Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:- Hitaji la kuni limekuwa kubwa kwa matumizi kama nishati ya kupikia na hivyo kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira:- Je, Serikali itawezesha vipi wananchi kupata nishati mbadala kwa matumizi ya kupikia majumbani?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ili nipate kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali ina nia njema ya kupeleka nishati mbadala katika maeneo mbalimbali ya Tanzania; na kwa kuwa, Jimbo la Kavuu lina idadi kubwa ya wafugaji na kinyesi cha wanyama kinapatikana kwa wingi hasa ng’ombe, nguruwe na mbuzi. Pia, kwa kuwa, bado hatuna mtandao mzuri wa majitaka katika miji mingi ya vijijini ikiwemo Jimbo langu la Kavuu. Je, Serikali sasa haioni ni wakati muafaka kupitia taasisi za TADETO na UN Habitat katika kuanzisha miradi ya biolatrine ambayo inatumia kinyesi cha binadamu katika maeneo ya mashule, ili tuweze kupata gesi ya uhakika kutokana na kwamba sasa uharibifu wa mazingira katika Jimbo la Kavuu umekuwa mkubwa especially katika kukata miti hovyo?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, naomba niulize si kwa Serikali na Watanzania kwa ujumla, je, matumizi ya mkaa na gesi yapi ni bora zaidi?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa niseme kwamba, Serikali inaupokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa tufanye utafiti wa kutosha ili tuweze kutumia human waste kutoka kwenye pitlatrin na ku-convert kuwa energy ambayo inaweza ikasaidia matumizi ya binadamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwamba, Serikali iko tayari kutumia hii taasisi ya TADETO ambayo tayari imeshafanikisha miradi miwili Dar es Salaam kwa kujenga bioelectric ambayo sasa hivi inatumika kwenye sekondari mbili pale Dar es Salaam ikiwemo Sekondari ya Manzese. Teknolojia hii inatumiwa zaidi na Uganda kwenye shule za sekondari na shule za misingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake pili kuhusu yapi matumizi bora, tutumie gesi au tutumie mkaa. Ni bora kutumia gesi kwa sababu kwanza gesi bei yake ni nafuu ukilinganisha na bei ya mkaa. Kwa mfano, Dar es Salaam gunia moja la mkaa la kipimo cha kawaida ni Sh.75,000/= lakini ukienda kwenye teknolojia ya nguvu gani inapatikana katika mkaa, wataalam wameshafanya vipimo wakaona kwamba, tunapata unit 2.645 kwenye gunia la mkaa ni energy ambayo inayojulikana kwa kwa jina la Gigajoule.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maana hiyo, unit moja ya gunia la mkaa inauzwa kwa Sh. 28,000/=, lakini ukienda kwenye gesi unit moja inauzwa kwa shilingi 18,000. Pia, ukitumia gesi tayari unakuwa umeshaokoa mazingira yetu, watu wa mazingira ukikata miti unaleta uharibifu wa mazingira ambao unaweza ukatuathiri kwenye mambo mengine kama kutopatikana kwa mvua inayostahili kwa masuala ya kilimo.