Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Mradi wa Maji wa Hydom umechukua muda mrefu kumalizika na wananchi wanasubiri maji huku muda wa mkataba na mkandarasi ukiwa umeisha. Je, kwa nini Serikali isimfukuze mkandarasi huyo?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kueleza masikitiko yangu kuhusiana na mradi huu, mwaka 2014 alikuja Katibu Mkuu wa Chama akadanganywa kuhusu mradi huu. Akaja Waziri Kamwelwe Januari mwaka jana akadanganywa kuhusu mradi huu, mimi nimekuja Ofisi na hao uliowasema mwaka jana Desemba mradi ulikuwa uishe tukadanganywa tena.
Mheshimiwa Naibu Spika, nahitaji muda gani na mara ngapi kuja hapa kuuliza maswali haya na uwongo wa kudanganywa namna hii, wananchi kule umetaja 17,000 hawana maji?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa miradi ya maji katika Jimbo la Mbulu Vijijini iko mingi, nayo hakuna muda ambao umetajwa wa kumalizika na mikataba imeisha, na mimi kule sina fundi kabisa au Mhandisi wa Maji ndani ya Halmashauri yangu.
Je, unanisaidia pamoja na kwamba tutakaa baadae kuhusu ya watumishi katika Wizara hii au katika sekta ya maji?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

MHE. JOSEPH J. KAKUNDA - NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI):
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema wakati ninajibu swali la msingi kwamba mradi huu kimsingi umeshatekelezwa kwa asilimia 90 bado asilimia 10 tu, zikazuka changamoto ambazo zilizungumzwa kwenye kikao, zikaonekana kwamba zinatatulika, lakini usiku wa leo nimepata mwendelezo unaohusu changamoto za ziada ambazo tunahitaji kuzitatua baada tu ya kikao hiki.
Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote wa Haydom na Jimbo la Mbulu Vijijini kwamba mradi huu kama tutatatua hizi changamoto ambazo amekumbana nazo mkandarasi ninaamini ndani ya wiki mbili hadi tatu hii asilimia 10 itakuwa imekamilishwa, ndiyo maana tumesema ifikapo mwezi Aprili, tutakuwa tumekamilisha mradi huu.
Swali la pili, kuhusu watumishi, napenda nimwakikishie ndugu yangu Mheshimiwa Flatei kwamba tunaiangalia Wilaya ya Mbulu kwa ujumla na Halmashauri yake ya Mbulu Vijijini kwa uangalifu mkubwa kutokana na mazingira ya eneo lenyewe na physiology ya eneo lenyewe la Wilaya ambalo nimefika ni juu na tambarare zimechanganyika na kwa hiyo tutampatia Mhandisi wa Maji hivi karibuni.(Makofi)

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Mradi wa Maji wa Hydom umechukua muda mrefu kumalizika na wananchi wanasubiri maji huku muda wa mkataba na mkandarasi ukiwa umeisha. Je, kwa nini Serikali isimfukuze mkandarasi huyo?

Supplementary Question 2

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo Mradi wa Maji wa Haydom, Mradi wa Maji wa Chujio Wilaya ya Maswa na wenyewe umekuwa wa muda mrefu sana. Mkandarasi amepewa extension ya kwanza hakumaliza, akapewa ya pili, hakumaliza akapewa ya tatu hakumaliza.
Je, Serikali inaonaje kumwondoa huyu mkandarasi na kuweka Mkandarasi mwenye uwezo zaidi?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa Mkandarasi yule amechukua muda mrefu katika utekelezaji wa mradi, lakini mradi ule uliharibiwa tangu wakati wa usanifu wake. Walisanifu kujenga chujio sehemu ambayo siyo yenyewe, baadaye walivyoingia katika eneo la mradi ikabidi tena wakae kubadilisha, lakini hali m ulipofikia kwa sasa amebakisha sehemu ndogo sana, ameagiza vifaa kutoka nje ya nchi, hatuoni kwamba kwa sasa itakuwa ni busara kumsimamisha kwa sababu vile vifaa vikishafika ni kazi ya kufunga tu na mradi unaanza kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, na nishukuru hata bwawa ambalo litahudumia lile chujio sasa hivi mvua zimenyesha maji yamejaa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge ninakuomba uwe na subira baada ya muda kidogo tu huo mradi utaanza kufanya kazi. (Makofi)

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Mradi wa Maji wa Hydom umechukua muda mrefu kumalizika na wananchi wanasubiri maji huku muda wa mkataba na mkandarasi ukiwa umeisha. Je, kwa nini Serikali isimfukuze mkandarasi huyo?

Supplementary Question 3

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.
Kwa kuwa, katika Halmashauri ya Njombe Mji kuna tatizo kubwa la maji na Serikali imekuwa ikiahidi kuwasaidia wananchi kutatua tatizo hili la maji kupitia mradi wa Hagafilo lakini hakuna dalili yoyote.
Je, ni lini sasa Serikali itaanza kutekeleza mradi huo ambao imekuwa ikiwahaidi wananchi siku zote? Ahsante.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Njombe ni miongoni wa Miji 17 itakayofaidika na mkopo kutoka Serikali ya India wa dola milioni 500, kwa hiyo nikukuakikishie pamoja na wananchi wa Njombe kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi imeshajipanga tayari, mwaka wa fedha unaokuja tutasaini mikataba na kuekeleza mradi wa kuchukua maji kutoka mto Hagafilo na kuhakikisha kwamba Mji wa Njombe sasa unakuwa na maji.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Mradi wa Maji wa Hydom umechukua muda mrefu kumalizika na wananchi wanasubiri maji huku muda wa mkataba na mkandarasi ukiwa umeisha. Je, kwa nini Serikali isimfukuze mkandarasi huyo?

Supplementary Question 4

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa nia ya Serikali ni kumtua mama ndoo, kumsogezea huduma jirani ili kuweza kupata maji hasa vijijini na mijini; na kwa kuwa kuna miradi 17 mikubwa ya maji hasa fedha za kutoka India ambazo zilipitishwa kwenye bajeti hapa; na kwa kuwa Mji wa Makambako umekuwa ni miongoni mwa miji ya kupata mradi huu mkubwa wa maji katika miji ile 17.
Je, Serikali inawaambia nini wananchi wangu wa Mji wa Makambako ili waweze kupata maji, ni lini miradi hii itaanza?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Deo Sanga kwa kufuatilia mradi huu wa mkopo wa dola milioni 500 kutoka Serikali ya India. Hata jana tulizungumza naye na alinituma niende kwa Waziri wa Fedha na majibu niliyopewa na Waziri wa Fedha ni haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, taratibu sasa zinakamilishwa ili tuweze kusaini mkataba wa fedha (financial agreement) na baada kukamilisha kusaini basi moja kwa moja Wizara ya Maji na Umwagiliaji itaanza kutangaza tender kumalizia usanifu ili pamoja na hiyo miji 17 bwawa lako la Tagamenda litajengwa ili Mji wa Makambako upate huduma ya maji.