Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI aliuliza:- Askari Polisi wengi katika Jiji la Tanga wanaishi uraiani ambapo ni kinyume cha maadili kutokana na ukosefu wa nyumba za kuishi katika kambi zao. • Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga upya nyumba za askari hao? • Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwajengea nyumba za ghorofa askari wa Kambi za Chumbageni, Mabawa na Madina Msambweni, ili ziweze kuwaweka askari wengi katika eneo moja, kama ilivyo Kilwa Road Dar es Salaam?

Supplementary Question 1

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Naibu Spika, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, miundombinu ya vyoo hususan katika Kambi ya Polisi wanaoishi katika eneo la Msambweni Madina ni mibaya sana kiasi ambacho wenyewe wanaita ni SACCOS.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatengenezea vyoo vyao wakati wanasubiri utaratibu wa kujengewa hizo nyumba?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa askari wale wanatumia maji ambayo Serikali ndio inawalipia, lakini maji hayo hayo utakuta wenyewe hawayatunzi vizuri, utakuta maji yanamwagika na wanayaachia.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawekea mita kama walivyoweza kuwawekea LUKU?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa maswali mawili madogo ya nyongeza. Nikianza na lile la uchakavu, la vyoo, niseme tu kwamba naelekeza wafanye tathmini na nitawaambia watu wangu Wizarani ili tuweze kuangalia namna ambavyo tunaweza kusaidia kwa sababu hilo ni jambo ambalo linahitaji uharaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hili la kuhusu maji kumwagika ni suala la miundombinu na ni suala la umakini katika utumiaji wa maji. Tutayaangalia yote pamoja, lakini la msingi sana ambalo linafaa kwa askari wetu ni upatikanaji wa maji wa kila wakati. Tumejaribu kwenye LUKU, maeneo mengi sana tumepata shida sana kwa sababu ya wakati fulani fedha ambazo zinatakiwa zilipie kuchelewa na hivyo kuwafanya askari walipe kwa fedha zao na baadae kuanza kuhangaika kupata fedha za kufidia. Kwa hiyo, tutayaangalia yote kwa pamoja, ili tuweze kuhakikisha kwamba, tunatunza maji ili askari wapate maji kwa kila wakati. (Makofi)

Name

Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI aliuliza:- Askari Polisi wengi katika Jiji la Tanga wanaishi uraiani ambapo ni kinyume cha maadili kutokana na ukosefu wa nyumba za kuishi katika kambi zao. • Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga upya nyumba za askari hao? • Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwajengea nyumba za ghorofa askari wa Kambi za Chumbageni, Mabawa na Madina Msambweni, ili ziweze kuwaweka askari wengi katika eneo moja, kama ilivyo Kilwa Road Dar es Salaam?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, askari wanaoishi uraiani huwa wanapewa shilingi 40,000 kwa ajili ya pango. Shilingi 40,000 hii ni kwa ajili ya room moja, maji, umeme na familia hizi wana watoto.
Je, Serikali haioni umuhimu a kuongeza kiasi hiki cha fedha, ili askari wetu wanaporudi kupumzika nyumbani waweze kupumzika vizuri bila kelele za watoto?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Grace kwa swali alilolileta. Niseme tu jambo alilolisemea ni kilio cha askari na hata nilipozunguka maeneoe mengi nimekutananacho na Mheshimiwa Rais tayari alishatuelekeza tufanye upya uchambuzi wa masuala mengi yanayohusu stahiki za askari pamoja na sheria zinazo-govern utaratibu mzima wa taasisi hizi za majeshi yaliyoko ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani na hiyo ni moja ya kitu ambacho tutakiangalia yakiwepo na mengine ambayo yanashusha morali ya kazi ya askari wetu. (Makofi)

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI aliuliza:- Askari Polisi wengi katika Jiji la Tanga wanaishi uraiani ambapo ni kinyume cha maadili kutokana na ukosefu wa nyumba za kuishi katika kambi zao. • Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga upya nyumba za askari hao? • Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwajengea nyumba za ghorofa askari wa Kambi za Chumbageni, Mabawa na Madina Msambweni, ili ziweze kuwaweka askari wengi katika eneo moja, kama ilivyo Kilwa Road Dar es Salaam?

Supplementary Question 3

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa pale kwenye Mji wetu wa Musoma tatizo la nyumba za polisi limekuwa ni tatizo kubwa na kwa muda mrefu. Na ninakumbuka kuanzia mwaka 2006 nimekuwa nikipiga kelele hapa Bungeni na bahati nzuri Serikali yetu sikivu ikakubali na ikaanza kujenga pale jengo na kufikia mwaka 2014 likawa limekamilika zaidi ya asilimia 85, lakini cha ajabu Serikali imeshindwa kutoa fedha za kulimalizia, matokeo yake wameanza kuiba milango, masinki na vitu vingine.
Je, Serikali sasa ni lini itatoa fedha ili ujenzi huu uweze kumalizika na wale askari waweze kuihsi vizuri?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru babu yangu Mheshimiwa Veda Mathayo kwa swali lake alilolileta. Nilishafika kwenye jengo hilo analoliongelea na kwa kweli limeshakamilika kwa kiwango kikubwa. Na sisi kama Wizara tunajipanga kuhakikisha kwamba, katika mwaka wa fedha huu fedha zitakazopatikana na ambazo zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo ambayo yameshafikia hatua nzuri, likiwepo hilo pamoja na maeneo mengine yanakamilishwa.
Kwa hiyo, punde fedha zitakapopatikana tutatoa kipaumbele kwa majengo haya ambayo yameshafikia hatua nzuri, ili yaweze kukamilishwa na askari waweze kuhamia. (Makofi)

Name

Munira Mustafa Khatib

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI aliuliza:- Askari Polisi wengi katika Jiji la Tanga wanaishi uraiani ambapo ni kinyume cha maadili kutokana na ukosefu wa nyumba za kuishi katika kambi zao. • Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga upya nyumba za askari hao? • Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwajengea nyumba za ghorofa askari wa Kambi za Chumbageni, Mabawa na Madina Msambweni, ili ziweze kuwaweka askari wengi katika eneo moja, kama ilivyo Kilwa Road Dar es Salaam?

Supplementary Question 4

MHE. MUNIRA MUSTAFA KHATIBU: Mheshimiwa Naibu Spika, asante. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri swali moja dogo tu. Mheshimiwa Waziri nyumba zilizopo ndani ya Mkoa wa Kusini Pemba, hasa Wilaya ya Mkoani ni chakavu sana. Je, Serikali ina mkakati gani kukarabati nyumba hizo?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuleta swali hili. Ni kweli, hata mazingira ya kazi tu katika Mkoa wa Pemba ni magumu sana kufuatana na uchache wa nyumba za askari. Jambo hili Waheshimiwa Wabunge wamekuwa wakilipigia sana akiwemo Balozi wa Askari, Mheshimiwa Faida Bakar.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba, kama ambavyo nimesemea katika maeneo mengine ambayo yana hali tete za makazi ya askari, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ambaye nay eye amekuwa akifuatilia sana masuala ya askari, yakiwemo nyumba pamoja na haki zao nyingine yakiwemo madai kwamba, tutatoa kipaumbele kwa ajili ya nyumba hizo kwa sababu, mazingira ya kazi yanakuwa magumu pale askari wanapokosa makazi bora ya kukaa.