Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kiwango cha elimu katika Mkoa wa Tabora kimeshuka sana, Mkoa umefanya vibaya katika mtihani wa darasa la saba, kidato cha nne na cha sita. Kufanya vibaya kunatokana na changamoto mbalimbali kama walimu, upungufu wa madawati na idadi kubwa ya wanafunzi katika madarasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kero hizi zinatatuliwa ili kurejesha hadhi ya elimu Mkoa wa Tabora?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Naibu Waziri ambaye na yeye pia ni mkazi wa Mkoa wa Tabora katika Jimbo la Sikonge anafahamu hali halisi ya elimu za watoto wetu na ndugu zetu katika mkoa wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachotokea hapa na takwimu zinazooneshwa ni shule chache ambazo zimefaulu kwa kiwango kikubwa zinatengenezewa takwimu na zinaonekana kwamba ndiyo takwimu halisi; lakini uhalisia uliopo katika Mkoa wa Tabora, elimu yetu imeshuka kutokana na miundombinu hakuna walimu. …

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha wa kuboresha miundombinu ya elimu katika Mkoa wa Tabora ili watoto wetu waweze kufanya vizuri?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika shule za sekondari ambazo ni shule zilizokuwa zinafaulisha vizuri miaka ya nyuma ambapo watu wengi humu ndani wamesoma katika shule hizo leo shule hizo zimekuwa na changamoto za vitanda, changamoto za viti na changamoto za miundombinu mbalimbali. Serikali ina mpango gani pia wa kuweza kuhakikisha maeneo yale yanaboreshwa ili shule zile ziweze kufanyavizuri kama ilivyokuwa hapo awali?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. GEORGE J. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimsifu san binamu yangu kwa kufuatailia sana sekta ya elimu. Nakubaliana nae kwamba kuna baadhi ya shule hususani za pembezoni kabisa hazifanyi vizuri lakini mara nyingi tunapozungumzia mkoa huwa tunajumlisha kupata matokeo ya kimkoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza, Serikali ina mpango gani kuboresha miundombinu? Kama tulivyowasilisha bajeti yetu vizuri ya juzi, tumejidhatiti kweli kweli. Mwaka huu tumepeleka walimu 112 katika shule za msingi, walimu wa sayansi tumepeleka walimu 20 katika Mkoa wa Tabora lakini kwa mwakani 2018/2019 tutajenga vyumba vya madarasa 207, matundu ya vyoo 689, nyumba za walimu 123 na kwa upande wa sekondari tutajenga nyumba za walimu 179, vyumba vya madarasa 159, matundu ya vyoo 166 na kukamilisha maabara 163 kwa ajili ya masomo ya sayansi. Tunaamini kuwa mchango huu utasaidia kuboresha sana hali ya ufaulu wa vijana wetu katika shule mbalimbali za msingi na sekondari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili; shule maalum ambazo zilikuwa zinafaulisha sana zamani. Kwanza naendelea kuzipongeza shule hizo ikiwemo Tabora Boys ambayo imekuwa ikichangia sana kuinua ufaulu wa Mkoa wa Tabora na ni kweli kwamba baadi ya miundombinu yake iko katika hali ambayo inahitaji sana msaada na naomba niungane nae katika kuzifuatilia shule hizo ili tusaidiane katika kuzitendea haki.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kiwango cha elimu katika Mkoa wa Tabora kimeshuka sana, Mkoa umefanya vibaya katika mtihani wa darasa la saba, kidato cha nne na cha sita. Kufanya vibaya kunatokana na changamoto mbalimbali kama walimu, upungufu wa madawati na idadi kubwa ya wanafunzi katika madarasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kero hizi zinatatuliwa ili kurejesha hadhi ya elimu Mkoa wa Tabora?

Supplementary Question 2

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa matatizo yanayowakabili wananchi wa Mkoa wa Tabora yanafanana kabisa na wananchi wa Mkoa wa Morogoro hususani katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki hasa katika shule ya Mkuyuni ambayo upungufu wa madarasa yanayohitajika ni zaidi ya 18, shule ya msingi Ngerengere Njia Nne madarasa 21 yanahitajika na shule ya msingi Mikese Fulwe madarasa zaidi ya 10.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa kuwa uwezo wa halmashauri yetu ni mdogo na uwezo wa wananchi kujenga madarasa haya yote ni mdogo sana. Je, Serikali kuu ina mpango gani wa kutusaidia kumaliza tatizo hili la vyumba vya madarasa ili kuinua ubora katika shule zetu?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. GEORGE J. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba sana Mheshimwa Omari Tebweta Mgumba, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki nikutane naye baada tu ya Bunge mchana saa saba na nusu ili tuweze kupanga mikakati pamoja. (Makofi)

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kiwango cha elimu katika Mkoa wa Tabora kimeshuka sana, Mkoa umefanya vibaya katika mtihani wa darasa la saba, kidato cha nne na cha sita. Kufanya vibaya kunatokana na changamoto mbalimbali kama walimu, upungufu wa madawati na idadi kubwa ya wanafunzi katika madarasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kero hizi zinatatuliwa ili kurejesha hadhi ya elimu Mkoa wa Tabora?

Supplementary Question 3

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Udhaifu katika sekta ya elimu ni mkubwa kwa nchi nzima na hiyo imekuwa ni mjadala kwa muda mrefu na Wabunge hapa wanaulizia miundombinu na mambo mengine kama walimu, mishahara, yapo ni mambo mtambuka. Sasa Serikali haioni umuhimu, ili elimu yetu iweze ikawa sawa, bora na shirikishi kwa wote, tukawa na mjadala wa Kitaifa namna ya kuboresha elimu kwa kuwa ndio tunda la mfumo wa maendeleo yote Tanzania?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. GEORGE J. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nimshukuru sanaMheshimiwa James Mbatia kwa kurejea kauli ambayo aliitoa Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, Rais wetu mstaafu kuhusu mjadala wa kitaifa ambao sasa hivi tunafikiria namna ya kuuandaa. Kwahiyo naomba ashiriki na sisi katika kuandaa mjadala huo.