Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:- Wilaya ya Chemba haina Kituo cha Polisi; je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Polisi na nyumba za askari?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA S NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
• Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri anasema Jeshi la Polisi likishirikiana na wadau Wilayani Chemba wamekaribia kuanza ujenzi ningeomba anihakikishie ni wadau gani hawa ambayo yeye ana taarifa kwamba tayari wanaanza kushirikiana kujenga kituo cha polisi?
• Binafsi nimechangia kwa kiwango kikubwa sana katika ujenzi wa kituo kipya cha Polisi kule Kwa Mtoro na Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani Komredi Mwigulu alinihaidi hapa ndani ya Bunge kwamba kutokana na mazingira ya Kwa Mtoro hadi Makao Makuu ya Wilaya ya Chemba ambao ni karibu kilometa zaidi ya 120 Serikali ingeweza kuwapatia askari wale gari la kuweza kuwasaidia kwa sababu wanapita kwenye Hifadhi ya Swagaswaga na kuna wanyama wakali. Je, hilo gali litapatikana lini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu katika swali langu la msingi nilieleza kwamba Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ikishirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo wananchi wameanza mchakato wa ujenzi wa kituo hiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana na swali lake la pili kwanza nimpongeze kwa juhudi zake za kuchangia maendeleo ya Jeshi la Polisi katika Wilaya yake, lakini kuhusiana na hali ya Mheshimiwa Waziri nataka nimhakikishie kwamba ahadi ya Mheshimiwa Waziri kama alitoa iko palepale tatizo linalokwamisha ni kwamba bado magari hayo hayajapatikana, naamini kabisa wakati ambapo tumepata magari ya kutosha basi ahadi hiyo itatekelezwa.