Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha pamba yote iliyopo katika Jimbo la Bunda inanunuliwa kwa bei nzuri na kwa wakati muafaka? (b) Katika Jimbo la Bunda kuna kilimo cha mkataba kwa kampuni moja na wakulima wana hofu kuwa huenda kampuni hiyo isifanye vizuri kwa wingi wa pamba iliyopo, je, Serikali inatoa kauli gani juu ya hali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini pia nawapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu wake na watendaji wote wa Kilimo, wanajitahidi sana kuokoa zao la pamba. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Kabla sijauliza, nisahihishe tu kwenye Hansard kwamba hakuna Jimbo linaitwa Bunda Vijijini. Kuna Jimbo linaitwa Bunda. Kwa hiyo kwenye Hansard kusomeke kuna Jimbo linaitwa Bunda.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa wakulima wa pamba na kwa kuwa katika jibu la msingi Naibu Waziri amesema kuna watu walikopa pamba na kuna vikundi vilifanya mkataba na wana makampuni kukopa pamba, sasa hili tamko la Serikali la kukata shilingi moja kwa kila mkulima ili kulipia pembejeo na hata yule ambaye hakukopa, ni la nini? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Serikali imejiandaa vipi sasa kukabiliana na changamoto zitakazojitokeza kutokana na miongozo yake ya mara kwa mara ambayo haijawa na maandalizi? Kwa mfano, kuna suala la wakulima kufungua akaunti, kuna suala la pamba kununuliwa na ushirika au na watu binafsi kwa maana ya ushirika kununua pamba, kuna suala la kwamba ushirika hauna fedha ya kununulia pamba, sijui ni watu binafsi watatoa kwenye ushirika; Serikali imejiandaa vipi sasa kukabiliana na matatizo haya ambayo watu watayapata kutokana na miongozo yake hii mifupi? (Makofi)

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya swali la msingi. Pia nampongeza Mheshimiwa Getere kwa maswali haya ya muhimu sana katika tasnia ya pamba. Nianze na swali lake la nyongeza la kwanza kuhusu fedha; shilingi moja moja aliyoisema.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pembejeo waliyopata wakulima wengi walio katika mkataba ni lazima ilejeshwe na utaratibu wa kuirejesha ile pesa ni kwa makato kutokana na mauzo yao. Hiyo fedha inayokatwa siyo tu kwamba itafanya kazi ya kurejesha pembejeo waliyopata, lakini ili twende vizuri katika msimu ujao tunapaswa kuwa na fedha ya kuanzia kwa ajili ya kupata pembejeo hizo hizo ambazo wakulima watapata. Ndiyo maana Serikali imeshatamka kwamba msimu ujao wakulima wa pamba kote nchini hawatakopeshwa au pembejeo kwa maana ya dawa au mbegu za pamba. Watapata bure na hii inatokana na hii fedha ambayo wanakatwa sasa hivi.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la nyongeza, siyo kwamba Serikali imesema ushirika utanunua pamba ya wakulima, kwa sababu wakulima wenyewe ndiyo ushirika. Kwa hiyo, kitakachofanya sasa hivi na kinachofanyika ni ushirika unakusanya pamba ya wanachama wake halafu wanunuzi wanaenda kununua kwenye ushirika huo.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha pamba yote iliyopo katika Jimbo la Bunda inanunuliwa kwa bei nzuri na kwa wakati muafaka? (b) Katika Jimbo la Bunda kuna kilimo cha mkataba kwa kampuni moja na wakulima wana hofu kuwa huenda kampuni hiyo isifanye vizuri kwa wingi wa pamba iliyopo, je, Serikali inatoa kauli gani juu ya hali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona.
Kati ya wakulima wanaopata taabu kwa kulaliwa bei na watu ambao hawana soko la uhakika ni wakulima wa pamba. Kwa sababu wanunuzi wengi wanalangua na wanapanga bei wanayoitaka wao na mwisho wa siku wakulima wanapata hasara.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba, ni lini Serikali itawatafutia wakulima wa pamba soko la uhakika ili na wenyewe waweze kunufaika na kilimo cha pamba? (Makofi)

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tu nitofautiane kidogo sana na Mheshimiwa Bulaya kuhusu uhakika wa soko. Soko la pamba ni la uhakika na hatujawahi kuwa na tatizo la kuuza pamba nchini. Pamba ni bidhaa inayouzwa na nchi nyingi duniani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, soko la Tanzania haliwezi kuwa tofauti na Soko la Dunia la Pamba. Majadiliano yanapofanyika kati ya wadau na wauzaji, ni zao pekee ambalo kwa msingi wadau wanajadiliana na wanunuzi, wanafikia muafaka wa bei. Hii inakuwa pegged kwenye bei ya pamba katika Soko la Dunia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, bei inayopatikana siyo kwamba inawalalia wakulima, lakini pia inawapa faida wafanyabiashara na wakulima wanapata haki yao kutegemea na soko la dunia lilivyo.

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha pamba yote iliyopo katika Jimbo la Bunda inanunuliwa kwa bei nzuri na kwa wakati muafaka? (b) Katika Jimbo la Bunda kuna kilimo cha mkataba kwa kampuni moja na wakulima wana hofu kuwa huenda kampuni hiyo isifanye vizuri kwa wingi wa pamba iliyopo, je, Serikali inatoa kauli gani juu ya hali hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Suala hili ni nyeti sana na sijui kwa muda tulionao kama unatosha kulizungumzia. (Makofi)
Mheshimiwa Waziri anasema pamba itauzwa kwa kukusanywa na Vyama vya Ushirika vilivyoko kwenye maeneo yetu, makampuni wataenda wanunue pamba hapo. Tunajua wote ushirika kwenye nchi yetu hali yake ilivyokuwa na sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kuuliza swali, nisirefushe maneno, je, Serikali imejiandaa kwa namna gani kuhakikisha kwamba huu ushirika tunaouzungumza uko imara na kwamba utahakikisha mkulima hapotezi pamba yake na bei ya pamba inapanda kulingana na mahitaji?

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ni kweli ushirika kwa miaka ya nyuma hapa umekuwa na tatizo sana hasa ushirika wa zao la pamba. Siyo siri kwamba wakulima wengi wa pamba walipoteza pesa zao kutokana na viongozi wa Ushirika ambao hawakuwa waaminifu na hivyo kupelekea Serikali wakati ule kuruhusu watu binafsi kuingia katika kununua pamba.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ndaki na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba tumefanya jitihada kubwa sana kwanza za kuhakikisha kwamba viongozi waliochaguliwa katika Vvyama vya Msingi vya Wakulima wa Pamba safari hii ni wale viongozi waadilifu ambao hawatachezea pesa za wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimetoa rai kwa Viongozi wa Ushirika katika Vyama vya Msingi nchini kote kwamba yule anayetaka kuonja sumu kwa kuiba pesa ya wakulima wa pamba afanye hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na matatizo ya ushirika yaliyokuwapo, lakini lengo la Serikali ni kuhakisha kwamba ushirika utaimarika, wizi katika ushirika utakoma na wakulima wapate sauti ya pamoja kupitia ushirika. (Makofi)