Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:- Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa? (b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini? elezaji wa REA Awamu ya I na II Wilaya ya Mwanga MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:- Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa? (b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake. Wizara ya Nishati imesema mara nyingi ndani na nje ya Bunge kwamba katika vijiji ambavyo vinahusika na mradi wa REA watu wote walioko kwenye vijiji hivyo, hata wale ambao nyumba zao ni za majani watapewa umeme. Hata hivyo, katika utekelezaji wa miradi hii Awamu ya Kwanza na Pili katika Wilaya ya Mwanga ni familia chache sana zilizokuwa zimejitayarisha kupewa umeme ambazo zimefungiwa umeme huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeambiwa kwamba nia yake ni kuipa TANESCO biashara ya kuzifungia kaya hizo umeme kwa Sh.177,000/= baada ya mradi kukamilika. Je, sera hii tuliyotangaziwa hapa imefutwa lini ikaja hii ya TANESCO kuchagua watu wachache kuwapa umeme na wengine kuwaacha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tuliambiwa kwamba, mkandarasi huyu ambaye ameshindwa kazi ya kusambaza umeme pale awali hawezi tena kupewa kazi katika Wizara ya Nishati na Madini, hasa kazi ileile ambayo yeye alifukuzwa kwa kushindwa kutekeleza. Sasa katika Wilaya ya Mwanga aliyekuwa anatekeleza mradi huu kwa niaba ya SPENCON alikuwa bwana mmoja anaitwa Mrs. Njarita & Company Limited. Sasa Njarita huyo huyo amepewa kazi ya kutekeleza mradi huo kwa jina lingine la Octopus. Je, inatuambia nini au inawezaje kututhibitishia kwamba, huyu aliyeshindwa kutekeleza huu mradi huko nyuma, sasa ataweza kutekeleza round hii? Ahsante. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Profesa Jumanne Abdallah Maghembe kwa maswali yake mawili ya nyongeza, lakini na kwa kazi nzuri anayofanya katika kufuatilia mahitaji ya nishati katika Jimbo lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa kwenye ziara wiki iliyopita katika Jimbo la Mheshimiwa Maghembe, kukagua maeneo mbalimbali ambako mradi huu wa REA Awamu ya Pili haukufanyika vizuri, lakini utakubaliana na mimi kwamba, ni kweli kuna mahitaji makubwa na kwa kuwa, hizi kazi zinatekelezwa kwa mujibu wa scope na kwamba, scope ile inakuwa haikidhi mahitaji, lakini Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutambua hilo imekuja na Mradi Mpya wa Ujazilizi (densification).
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu unatekelezwa katika mikoa sita ya awali ya mfano. Ilipofika Mkoa wa Kilimanjaro na wao Mkandarasi Mshauri Elekezi yupo ndani ya mkoa ule kujaribu kufanya feasibility study kwa ajili ya mradi huu, densification kwa maeneo ambayo au kwa kaya ambazo hazijaguswa au taasisi za kijamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mbunge hakuna ukweli wowote kwamba, zile kaya ambazo hazijaunganishwa nia ya kwamba, iipe kazi TANESCO.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TANESCO ni Serikali ambayo nayo ina kazi ya kusambaza umeme, lakini kwa utaratibu mwingine, lakini si kweli kwamba, kaya hazifikiwi kwa sababu ya kuipa kazi TANESCO. TANESCO itaendelea na kazi ya kusambaza umeme, lakini kama umeme vijijini na ndio maana Serikali imetambua uwepo wa ukubwa wa mahitaji imekuja na huo Mradi wa densification. Kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge zile kaya ambazo hazijaunganishwa, zile taasisi za umma ambazo hazijaunganishwa, zitaunganishwa kupitia mradi huu wa densification ambao umefanya vizuri katika Mikoa ya Songwe, Mbeya, Pwani, Arusha, Tanga, Iringa na Mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ameeleza kwamba mbona mkandarasi yuleyule ndio amepewa kazi na kwamba, Wizara itathibitishaje kwamba kazi zitafanyika. Ni kweli kazi ilifanywa na Kampuni ya SPENCON ambayo ndio ilikuwa main contractor. Huyu Kampuni ya Njarita Octopus walikuwa Sub Contractor. Uchunguzi uliofanyika na Serikali na Wakala wa Umeme Vijijini ulithibitisha kwamba, tatizo lilikuwa kwa main Contractor mwenyewe ambaye ni Spencon si hawa Sub Contractor.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo nilipokuwa katika ziara tulikuwa na Mkandarasi huyu Njarita na sisi tumempa maelekezo na masharti, ndani ya miezi sita kazi zile zilizoshindwa kufanywa zimalizike na zikamilike.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati nzuri nilipokuwa eneo la tukio mkandarasi alikuwa ameshaanza kazi na niliwaomba viongozi wa maeneo hayo, Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya, Waheshimiwa Wenyeviti wa Halmashauri, pia nilizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mama yangu Anna Mghwira kwamba Ofisi yetu au Wizara yetu itasubiria taarifa za mara kwa mara za Mkandarasi huyu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wakandarasi hawa waliopewa kazi hii tutawafuatilia kwa kila hatua kuona kwamba, makosa yaliyojitokeza awamu zilizopita hayajitokezi tena. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:- Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa? (b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini? elezaji wa REA Awamu ya I na II Wilaya ya Mwanga MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:- Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa? (b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niipongeze Serikali chini ya Wizara ya Nishati kwa kazi nzuri wanayofanya ya usambazaji wa umeme vijijini, hasa hii REA Awamu ya Tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba, kwa kuwa gharama za kuunganisha umeme wakati mradi unaendelea katika eneo ni Sh.27,000 na mradi ukishapita ni Sh.177,000; na kwa kuwa idadi nzuri na kubwa ya watumiaji wa umeme ni biashara nzuri kwa TANESCO, kwa nini sasa bei hii isiwe moja hiyohiyo ya 27,000 badala ya bei kupanda baada ya mradi kwisha? Kama haiwezekani, basi REA hawa waendelee na kazi ya usambazaji wa nguzo na miundombinu na TANESCO wafanye kazi moja tu ya kupeleka umeme na kukusanya kodi yao baada ya kupeleka umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa na namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, Kaka yangu Nape Nnauye. Ni kweli bei ya kusambaza umeme ya vijijini ni Sh.27,000 kipindi cha mradi na hii ni hatua ya Serikali yetu ya Awamu ya Tano kwamba, imegharamia gharama zote za uunganishwaji kwa umeme huu na kwamba mwananchi yeye gharama yake ni analipia VAT.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wazo alilolisema kwamba, mara baada ya mradi kukamilika na miundombinu kukabidhiwa TANESCO ni kweli wananchi wanaunganishwa kwa bei ya Sh.177,000, lakini hata hivyo niseme hata hii bei pia, Sh.177,000 nayo ina mchango wa Serikali kwa sababu, mijini kwa bei hii wanaunganishwa kwa Sh.321,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, wazo alilosema linapokelewa na litafanyiwa kazi na ni la msingi kwa sababu, Wizara yetu na Shirika letu la TANESCO na wadau wengine wa nishati kwamba, tunauza bidhaa ya umeme. Kwa hiyo, ni vema zaidi kwamba, tunapoiuza tupate wateja wengi, ili tupate mapato na kuendesha shughuli mbalimbali na uwekezaji mpya wa maeneo ya nishati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, nimelipokea na Serikali itaona utaratibu gani wa kufanya ili iweze kurahisisha. Ahsante sana.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:- Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa? (b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini? elezaji wa REA Awamu ya I na II Wilaya ya Mwanga MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:- Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa? (b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini?

