Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. SAUL H. AMON) aliuliza:- Jimbo la Rungwe ambalo lina kata 29 lina vituo viwili tu vya afya ambavyo ni Masukulu na Ikati; wananchi wa Kata ya Mpuguso na Isongole kwa nguvu zao wameanzisha ujenzi wa vituo vya afya:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia kumaliza ujenzi huo ili kuwapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu katika Hospitali ya Wilaya ambayo baadhi ya maeneo ni takriban kilometa 50 na usafiri usio wa uhakika?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni Serikali imeziagiza halmashauri ziwasilishe miradi viporo ambayo ilihubiriwa na wananchi isiyozidi kiasi cha shilingi bilioni 1 na kwamba fedha hizo zitaletwa katika mwaka huu wa fedha ili kuwapa wananchi nguvu waweze kumalizia miradi ile ambayo waliianzisha kwa nguvu zao. Je, ni lini Serikali sasa inaleta fedha zile kwa sababu umebaki takriban mwezi mmoja mwaka wa fedha kuisha na ni Serikali yenyewe ndiyo ilituambia sisi halmashauri tulete hizo fedha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, pale Mafinga tunakusudia kukamilisha Kituo cha Afya cha Bumilayinga pamoja na zahanati mbili na kujenga nyumba za watumishi kwa maana ya wauguzi watakaoishi katika hizo nyumba kwenye Kituo cha Afya cha Bumilayinga na zahanati mbili za Ulole na Kisada pamoja na ile zahanati ya Sao-Hill. Je, ni lini Serikali inatuletea fedha ili tukamilishe miradi hiyo?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Cosato Chumi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tulielekeza orodha ya miradi viporo iletwe TAMISEMI lakini hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kujipanga vizuri kuweza kuwasaidia au kuunga mkono nguvu za wananchi. Kwa hiyo, naomba sana Mheshimiwa Chumi na Waheshimiwa Wabunge wote kwenye halmashauri zao wawe na subira wakati Serikali inaendelea kujipanga. (Makofi)

Name

Dr. Tulia Ackson

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. SAUL H. AMON) aliuliza:- Jimbo la Rungwe ambalo lina kata 29 lina vituo viwili tu vya afya ambavyo ni Masukulu na Ikati; wananchi wa Kata ya Mpuguso na Isongole kwa nguvu zao wameanzisha ujenzi wa vituo vya afya:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia kumaliza ujenzi huo ili kuwapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu katika Hospitali ya Wilaya ambayo baadhi ya maeneo ni takriban kilometa 50 na usafiri usio wa uhakika?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. TULIA ACKSON: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo hili la Rungwe ni kubwa sana. Hiyo ahadi iliyotolewa hapo na Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu Kituo cha Mpuguso na Isongole, ndiyo, wadau wameendelea kuchangia lakini sijasikia namna ambavyo Serikali imejipanga. Kwa sababu amesema shilingi milioni 100 zitatoka katika mapato ya ndani, hayo yamekuwepo kila wakati, je, Serikali imejipangaje? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson, Mbunge wa Kuteuliwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika jibu la msingi nimeeleza kwamba halmashauri ya wilaya imetenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa OPD katika Kituo cha Afya cha Mpuguso ambacho wameanza wenyewe kujenga kwa kushirikiana na wananchi. Nimetoa ahadi kwamba Serikali katika mwaka 2018/2019 itahakikisha kwamba vituo hivi viwili; cha Mpuguso na Isongole vinakamilishwa kwa utaratibu uleule ambao tumeutekeleza mwaka huu wa fedha. Kwa hiyo, kwa Rungwe, tutakuwa na vituo hivyo viwili kwa kuanzia. Naomba sana Mheshimiwa Mbunge tuwe na mawasiliano ya karibu, inapofika mwezi wa Agosti au Septemba kusudi tuhakikishe kwamba vituo hivi viwili vinapatiwa fedha za ujenzi ili viweze kukamilika 2018/ 2019.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hapo hapo tuendelee kuwa na mawasiliano ya karibu kwa sababu Jimbo la Rungwe ni kubwa sana ili kusudi tuangalie na maeneo mengine.

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. SAUL H. AMON) aliuliza:- Jimbo la Rungwe ambalo lina kata 29 lina vituo viwili tu vya afya ambavyo ni Masukulu na Ikati; wananchi wa Kata ya Mpuguso na Isongole kwa nguvu zao wameanzisha ujenzi wa vituo vya afya:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia kumaliza ujenzi huo ili kuwapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu katika Hospitali ya Wilaya ambayo baadhi ya maeneo ni takriban kilometa 50 na usafiri usio wa uhakika?

Supplementary Question 3

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika kuipunguzia mzigo Hospitali ya Halmashauri ya Mji, Kondoa ambayo inahudumia zaidi ya halmashauri tatu, zahanati za Kata mbili za Kolo pamoja na Kingale zimewekwa katika mpango wa kupandishwa hadhi na kuwa vituo vya afya. Je, ni lini sasa Serikali italeta hizo fedha kwa ajili ya kutekeleza hiyo awamu ya kuweka vituo vya afya?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ME. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Edwin Sannda, Mbunge Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Zahanati za Kolo na Kingale zikipandishwa hadhi zinaweza sana kupunguzia mzigo hospitali ya wilaya. Kama nilivyojibu swali la Mheshimiwa Dkt. Tulia, naomba awe karibu sana kimawasiliano, mwezi Agosti na Septemba ili tuone namna ya kuzipatia fedha zahanati hizi hatimaye ziweze kupandishwa hadhi na Wizara ya Afya ziwe vituo vya afya.