Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA (K.n.y. MHE. JAFFAR SANYA JUSSA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itavipatia Vituo vya Polisi vya Paje na Jambiani samani za ofisi pamoja na magari kwa ajili ya patrol?

Supplementary Question 1

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Vile vile nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nina swali moja la nyongeza. Tatizo la samani katika vituo vya Zanzibar, zaidi katika Majimbo ya Chwaka, lakini yako katika Wilaya nyingi za Zanzibar yote. Jimboni kwangu kuna Kituo cha Chumbuni ambacho kinahudumia wilaya mbili, Wilaya ya Magharibi na Wilaya ya Mjini, lakini kituo hiki hakina samani, hakina gari, kinahudumia watu zaidi ya 70,000 na kinavuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeshalisemea sana suala hili na nimeshaliuliza zaidi ya mara tatu, mara nne na nikaahidiwa kitatengenezwa na huduma zitapatikana, lakini mpaka leo hali iko vile vile. Je, Mheshimiwa Waziri anatuambia nini wananchi wa Chumbuni kuhusu suala letu hili?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa mfuatiliaji sana wa masuala ya jimbo lake na masuala yanayohusu Vituo vya Polisi vilivyoko katika Jimbo lake. Amekuja Mara kadhaa akisemea jambo hilo na tulishatuma wataalam wetu wafanye tathmini ili tuweze kujua namna tunavyoweza kulishughulikia. Kwa kuwa tunaelekea kwenye bajeti niendelee tu kumhakikishia kwamba, punde bajeti inavyoruhusu tutaweka kipaumbele kwenye jambo hilo ambalo amekuwa akilisemea mara kwa mara. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA (K.n.y. MHE. JAFFAR SANYA JUSSA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itavipatia Vituo vya Polisi vya Paje na Jambiani samani za ofisi pamoja na magari kwa ajili ya patrol?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi. Kwa kuwa mwaka 2015 nilipokuwa Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki nilitoa ufadhili wa gari la golisi kwenye Kituo cha Kata ya Maore kwa ajili ya Jimbo la Same Mashariki; nina uhakika Serikali inalifahamu hilo. Kwa kuwa, lile gari sasa halina matairi, linahitaji kufanyiwa maintainance kubwa. Je, Serikali mnatoa ahadi gani leo hapa ili wananchi wa Same Mashariki wasikie?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mhesimiwa Mbunge Anne Kilango Malecela kwa kusaidia kazi za Ofisi ya Polisi katika Jimbo la Same Mashariki kuweza kufanya kazi na wanakukumbuka sana. Nimefika mwenyewe Same nimeona wakikukumbuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba Serikali inatambua jitihada alizofanya Mheshimiwa Mbunge na tutaongea na Kamanda wa Polisi wa Mkoa ili tuweze kuona namna ambavyo tunaweza tukaunga mkono jitihada hizo ambazo Mheshimiwa Mbunge ulizifanya. Hata hivyo niendelee kukuomba uendelee kuwakumbuka wananchi wa Same kwani wanakukumbuka sana ili vitu kama vile matairi wasiendelee kuvikosa, waendelee kupata kama ulivyokuwa unafanya.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA (K.n.y. MHE. JAFFAR SANYA JUSSA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itavipatia Vituo vya Polisi vya Paje na Jambiani samani za ofisi pamoja na magari kwa ajili ya patrol?

Supplementary Question 3

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kituo cha Polisi cha Kingeja, Jimbo la Mtambire ni kibovu, chakavu na kimekaliwa tangu enzi ya ukoloni. Kumekuwa na ahadi ya Serikali karibu miaka 13 kwamba watakijenga kituo kile, lakini dalili hazioneshi kwamba kuna nia njema ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali ituambie ina mkakati gani wa ziada kuhakikisha kwamba, Kituo cha Polisi cha Kingeja kinajengwa sambamba na Kituo cha Polisi cha Mkoani hasa ukizingatia kuna vifaa vya Polisi ambavyo tayari vimewekwa katika eneo la Wilaya ya Mkoani ambavyo vinatakiwa viweze kusambazwa. Je, Kituo cha Polisi cha Kingeja…

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nia ya Serikali ni njema na utaona kwamba, wiki moja iliyopita Mheshimiwa Makamu wa Rais alikuwa ziarani kule pamoja na Naibu Waziri. Pia utaona kwamba, wamefanya shughuli kubwa ambayo inahusu ujenzi wa vituo na kazi inaendelea. Kwa hiyo kazi ile inayoendelea itafika pia mpaka Jimboni kwako pamoja na kituo kile ulichokitaja na vituo vingine ambavyo vinahitaji huduma kama hiyo.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA (K.n.y. MHE. JAFFAR SANYA JUSSA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itavipatia Vituo vya Polisi vya Paje na Jambiani samani za ofisi pamoja na magari kwa ajili ya patrol?

Supplementary Question 4

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa, Kituo cha Polisi Makambako ni kituo cha kiwilaya na kwa sababu Makambako ndipo katikati ya kwenda Songea, Mbeya na Iringa; na kwa sababu, Waziri alituahidi kutupatia kitendea kazi cha gari. Je, ahadi yake ya kutupatia gari iko pale pale ili shughuli za kipolisi pale ziweze kufanyika kwa ufanisi mzuri?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli pana uhitaji mkubwa wa gari katika Kituo cha Makambako. Niendelee kusema tu kwamba, Serikali inaendelea kuweka umuhimu mkubwa wa kukipatia gari kituo kilichopo hapo na punde magari yatakapopatikana tutaweka kipaumbele kile kama ambavyo tuliahidi.