Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifungua Zahanati za Solowu na Makoja ambazo zimekamilika ili kuwapunguzia adha ya kufuata huduma ya afya vijiji vya mbali akina mama, watoto, wazee na wananchi wa vijiji hivyo kwa ujumla?

Supplementary Question 1

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri yanayotia moyo wananchi wa Jimbo la Chilonwa. Lakini pamoja na majibu mazuri sana naomba niwe na swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya sababu zinazofanya badhi ya watumishi kukwepa kwenda kufanya vijiji vya ndani ndani ni ukosefu wa nyumba za kuishi.
Je, Serikali haioni kwamba kuna haja ya kusaidia upatikanaji wa nyumba katika zahati zilizo vijiji vya ndani ndani sana? Ahsante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwaka, Mbunge wa Ikulu kuwa kwanza naomba niipongeze Halmashauri ya Chilonwa kwa jinsi ambavyo wameweza kukamilisha zahanati nne. Yeye katika swali lake anauliza namna Serikali kuwezesha kupatikana nyumba za watumishi. Kama ambavyo amefanya kazi nzuri kwa kushirikiana na Halmashauri yao kuhakikisha wanakamilisha zahanati hizo ni vizuri jitihada hizo ambazo zimefanyika wakaanzisha uanzishaji na ukamilishaji wa nyumba za watumishi kwa sababu ni ukweli usiopingika kwamba ukiwa na zahanati nzuri bila watumishi kuwa na sehemu iliyo salama ya kwenda kufanyia kazi.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifungua Zahanati za Solowu na Makoja ambazo zimekamilika ili kuwapunguzia adha ya kufuata huduma ya afya vijiji vya mbali akina mama, watoto, wazee na wananchi wa vijiji hivyo kwa ujumla?

Supplementary Question 2

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa mwenyekiti, ahsante, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Naomba na mimi nimuulize Mheshimiwa Waziri.
Kwa kuwa wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Monduli katika Kata ya Makuyuni, Lemowoti na Halaramii wameonesha juhudi kubwa katika ujenzi wa vituo vya afya; na kwa kuwa Waziri wa TAMISEMI alivyokuja Monduli mwaka 2016 akiwa Naibu Waziri aliahidi kutoa michango kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za wananchi wale. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ya kuwasiadia wananchi wale?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri na kwamba na yeye mwenyewe atakiri na kuungana na jitihada za Serikali na hivi karibuni tumepeleka pesa katika vituo 25.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie kwamba safari ni hatua, azma ya Serikali ni kuhakikisha kwamba vituo vya afya vinajengwa katika kila kata. Kama tumefanya katika kata nyingine, naamini kabisa na kwake itakuwa katika safari ijayo.