Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Sekta ya uvuvi bado haijatumika kikamilifu kulipatia Taifa pato na kuwaondoa Watanzania hususani wavuvi katika dimbwi la umaskini. (a) Je, ni lini Serikali itaweka jitihada za kusaidia wavuvi hasa wale wanaojihusisha na uvuvi wa Bahari Kuu? (b) Je, ni lini Serikali itatoa mikopo yenye masharti nafuu kwa wavuvi wadogo wadogo ili waweze kuvua katika Bahari Kuu?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, uvuvi wa bahari Kuu unahitaji uwekezaji wa fedha na mitaji na wavuvi wengi katika maeneo ya Ukanda wa Pwani walikuwa wanatumia uvuvi wa kupiga mabomu ili kupata samaki na Jimboni kwangu katika maeneo ya Mchinga, Ruvu, Mvuleni, Maloo na maeneo mengine wale watu wameacha sasa upigaji wa mabomu kwa kufuata na kutii sheria za nchi sasa.
Je, nauliza Serikali ina mpango gani ya kuwasaidia hawa wavuvi ambao walikuwa wanavua kwenye eneo la bahari kuu kwa kutumia mabomu na sasa wameacha kwa kutii sheria wana mpango gani wa ziada wa kuwasaidia ili waendelee kuvua?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ukanda wetu wa bahari una takribani urefu wa kilometa 1,424 kutoka Tanga mpaka Mtwara, lakini ukiacha maeneo ya Miji Mikuu kama Dar es Salaam, Tanga na Mtwara, maeneo yote yaliyopo kwenye ukanda wa bahari watu wake ni maskini sana. Nataka kujua, Serikali inajifunza nini kwa watu wa Ukanda wa Pwani kuwa maskini kwa kiwango kile wakati wana rasilimali hii nzuri ya bahari? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA UVUVI NA MIFUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ametaka kujua mikakati zaidi ya namna ambavyo Serikali imejipanga kuwasaidia wavuvi ili waweze kuvua katika eneo la bahari kuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu la msingi ya kwamba Serikali ina mipango kadha wa kadha na tayari tumekwisha anza nayo. La kwanza ni hili la kuwawezesha kupata ruzuku kupitia vikundi vyao ambapo wavuvi mbalimbali katika nchi yetu wamepata ruzuku hii ya mashine. Hata yeye Mheshimiwa Bobali wavuvi wake wa jimbo la Mchinga tuko tayari kuhakikisha kwamba wanapata mashine hizo za kuweza kwenda kuwasaidia kwenda kufika bahari kuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama haitoshi, Serikali kupitia Taasisi mbalimbali na mifumo ya ushirikiano tunao mradi mkubwa wa SEOFISH ambao utakwenda kuhakikisha kwamba kama tulivyofanikiwa katika Mradi wa MACEMP hapo nyuma utakwenda kuwasaidia wavuvi hawa wa Ukanda wa Pwani kuweza kupata elimu za ujasiriamali, kuweza kuwasaidia kivyombo na kimifumo ili waweze kuwaondoa katika umaskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili linahusu kwa nini na Serikali ina mpango gani. Ni kweli jamii nyingi za wavuvi wakiwemo wavuvi wa Jimbo la Mkuranga katika eneo la Kisiju ni kweli wapo katika hali ya umaskini na wavuvi wengine wote nchini. Ndiyo maana Serikali ya Awamu ya Tano ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kujua hilo tukadhamiria kuona kwamba tuondoe tozo mbalimbali ambazo zinawagusa wavuvi na kuwarudisha nyuma na kupata unafuu wa maisha yao. Tutaendelea na jitihada hizo ili kuhakikisha wavuvi wetu wanapiga hatua ya maendeleo. (Makofi)