Supplementary Question 3

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikiahidi mara nyingi sana kulipa fidia wananchi ambao maeneo yao yanapitiwa na umeme wa KV400. Miongoni mwa maeneo hayo ni Mkoa wa Manyara na katika Jimbo langu la Babati Mjini, wameahidi zaidi ya mara tatu na ahadi ya mwisho ni tarehe 17 Disemba, kwamba, mngewalipa. Hata hivyo, mpaka sasa Mheshimiwa Naibu Waziri mmekuwa mkisema kwamba, Wizara ya Fedha haiwapi pesa na Waziri wa Fedha yuko hapa. Naomba awatangazie wananchi wa Jimbo langu la Babati Mjini kwamba, ni lini wanawalipa fidia hiyo kwa sababu, wamechoka kusubiri?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Pauline Gekul kwa swali lake zuri, lakini naomba niseme haijapata kutokea Wizara yetu ya Nishati ikasema Wizara ya Fedha haijatupa pesa, kwa sababu Serikali inafanya kazi kwa pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ambayo ilijitokeza ni kwamba tulipata jedwali la thamani ya fidia. Wizara yetu ya Fedha kazi yake yeye hata inapoleta pesa ni kuangalia malipo yanafanyika kwa walengwa na kwa viwango sahihi. Kwa hiyo kulikuwa na changamoto ndogo ndogo tu za kumalizia kwa ajili ya kuthibitisha uhalali, kiwango na walipwaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimwambie Mheshimiwa Mbunge mradi huu wa KV400 msongo huu ni muhimu ambao unaunganisha na nchi ya jirani ya Kenya kwa kusafirisha umeme kwa maeneo mbalimbali. Kwa hiyo nimthibitishie kwamba fidia ya wananchi wa maeneo hayo italipwa muda si mrefu, ndani ya mwaka huu wa fedha na maandalizi yanaendelea vizuri. Ahsante sana.

Name

Suleiman Masoud Nchambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:- Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa? (b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini? elezaji wa REA Awamu ya I na II Wilaya ya Mwanga MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:- Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwanga haikukamilika na fedha zilizokuwa zimepangwa hazikutumika:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia umeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bila kufungiwa? (b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga, mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini?

Supplementary Question 4

MHE. SULEIMAN S. MURAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, na yeye apewe maelekezo afike kwenye kaya zote. Na Mheshimiwa Naibu Waziri nakukaribisha Mvomero karibu sana. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Murad kwa swali lake la nyongeza na kazi anazoendelea kufanya za kufuatilia miradi ya umeme. Nakubaliana na yeye kwamba, huyu Mkandarasi MDH kwa kweli hakufanya vizuri na hakuwa mkandarasi katika mkoa wake tu, lakini alikuwa mkandarasi pia katika Mkoa wa Pwani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi tumetoa maelekezo kwa REA kwa sababu, wakandarasi wote wa Miradi ya REA Awamu ya Pili ni Mikoa miwili tu Tanga na Arusha ambao wametimiza vigezo na wamemaliza kipindi cha uangalizi. Kwa hiyo mikoa mingi ina changamoto, Singida, Mbeya, Mikoa ya Kanda ya Ziwa. Kwa hiyo, tumetoa maelekezo na tumewataka REA wafanye tathmini na tutachukua hatua na kwamba, maelekezo ni kwamba, awamu ya tatu isiruke kitongoji chochote wala taasisi ya umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niliahidi Bunge lako Tukufu kwamba, nimesema tangu awali kwamba, upungufu wa awamu ya pili tumeubaini, tathmini imefanyika, awamu ya tatu tumejipanga vizuri kuhakikisha kwamba, umeme huu au miradi hii inatimiza lengo lililotarajiwa na maelekezo ya Serikali kwamba, kila kitongoji kisirukwe. Ahsante sana.