Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Maeneo mengi ya Bukoba Vijijini kama vile Kata za Ruhunga, Kibirizi, Izimbya, Mugajwale, Rukoma, Kikomelo na nyingine yana tabu kubwa sana ya upatikanaji wa maji na kilio hiki kimekuwa cha muda mrefu sana:- Je, ni kwa nini Serikali haichukui hatua ya kuwasaidia wananchi hao.

Supplementary Question 1

MHE. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu ingawa baadhi ya maeneo aliyosema yamekamilika, miradi yake haijakamilika. Nina maswali mawili ya nyongeza:
Swali la kwanza; maeneo niliyoyataja haya ya Kata ya Ruhunga, Kibirizi, Izimbya, Mugajwale, Rukoma, Kikomelo na mengine kama Kaitoke, Kyamuraire yana shida kubwa sana ya maji na swali hili nimeliuliza leo ni mara ya nne. Je, niulize mara ngapi ili hawa wananchi nao wafikiriwe kupata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa vile tumeshapata ufumbuzi wa tatizo la maji nchi nzima maana yake siyo kwangu tu ni nchi nzima kuna tatizo la maji nao ufumbuzi huo ni kuunda wakala au Mfuko wa Maji nchi nzima kama ilivyo REA kwenye umeme. Tumelijadili humu mara nyingi na tumekubaliana. Je, kwa nini Mfuko huu hauanzi ili tatizo hili liweze kupata ufumbuzi. (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza huo mradi wa maji kwenye eneo lake tulishaujadili na tukaangalia uwezekano wa namna gani tunaweza tukapeleka maji pale kwa kutumia chanzo cha maji cha Ziwa Victoria kutoka kwenye mradi uliokamilika pale Bukoba na tayari tulishaagiza wataalam wanafanyia kazi ili tuweze kufikisha maji katika hayo maeneo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili kuhusu uanzishaji wa Mamlaka ya Maji Nchini tunalifanyia kazi na tuko katika hatua nzuri kabisa wakati wowote tutaleta tangazo kwamba tayari Wakala wa Maji Nchini utaanzishwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji pale tutakapopata ridhaa ya Bunge. (Makofi)

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Maeneo mengi ya Bukoba Vijijini kama vile Kata za Ruhunga, Kibirizi, Izimbya, Mugajwale, Rukoma, Kikomelo na nyingine yana tabu kubwa sana ya upatikanaji wa maji na kilio hiki kimekuwa cha muda mrefu sana:- Je, ni kwa nini Serikali haichukui hatua ya kuwasaidia wananchi hao.

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Matatizo ya maji yaliyoko Bukoba Vijijini yanafanana na matatizo tuliyonayo kule Karatu. Kata ya Rotia na Kata ya Mang’ola zina upungufu mkubwa wa maji kutokana na miundombinu iliyokuwepo kuwa ya muda mrefu na hivyo kushindwa kupeleka huduma ya maji stahiki. Je, ni lini sasa Serikali itatenga fedha ili kuboresha huduma ya maji katika Kata hizo mbili. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) : Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo yeye mwenyewe amekiri maeneo ya Karatu ni miongoni mwa maeneo ambayo tangu zamani kumekuwa na uwekezaji kwenye miradi ya maji na ndiyo maana miradi hiyo aliyoitaja amesema kwamba miradi ile ina uchakavu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwenye awamu ya pili ya utekelezaji wa program ya maji tumeweka kipaumbele kikubwa kwanza kukarabati miradi iliyokuwepo ikiwemo hiyo ya Kata ya Rotya na Kata na Mang’ola ambayo kuna miundombinu ya maji ya muda mrefu. Kwa hiyo kipaumbele ni kukarabati kwanza hiyo kabla hatujaanza miradi mipya.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Maeneo mengi ya Bukoba Vijijini kama vile Kata za Ruhunga, Kibirizi, Izimbya, Mugajwale, Rukoma, Kikomelo na nyingine yana tabu kubwa sana ya upatikanaji wa maji na kilio hiki kimekuwa cha muda mrefu sana:- Je, ni kwa nini Serikali haichukui hatua ya kuwasaidia wananchi hao.

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Swali langu narudia pale pale kwamba kama alivyouliza Mheshimiwa Rweikiza ni kwamba ni lini Serikali itafikiria kuanzisha Mfuko huu wa Maji ili kuweza kuondoa kero kubwa kwa wananchi kuhusu matatizo ya maji kama ambavyo tumeweza kuondoa kero ya umeme sasa katika sehemu nyingi vijijini. Je, ni lini tutaanzisha huu Mfuko wa Maji? Nadhani ndiyo hoja ya msingi zaidi hapa.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kuna mambo mawili; Mfuko ulishaanzishwa. Mfuko tayari tunao na Mwaka huu wa Fedha tulionao Mfuko una jumla ya shilingi bilioni 158. Suala la pili sasa tunataka kuanzisha Wakala kwa ajili ya kutumia huo Mfuko ili tuwe na wakala utakaohakikisha kwamba tunapata huduma ya maji vijijini kwa haraka. (Makofi)