Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali ina mpango gani wa kuwalipa posho au mishahara Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji ili kurahisisha ufanisi wa shughuli zao?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wanafanya kazi nzuri na imekuwa ikiwategemea kwenye kazi zote na hata kualika mikutano yote ya Wabunge, Madiwani na kufanya kazi kubwa, asilimia 20 ambayo Mheshimiwa Waziri ameitaja katika majibu yake ya msingi haijawahi kupelekwa hata siku moja.
Je, kwa nini sasa Serikali isilete namna nzuri ya kuwalipa moja kwa moja hawa Wenyeviti kwa sababu, ni viongozi ili pasiwe na utaratibu huu wa asilimia ambayo haijawahi kupelekwa tangu wameanza kazi hizi mpaka sasa? (Makofi)
Swali la pili, kwenye swali langu la msingi nilieleza habari ya Madiwani. Madiwani kimsingi wanapata posho ndogo ya shilingi 300,000 na kitu kama sikosei. Je, ni lini sasa mnaongeza posho hizi ili walau basi wafanye kazi nzuri katika chini ya Halmashauri zetu huko Wilayani? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nafahamu concern ya Mheshimiwa Flatei, lakini jambo hili sio la Mheshimiwa Massay peke yake, naamini Wabunge wengi sana wanaguswa na jambo hili. Na ndio maana unaona Mheshimiwa Massay alivyosimama hapa watu wengi sana, kila mtu alismama kutaka kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zangu naomba niseme ni kweli, kuna baadhi ya Halmashauri hizi posho hazirudi, lakini Halmashauri nyingine zinafanya vizuri katika urejeshaji wa posho hii ya asilimia 20. Ndiyo maana sasa tumesema katika mpango wetu wa kufanya marekebisho ya Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa, Sura Namba 290, tumeweka kifungu maalum ambacho kinampa Waziri mwenye dhamana na jambo hilo kuweka suala zima la regulation maalum ya kulilazimisha suala hili sasa liwe suala la kisheria sio suala la kihiyari.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni kwamba utaratibu wetu katika jambo hili mimi ninaamini si muda mrefu sheria hiyo ya fedha itakuja hapa, tutaifanyia marekebisho, sasa itakuwa ni muarobaini na katika hili naomba niwasihi kwa hali ya sasa hasa Wakurugenzi wetu wote kwamba asilimia 20 kupeleka kila kijiji sio jambo la hiyari ni jambo la lazima sasa tulipeleke ili wananchi wetu kule chini waweze kufanya kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ajenda ya posho ya Madiwani, ninakumbuka kwamba tulikuwa na Tume Maalum hapa ilikuwa maarufu kama Tume ya Lubeleje ambayo ilipitia maeneo mbalimbali na bahati nzuri Mheshimiwa Mzee Lubeleje amerudi tena Bungeni kama Senior MP, ilipendekeza mapendekezo mbalimbali, ndio maana tumesema kwa nyakati mbalimbali kwamba, Serikali inaangalia jambo hili na jinsi gani utaratibu wetu wa mapato utakuwa vizuri basi tutafanya marekebisho kwa kadri itakavyowezekana. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali ina mpango gani wa kuwalipa posho au mishahara Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji ili kurahisisha ufanisi wa shughuli zao?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Na mimi niseme tu kwamba mimi ni miongoni mwa Wenyeviti wa Tanzania wa Serikali ya Mtaa wa Vodacom Kata ya Chanji kwa hiyo, ninaloliuliza ninalijua na changamoto zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya Serikali inayotengwa watekelezaji wa kwanza ni Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji, kauli hii ya kwamba wataanza kulipwa posho sio mara ya kwanza ndani ya Bunge hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba time frame ni lini sheria italetwa hapa ili Wenyeviti waanze kulipwa posho kwa sababu sio hisani wanafanya kazi kubwa? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Dada yangu, Mheshimiwa Aida, Mbunge wa Viti Maalum, lakini Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji, kama walivyokuwa Wenyeviti wengine wa Jimbo la Ukonga kule nikifahamu hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama nilivyosema hapa kwamba kwanza kulikuwa na uzembe. Naomba niseme kwamba hata ile asilimia 20 kama kungekuwa na commitment ya kurudi vizuri katika Halmashauri zetu, maana sasa hivi tunapozungumza kuna Halmashauri nyingine zinafanya vizuri katika hilo. Tuna baadhi ya ushahidi kuna Halmashauri nyingine Wenyeviti wake wa vijiji wanalipwa vizuri kutokana na kwamba wameweka commitment ya asilimia 20 lazima irudi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la time frame ni kwa sababu ni suala la sheria ni suala la kimchakato na taratibu zote sheria hii imeshapitia hivi sasa inaenda nadhani katika Baraza la Mawaziri kupitia katika vifungu mbalimbali, ikishakamilika itakuja humu Bungeni. Sasa niwaombe Waheshimiwa Wabunge sheria ikija humu tunawaomba tushiriki wote kwa pamoja vizuri kwa sababu, ina vifungu vingi sana vinazungumzia suala la mapato katika Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni imani yangu kwamba tutajadili kwa kina tuje kuangalia jinsi gani tutafanya marekebisho mazuri ambayo yataenda kuwagusa Wenyeviti wetu wa Serikali za Vijiji kuweza kupata ile posho yao kwa kadiri inavyostahiki. (Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali ina mpango gani wa kuwalipa posho au mishahara Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji ili kurahisisha ufanisi wa shughuli zao?

Supplementary Question 3

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuwa na sheria ni zuri kwa upande mmoja, lakini kwa upande wa pili Halmashauri zetu zinakabiliwa na matatizo makubwa ya kiuchumi. Sasa Serikali inatoa tamko gani kuhusu kuziwezesha Halmashauri zetu hizi kuweza kukusanya pesa za kutosha ili ziweze kuwalipa watu hawa ambao ni muhimu sana kwenye maendeleo ya vijiji vyetu?(Makofi)

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la ukusanyaji wa mapato la Halmashauri kuwa katika hali ngumu ya uchumi, kwanza ni commitment yetu wote Wabunge na Madiwani kuhakikisha kwamba Halmashauri zetu zikusanye vizuri. Kwa sababu, miongoni mwa kigezo kimojawapo cha existence ya Halmashauri lazima iweze kukusanya mapato ndiyo maana imepewa ridhaa kuwa Halmashauri kamili. Katika hili sasa ndiyo maana katika kipindi hiki kilichopita tumetoa maelekezo mbalimbali katika suala zima la ukusanyaji wa mapato, hasa kutumia mifumo ya electronic.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, katika maeneo mbalimbali tuna- success story kwamba leo hii kwa kutumia mifumo ya electronics tumepata mafanikio makubwa. Sasa maelekezo yangu nadhani twende katika compliance vizuri katika matumizi mazuri ya hii mifumo, kuna mahali pengine mifumo ipo, lakini haitumiki vizuri, watu wana-divert kutoka katika mifumo ya ukusanyaji wa mapato hivi, mifumo ile sasa inajukana ipo, lakini wengine hawapati manufaa katika hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwasihi sana Wakurugenzi wote katika Halmashauri zote twende kuhakikisha kwamba katika idara zetu za fedha tunazisimamia vizuri. Lengo kubwa ni kwamba, mapato yaliyopangwa kupitia Mabaraza ya Madiwani yaende kukusanya vizuri ili tukuze mapato katika Halmashauri zetu. (Makofi)