Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA aliuliza:- Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusiana na ada ya Zimamoto ambayo wanatozwa wafanyabiashara katika Halmashauri ya Mji wa Tunduru huku kukiwa hakuna Jeshi la Zimamoto na Uokoaji eneo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kabla sijauliza swali la nyongeza ningependa nitumie fursa hii kuishukuru sana Serikali ya Zambia kwa kazi kubwa ambayo wamekuwa wakiifanya ya kuhakikisha kwamba wanatuazima gari yao ya Zimamoto kwa ajili ya kuzima moto kwenye mji wa Tunduma, ninasema mwasalifya sana mwe wantu wa Kuzambia. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza; najua kabisa kwamba Tunduma iko mpakani mwa Zambia na Tanzania na shehena kubwa sana ya mizigo inayoshuka kwenye bandari ya Dar es Salaam inapita Tunduma na Tunduma hatuna gari ya Zimamoto. Je, Serikali haioni kwamba inahatarisha maisha ya wana Tunduma lakini pia na mizigo inayopita kwenye mpaka wa Tunduma?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, wananchi wa Tunduma wanaendelea kutoa ada za zimamoto wakati huduma ya zimamoto kwenye Mji wa Tunduma haipo, hatuoni kama huu ni uzulumaji wa wazi kabisa wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa wananchi wa Tunduma kuendelea kutozwa fedha hizi bila kupata huduma ambayo ni muhimu katika maisha yao? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Spika, kwanza alivyotoa shukurani hizi nikapata mashaka sana, maana mipakani kule kuna mwingiliano sana wa uraia na nilipoona sifa nyingi sana zinaenda Zambia nikataka kujua sana babu zake wake wako wapi. (Makofi/Vicheko)

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Spika, lakini yote kwa yote ni kheri. Niseme tu kwamba yale aliyoyasema Mheshimiwa Mwakajoka kwa utaratibu wetu, tungekuwa hatuna gari kabisa katika eneo husika ingekuwa ni hatari sana, lakini vitu hivi vya moto huwa vinaharibika, na kama nilivyosema kimeenda matengenezo na baada ya hapo kitarudi.
Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu kuwatoza hii ni kwa mujibu wa sheria na sheria za kodi za nchi yetu, si kila kodi inakwenda specific huduma kwa mtu aliyechangia kodi hiyo, na tukifanya hivyo tutakuwa tumekosea kwa sababu kuna maeneo mengine makusanyo ni kidogo.
Kwa hiyo, mimi nitoe rai kwa wananchi wetu waendelee kutoa kodi hizo na hivi tunavyoongea kwenye bajeti iliyopita tumepitisha bajeti ya magari mengine, tunategemea kupata magari mengine kwa ajili ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na huduma hiyo itasambaa katika maeneo mengi zaidi kama ambavyo tumepanga katika malengo yetu. (Makofi)