweza kutusaidia ili kituo hicho kimalizike?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kituo cha Nanjilinji ni miongoni mwa vituo vingi ambavyo vimejengwa kwa nguvu za wananchi ambavyo vinahitaji kukamilika. Hiyo ni dhamira ya Serikali, kuhakikisha kwamba vituo vyote hivyo nchi nzima ambavyo vimejengwa kwa nguvu za wananchi vinakamilika, siyo tu kwa sababu ya faida na manufaa ya matumizi ya vituo hivyo, lakini pia kwa kuweza kutokuwavunja moyo wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Kituo cha Nanjilinji, pale ambapo hali ya kifedha itakaa vizuri, tutakimaliza pamoja na vituo vingine, lakini Mheshimiwa Mbunge vilevile anaweza akatumia fursa hiyo kusaidia kuweza kufanikisha ujenzi huo kwa kuhamasisha wananchi wake ama wadau kuendeleza jitihada hizi za Serikali na Serikali pale ambapo uwezo utakuwa tayari basi tutavimaliza.(Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:- Moja ya majukumu makubwa ya Serikali ni kulinda raia na mali zao kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama ikiwemo Polisi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukirejesha Kituo cha Polisi katika Tarafa ya Kipatimu Wilayani Kilwa ambacho kilihamishwa?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Ujenzi wa Kituo cha Polisi Keza, Wilaya ya Ngara, kilichojengwa kwa nguvu za wananchi, kitakamilika lini maana kina zaidi ya miaka saba kimeezekwa bado finishing. Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi huo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kituo cha Keza nacho ni miongoni mwa vituo ambavyo havijakamilika. Bahati njema ni kwamba mwaka huu wa fedha katika Mkoa wa Kagera tumetenga takribani bilioni 1.56 kwa ajili ya kumaliza miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo haijakamilika, ikiwemo nyumba pamoja na vituo vya Polisi. Hiyo inaonesha azma ya Serikali ya kuweza kukabiliana na changamoto ya kumaliza vituo hivi ambavyo havijakamilika pamoja na nyumba za Askari nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba dhamira ya Serikali ipo na pale ambapo hali ya kifedha itakaa vizuri basi tutakamilisha kituo hicho pamoja na vituo vingine ambavyo kama alivyosema mwanzo kwamba viko sehemu mbalimbali katika nchi yetu. (Makofi)

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na niwapongeze sana Waheshimiwa Wabunge wote waliochangia hoja hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo Mheshimiwa Oliver Semuguruka amesema, ni kweli tuna vituo vingi ambavyo vimeshafikia hatua hiyo, niwapongeze sana Waheshimiwa Wabunge kwa sababu wamechangia kwa kiwango kikubwa sana. Kwa sababu ni wengi tu siwezi kuwataja wote, lakini natambua Mheshimiwa Maige, Mheshimiwa Ritta Kabati, Mheshimiwa Oran Njeza na wengine wengi ambao mmechangia ujenzi wa vituo hivi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kituo kilichoulizwa, Mheshimiwa Ulega hapa ndiye aliyekianzisha, niwaombe Waheshimiwa Wabunge kwa sababu wameongelea sana masuala haya ya vituo ambavyo vimeshafikia hatua ya kukamilishwa pamoja na nyumba za vijana wetu ambazo zimejengwa kwa nguvu za wananchi, kwa sababu bado tuko hapa na bajeti tumeshapitisha, niwaombe Waheshimiwa Wabunge wanipenyezee maeneo ambayo yana vituo hivyo ili tunavyomaliza Bunge twende tukae ngazi ya Wizara tuweze kuweka vipaumbele ili tusiharibu nguvu kazi za wananchi ambazo zimeshafanyika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Joseph Selasini ameliongelea sana jambo hili, leteni hivyo vituo ili tutakapokwenda kukaa kwenye ofisi tuweze kuona kile tulichonacho na kuweza kumalizia vile ambavyo vimeshafikia hatua za kumaliziwa. (Makofi)