Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi Wilaya ya Mlele?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Kwanza naomba nimpongeze Mkuu wa Wilaya ya Mlele, tayari ameshaanza kufanya hamasa kwa ajili ya Kituo cha Polisi Wilaya ya Mlele, lakini kwa kuwa jengo hili la polisi ambalo wanalitumia sasa hivi ni jengo ambalo walijenga wananchi wakati ikiwa Kata ya Inyonga kwa ajili ya usalama wao, sasa hivi imekuwa Wilaya na matukio yamekuwa mengi zaidi kupita nyuma na uhitaji wa usalama unahitajika zaidi kwa sababu sasa hivi ni Wilaya siyo Kata na wananchi wale walivyojenga hili jengo ambalo walilikabidhi Polisi, walijenga Kituo kidogo na chumba cha mahabusu kidogo…
Mheshimiwa Naibu Spika, kama wananchi walijenga, Serikali inatakiwa ifanye maboresho. Je ni lini Serikali itafanya maboresho ili sasa kile kituo kionekane kama kituo cha Wilaya?
Swali langu la pili, kutokana na chumba kidogo cha mahabusu, kwa sababu sasa hivi mahabusu wale wanachukuliwa wanapelekwa Mpanda Mjini, halafu wanarudishwa Inyonga, gharama kila siku gari limekwenda Mpanda linarudi Inyonga, Serikali haioni ni vyema zile gharama ambazo zitumika kila siku kupeleka gari Mpanda Mjini na kurudisha Inyonga zikatumika kujenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Mlele?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nachukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge na wananchi wake wa eneo hilo na Mbunge wa Jimbo husika kwa jinsi ambavyo wameweza kufanikiwa kuanza ujenzi wa kituo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimekuwa nikijibu mara kadhaa hapa, siyo kwamba Serikali haina mpango wa kujenga vituo vya polisi hususan katika ngazi za Wilaya, mpango huo upo. Nilizungumza jana kwamba tuna mpango wa kujenga vituo takribani 95 nchi nzima, lakini kwa sasa hivi bado hali ya kibajeti haijakaa sawa. Pale ambapo hali ya kibajeti itakapokaa vizuri, eneo hili ni moja katika vipaumbele vyetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kabisa tutakapojenga kituo katika eneo hilo, litatatua vilevile changamoto ya udogo ya chumba cha mahabusu. (Kicheko)