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Sekta ya uvuvi bado haijatumika kikamilifu kulipatia Taifa pato na kuwaondoa Watanzania hususani wavuvi katika dimbwi la umaskini. (a) Je, ni lini Serikali itaweka jitihada za kusaidia wavuvi hasa wale wanaojihusisha na uvuvi wa Bahari Kuu? (b) Je, ni lini Serikali itatoa mikopo yenye masharti nafuu kwa wavuvi wadogo wadogo ili waweze kuvua katika Bahari Kuu?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Sambamba na swali la msingi la Mheshimiwa Bobali napenda niulize swali langu la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tunafahamu kwamba kwenye ukanda wa Pwani wavuvi wake ni maskini sana hasa katika mikoa hiyo iliyotajwa na ninataka nizungumzie Mkoa wa Lindi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Lindi hauna viwanda, rasilimali pekee iliyopo ni ya bahari na wavuvi wanategemea bahari hiyo ili kujipatia riziki zao. Wavuvi hao wote kule wanavua samaki wengi sana matokeo yake baada ya kuvua samaki wale kwa kuwa wanakosa soko kinachofanyika, samaki wale ni kuwakausha kwa mazingira ya kwetu tunaita ng’onda. Samaki wale wanafanywa kuwa ng’onda yaani samaki wakavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunaamini kwamba Serikali ya Awamu ya Tano ni Serikali ya viwanda. Je, Serikali ina mpango gani juu ya kutuletea au ya kuhakikisha kwamba wavuvi wale wanatengenezewa viwanda ili kuondokana na umaskini waliokuwa nao? Ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, Lindi sasa ni ya viwanda na ushahidi upo tayari wa kutosha kutokana na malighafi hiyo ya upatikanaji wa gesi. Lindi inanukia katika viwanda na tayari maeneo kama ya Kilwa yameonesha mfano, kuna kiwanda kikubwa sana cha mbolea ambacho kinaenda kujengwa pale. Nina imani kwa uwepo wa malighafi hii ya samaki na nina imani kwa kuwa Serikali yetu ya Awamu ya Tano ni Serikali ya viwanda na kwa kuwa Mheshimiwa Mwijage na Wizara yake wanafanya kazi kubwa sana ya kuhamasisha viwanda viweze kujengwa na sekta binafsi, ninaamini wawekezaji watavutika na wataenda kuweka kiwanda cha uchakataji wa samaki katika eneo la Lindi na kuondoa kilio hiki cha kukosekana kwa kiwanda cha samaki katika mwambao wetu huu wa Pwani. (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Sekta ya uvuvi bado haijatumika kikamilifu kulipatia Taifa pato na kuwaondoa Watanzania hususani wavuvi katika dimbwi la umaskini. (a) Je, ni lini Serikali itaweka jitihada za kusaidia wavuvi hasa wale wanaojihusisha na uvuvi wa Bahari Kuu? (b) Je, ni lini Serikali itatoa mikopo yenye masharti nafuu kwa wavuvi wadogo wadogo ili waweze kuvua katika Bahari Kuu?

Supplementary Question 3

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa miaka kumi mfululizo ulimwenguni sekta inayokua kwa kasi katika sekta ya kilimo ni sekta ya samaki. Serikali ipo tayari sasa kuwasaidia wavuvi walioko Ukanda wa Pwani kuondokana na umaskini kwa sababu sekta hii imeonekana ni sekta inayokua kwa kasi? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iko tayari kuwasaidia wavuvi kusonga mbele.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Sekta ya uvuvi bado haijatumika kikamilifu kulipatia Taifa pato na kuwaondoa Watanzania hususani wavuvi katika dimbwi la umaskini. (a) Je, ni lini Serikali itaweka jitihada za kusaidia wavuvi hasa wale wanaojihusisha na uvuvi wa Bahari Kuu? (b) Je, ni lini Serikali itatoa mikopo yenye masharti nafuu kwa wavuvi wadogo wadogo ili waweze kuvua katika Bahari Kuu?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kamati ya Mheshimiwa Chenge iliyokuwa inapendekeza kodi mbalimbali mpya ilitoa mapendekezo ya kutumia uvuvi wa bahari kwa ajili ya kuongeza mapato na mara zote ni kwamba Serikali inasema boti za kisasa ambazo zinaweza zikadhibiti wavuvi wa kina kirefu hazipatikani.
Je, Serikali haioni kwamba kwa kutopatikana kwa boti hizo Serikali inakosa mapato makubwa sana kutokana na wavuvi haramu wa nchi mbalimbali duniani wanaokuja kuvua katika bahari yetu? Ni lini sasa boti hizo zitapatikana? (Makofi)

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Selasini anaulizia juu ya uboreshaji wa sekta ya uvuvi na akihusisha na Kamati ya Chenge One ambapo mimi nilikuwa mjumbe wa Kamati hiyo tukiwa na Mheshimiwa Selasini. Nimwambie tu Mheshimiwa Selasini kwamba sasa kwa sababu mapendekezo yale tuliyapendekeza ili Waziri wa Uvuvi akayafanyie kazi na mimi ndiye Waziri wa Wizara hiyo sasa hivi aniachie ili tukamilishe mapendekezo hayo ambayo tulipendekeza kwa Waziri wa Uvuvi ambaye leo ni mimi. (Makofi)