Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI aliuliza:- Wananchi wa Kata za Mahinda, Ngoyoni, Mengwe na Kirongo – Samanga walifanya uamuzi wa kujenga vituo vya polisi kwa nguvu zao na vituo hivyo vimefikia hatua mbalimbali za ujenzi, lakini kutokana na kuwepo na shughuli nyingine zinazohitaji michango ya wananchi kama vile ujenzi wa vituo vya afya, zahanati na maabara wameshindwa kumalizia vituo hivyo. Je, Serikali iko tayari kuchukua hatua za kumalizia ujenzi wa vituo hivyo njia ya kuwatia moyo wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ningependa kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tukisubiri sungura mdogo huyu wa Serikali kugawanywa nchi nzima sisi watu wa Rombo tumeamua kujiongeza, na tumejenga Kituo cha Polisi Useri kimeshaanza kufanya kazi, Kituo cha Ngoyoni kiko kwenye rooffing, kituo cha Kirongo Samanga pamoja na nyumba ya polisi karibu inafika kwenye linta na kituo cha Mahida kiko kwenye msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ningependa jibu la hakika ili wananchi wa Rombo waamasike kuchangia zaidi ujenzi wa hivi vituo. Ni lini mtakuja kufanya hiyo tathimini ili kuwatia moyo wananchi wakamilishe hivi vituo kwa sababu kazi ya kuchangia vituo vya polisi ni ngumu kuliko hata kuchangia zahanati na shule?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa sababu ya urefu wa mpaka wa Rombo na Kenya na njia za panya kuwa nyingi, Jeshi la Polisi Rombo lina magari ya zamani sana na chakavu.
Je, Serikali iko tayari kuweka katika bajeti ijayo gari kwa ajili ya kusaidia shughuli za polisi katika Wilaya ya Rombo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue furusa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge, na hii ndiyo aina ya Wabunge wakutolewa mfano. Kazi waliyoifanya ni kubwa ya kushirikiana na kuhamasisha wananchi wake kujenga vituo vitatu hivi kituo cha Ngoyoni, Mahida na Kirongo si kazi ndogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwahakikishie mbele ya Bunge hili Tukufu kwamba jitihada za aina kama hii za Mbunge Selasini na Wabunge wengine wengi tu wamo katika Bunge hili wanafahamu wamefanya kazi nzuri kama hii. Serikali itaziunga mkono na mimi nimuhakikishie kwamba nitahakikisha tathimini hii imekamilika haraka na natarajia kufanya ziara hiyo karibuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikwenda kushuhudia hii kazi mimi mwenyewe na ndiyo maana nazungumza kwa kujiamini sana. Nilikwenda nilifanya ziara Rombo na nikaona kazi hii inafanyika vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa hiyo basi namuhakikishia kwamba nitakuja tena Rombo karibuni ili tushirikiane kwa pamoja. Kuna mambo mawili ambayo tutafanya; la kwanza tutatoa kipaumbele katika bajeti ambayo inakuja ili kuhakikisha vituo hivi vinakamilika; lakini la pili nitashirikiana na Mheshimiwa Mbunge ili kuendelea kuhamasisha wadau zaidi ili tumalize vituo hivi ili viweze kutumika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, kulingana na kazi nzuri ambayo Mheshimiwa Mbunge anaifanya nina uhakika kabisa tutaangalia uzito wa changamoto ya gari katika Mkoa wa Rombo ili tuone katika gari ambazo tunatarajia kuzipokea wakati wowote tuweze kupeleka huko zisaidie kupunguza changamoto za askari.

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI aliuliza:- Wananchi wa Kata za Mahinda, Ngoyoni, Mengwe na Kirongo – Samanga walifanya uamuzi wa kujenga vituo vya polisi kwa nguvu zao na vituo hivyo vimefikia hatua mbalimbali za ujenzi, lakini kutokana na kuwepo na shughuli nyingine zinazohitaji michango ya wananchi kama vile ujenzi wa vituo vya afya, zahanati na maabara wameshindwa kumalizia vituo hivyo. Je, Serikali iko tayari kuchukua hatua za kumalizia ujenzi wa vituo hivyo njia ya kuwatia moyo wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi naomba niulize swali la nyongeza.
Wilaya ya Itilima iliyoko Mkoani Simiyu ni miongoni mwa Wilaya zilizoanzishwa mwaka wa fedha 2012/2013, lakini ninavyozungumza hivi Wilaya hiyo haina Kituo cha Polisi. Ni lini mkakati wa Serikali kuhakikisha Wilaya hiyo mpya inapata Kituo cha Polisi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua Wilaya ya Itilima ina changamoto hiyo, lakini kama ambavyo tunatambua maeneo mengine vilevile na tuna mikakati ya kukabiliana na tatizo hilo, kama nilivyozungumza katika majibu yangu ya msingi na hili nalo tunalichukua, tunalijua na tutalifanyia kazi. Pale ambapo hali itakaporuhusu kituo kitajengwa katika Wilaya hiyo.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI aliuliza:- Wananchi wa Kata za Mahinda, Ngoyoni, Mengwe na Kirongo – Samanga walifanya uamuzi wa kujenga vituo vya polisi kwa nguvu zao na vituo hivyo vimefikia hatua mbalimbali za ujenzi, lakini kutokana na kuwepo na shughuli nyingine zinazohitaji michango ya wananchi kama vile ujenzi wa vituo vya afya, zahanati na maabara wameshindwa kumalizia vituo hivyo. Je, Serikali iko tayari kuchukua hatua za kumalizia ujenzi wa vituo hivyo njia ya kuwatia moyo wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kilindi ina takribani miaka 20 toka imeanzishwa lakini hali ya kusikitisha ni kwamba kituo kinachotumika ni kama post wakati ikiwa ni Wilaya ya Handeni zamani. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri au Waziri yuko tayari kutembelea Jimbo la Kilindi ili kujionea hali halisi ya jinsi ambavyo hata OCD anakaa guest house mpaka leo? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumjibu Mheshimiwa Shekilindi, Mbunge wa Kilindi kuwa....
Samahani Mheshimiwa Kigua, Mbunge wa Kilindi kuwa tutakuja Kilindi.