Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING aliuliza:- Mwaka 2013 Serikali ilianza kutekeleza mradi wa maji wa Kata za Kinyika na Matamba katika Wilaya ya Makete lakini mradi huo haukufanikiwa kutokana na Serikali kutoa maelekezo ya kulaza mabomba ya inchi 2.5 na 4 badala ya inchi 8 kwenye mradi wa kilometa 18; mradi wa maji wa Tarafa za Magoma na Bulongwa ulijengwa muda mrefu wakati idadi ya watu ikiwa ndogo lakini sasa idadi ya watu na matumizi vimeongezeka. (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa Tarafa ya Matamba? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Tarafa ya Bulongwa ili Kata za Bulongwa, Kipagalo na Luwumbu ziweze kupata maji?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali na pia natambua kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi imekuwa ikifanya kazi nzuri kwenye suala maji. Nina maswali mawili ya nyongeza.(Makofi)
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni kweli kabisa kwamba tangu mradi huu uanze, wananchi wa Matamba, Nakinyika, Itundu na Mlondwe hawajawahi pata maji hayo. Nini kauli ya Serikali ya kuhakikisha kwamba inakamilisha mradi huo?
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Tarafa hii ya Matamba pia linafanana sana kwenye Kata za Tandala, Mang’oto pamoja na Ukwama; nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba pia Kata hizi tatu zinapata maji?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Norman Sigalla, nimefanya ziara kule na hilo tatizo nililikuta, kwamba mradi umetekelezwa lakini wananchi hawapati maji, lakini pia wananchi wameongezeka na tukakubaliana. Tumetengeneza mpango ambao utakuwa na gharama ya zaidi ya bilioni nne, na tutatekeleza miradi katika eneo lake katika hiki kipindi cha miaka miwili iliyobaki kwenda mwaka 2020.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Norman Sigalla, amesimamia Halmashauri, andiko wameleta, tunakamilisha kulifanyia kazi ili utekelezaji uendelee. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Norman Sigalla pamoja na wananchi wa Matamba na Kinyika kwamba Serikali ya CCM itahakikisha ikifika 2020 wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING aliuliza:- Mwaka 2013 Serikali ilianza kutekeleza mradi wa maji wa Kata za Kinyika na Matamba katika Wilaya ya Makete lakini mradi huo haukufanikiwa kutokana na Serikali kutoa maelekezo ya kulaza mabomba ya inchi 2.5 na 4 badala ya inchi 8 kwenye mradi wa kilometa 18; mradi wa maji wa Tarafa za Magoma na Bulongwa ulijengwa muda mrefu wakati idadi ya watu ikiwa ndogo lakini sasa idadi ya watu na matumizi vimeongezeka. (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa Tarafa ya Matamba? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Tarafa ya Bulongwa ili Kata za Bulongwa, Kipagalo na Luwumbu ziweze kupata maji?

Supplementary Question 2

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Chama cha Mapinduzi inatekeleza mradi mkubwa sana wa maji wa kutoka Ziwa Victoria kwenda Tabora na mradi huo kuna kipindi vifaa vya ujenzi vilikuwa vina mikwamo kwamo. Swali langu ni dogo tu, je, mradi huo umefikia kwenye hatua gani ya utekelezaji na wananchi wa Tabora wategemee kupata maji hayo lini? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji unaendelea vizuri sana, tulikuwa na matatizo machache ya kuhusu masuala ya msamaha wa kodi lakini tumeshayamaliza, na Mheshimiwa Mbunge wewe mwenyewe ni shahidi; wakandarasi wote watatu wameshaanza kazi, mabomba wanaendelea kuleta na sasa hivi kama unaenda barabara ya kwenda Dar es Salaam utakutana na malori yanabeba mabomba kupeleka Tabora; kwa hiyo mradi unaendelea vizuri. (Makofi)

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING aliuliza:- Mwaka 2013 Serikali ilianza kutekeleza mradi wa maji wa Kata za Kinyika na Matamba katika Wilaya ya Makete lakini mradi huo haukufanikiwa kutokana na Serikali kutoa maelekezo ya kulaza mabomba ya inchi 2.5 na 4 badala ya inchi 8 kwenye mradi wa kilometa 18; mradi wa maji wa Tarafa za Magoma na Bulongwa ulijengwa muda mrefu wakati idadi ya watu ikiwa ndogo lakini sasa idadi ya watu na matumizi vimeongezeka. (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa Tarafa ya Matamba? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Tarafa ya Bulongwa ili Kata za Bulongwa, Kipagalo na Luwumbu ziweze kupata maji?

Supplementary Question 3

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwepo changamoto kubwa sana ya barabara kutokana na mitandao ya maji na hasa katika kata mbalimbali za Jimbo la Segerea ikiwemo Kata ya Vingunguti; je, ni kutokana na ubovu wa mabomba ndiyo maana tunazidi kuona maji yanazidi kutiririka hovyo katika maeneo haya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, changamoto hiyo ipo. Kama tunavyokumbuka, wakati nilipotembelea barabara ya Kwa Mnyamani kutoka hapa Buguruni barabara ya Kwa Mnyamani kwenda Vingunguti, barabara ile muda mwingi sana maji yamejaa barabarani’ Tatizo kubwa ni kwamba yale mabomba yanapasuka kwa hiyo yanajaa barabarani na barabara inaharibika.
Mheshimiwa Naibu Spika, na ndiyo maana nilitoa agizo pale kwamba Manispaa yetu ya Ilala, TARURA pamoja na DAWASCO waweze kukaa pamoja kuangalia ile miundombinu yote ambayo iko barabarani iwekwe vizuri. Bahati nzuri zoezi hilo limekamilika, hivi sasa linaendelea vizuri, niwashukuru sana DAWASCO, pia niwashukuru Manispaa ya Ilala kwa kazi kubwa waliyofanya, na hivi sasa hata ile barabara tunaiboresha, sasa itakuwa kwa kiwango cha lami yote kuanzia hapa Buguruni tunapoingilia mpaka unafika Vingunguti.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili limefanyika shirikishi, kwamba maeneo hayo sasa yawe yanapitika vizuri, vilevile na mitandao ile ya maji ambayo inachanganyana sana wataalam nimewaagiza waiweke vizuri kuhakikisha kwamba tunalinda barabara zetu hizi. (Makofi)

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING aliuliza:- Mwaka 2013 Serikali ilianza kutekeleza mradi wa maji wa Kata za Kinyika na Matamba katika Wilaya ya Makete lakini mradi huo haukufanikiwa kutokana na Serikali kutoa maelekezo ya kulaza mabomba ya inchi 2.5 na 4 badala ya inchi 8 kwenye mradi wa kilometa 18; mradi wa maji wa Tarafa za Magoma na Bulongwa ulijengwa muda mrefu wakati idadi ya watu ikiwa ndogo lakini sasa idadi ya watu na matumizi vimeongezeka. (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa Tarafa ya Matamba? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Tarafa ya Bulongwa ili Kata za Bulongwa, Kipagalo na Luwumbu ziweze kupata maji?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na shukrani za wananchi wa Bagamoyo kwa Mheshimiwa Waziri wa Maji kwa namna ambavyo amesimamia ujenzi wa tenki kubwa la maji Bagamoyo, swali langu ni kuwa, je, lini mradi wa usambazaji wa mabomba ya maji katika Mji wa Bagamoyo pamoja na kata zote za Bagamoyo utaanza?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Programu ya Maendeleo ya Utekelezaji wa Miradi ya Maji katika Mkoa wa Dar es Salaam tunakaribia kuikamilisha. Baada ya kupata vyanzo vya maji tunayo maji ya kutosha, tuliweka makadirio ya dola milioni 100 kwa ajili ya usambazaji. Awamu ya kwanza tulipata dola milioni 32 na miradi hii inaendelea, ndiyo ambayo imejenga hilo tenki analolisema Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sasa hivi tumepata tena dola milioni 45 na mwezi huu tunatangaza tender ili tuweze kupata mkandarasi ili ahakikishe kwamba sasa tunaweka mabomba ya kusambaza maji katika maeneo yote likiwemo eneo la EPZ kule Bagamoyo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wake kwamba huduma ya maji katika eneo lake tunakamilisha. (Makofi)

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING aliuliza:- Mwaka 2013 Serikali ilianza kutekeleza mradi wa maji wa Kata za Kinyika na Matamba katika Wilaya ya Makete lakini mradi huo haukufanikiwa kutokana na Serikali kutoa maelekezo ya kulaza mabomba ya inchi 2.5 na 4 badala ya inchi 8 kwenye mradi wa kilometa 18; mradi wa maji wa Tarafa za Magoma na Bulongwa ulijengwa muda mrefu wakati idadi ya watu ikiwa ndogo lakini sasa idadi ya watu na matumizi vimeongezeka. (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa Tarafa ya Matamba? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Tarafa ya Bulongwa ili Kata za Bulongwa, Kipagalo na Luwumbu ziweze kupata maji?

Supplementary Question 5

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa namna inavyofanya maendeleo nchini, lakini nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI kwa namna yeye na timu yake wanavyohangaikia maendeleo katika nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia Mheshimiwa Waziri akisema juu ya barabara za lami na mabomba kuanzia Buguruni kwenda Vingunguti, sikumsikia akisema kwenye eneo ambalo kodi ndiko zinakokusanywa, kuanzia Buguruni kurudi mjini. Je, maeneo haya ya Buguruni kurudi mjini barabara za lami na maji vipi Mheshimiwa Waziri?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli jambo la maji na barabara ni mtambuka lote kwa pamoja nafahamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Zungu kwanza kuhusu suala la hiyo mitandao ya barabara na maji tumetoa maelekezo, lakini hata hivyo tukija katika upande wa barabara, Mheshimiwa Zungu ofisi yetu itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba Jimbo lile la Ilala kupitia Mradi wa DMDP jimbo lako litaweza kuwa linang’ara zaidi kwa sababu hili ni jukumu la ofisi yetu, na kwa vile unapigana sana kwa wananchi wako, jambo hili tunalibeba na tunalisimamia kwa nguvu zote kwa kipindi hiki.