Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Askari wa Wilaya ya Bukombe wanazo changamoto nyingi zikiwemo ukosefu wa nyumba za askari. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia nyumba askari hao katika Wilaya ya Bukombe?

Supplementary Question 1

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii.
Mheshimiwa Spika, kabla sijauliza maswali yangu mawili ya nyongeza naomba nichukue nafasi hii, nilishukuru sana Jeshi la Polisi Wilayani Bukombe kwa kudhibiti uhalifu ambao umekuwa wa mara kwa mara na kwa kutumia kikosi cha Anti-Robbery cha Mkoa kwa kweli wametusaidia kudhibiti uhalifu huu ambao ulikuwa unasumbua sana wananchi.
Mheshimiwa Spika, sasa naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. La kwanza ukweli ni kwamba sisi wa Wilaya ya Bukombe tuna eneo tayari kwa ajili ya kuwapatia polisi waweze kujenga nyumba kwa ajili ya makazi ya askari wetu. Nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri anithibitishie sasa ni lini wataweza kujenga kwa kuwa eneo lipo?
Mheshimiwa Spika, la pili; kwenye Kata ya Namonge pamoja na Bulega wananchi wenyewe wameamua kujenga vituo vidogo vya polisi na wamefika mahali vinahitaji finishing kwa ajili ya kuweka askari. Nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri awaambie wananchi wa Bukombe, je yuko tayari kuwasaidia wananchi ambao wamejotolea kwa kiasi kikubwa sana, aweze kukamilisha vituo vidogo hivyo vya polisi? Ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii.
Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Doto Biteko kwa jinsi anavyofanya vizuri kazi za kibunge. Amesemea sekta zote ambazo ziko jimboni kwake kwa ufanisi mkubwa sana, na nadhani wananchi wa Bukombe watakuwa wameiona tofauti kati ya Ubunge wa Doto pamoja na ule mwingine ambao ulikuwa ni wa mvua hadi mvua. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nimhakikishie Mheshimiwa Doto Biteko kwamba kwa kuwa kiwanja kimeshapatikana, basi mimi naelekeza wataalam wangu watengeneze ramani zinazoendana na viwango ambavyo tumevisema kama Wizara na kama Makao Makuu ya Jeshi la Polisi ili baada ya fedha kuwa zimepatikana tuweze kuanza utekelezaji wa mradi huo ambao Mheshimwia Mbunge ameuleta.
Mheshimiwa Spika, kuhusu la pili ambalo amelisemea, wadau pamoja na vijana wangu walishafanya kazi hiyo ya kujenga nyumba na zinahitaji ukamilishwaji, nielekeze watuletee makadirio yanayohitajika kwa ajili ya ukamilishwaji ili niweze kuwakabidhi wataalam wangu na watendaji wangu waweze kutafuta kwenye akiba ya bajeti yetu tuliyonayo ili tuweze kukamilisha ili vijana wangu waweze kuhamia. Na nikupongeze Mheshimiwa Doto kwa kuwasemea vijana wangu Jeshi la Polisi kwani polisi wanapofanya kazi vizuri na mimi nakuwa Waziri wa Mambo ya Ndani mzuri na naendelea kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani. (Makofi)

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Askari wa Wilaya ya Bukombe wanazo changamoto nyingi zikiwemo ukosefu wa nyumba za askari. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia nyumba askari hao katika Wilaya ya Bukombe?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Spika, ahsante nashukuru. Kwanza awali ya yote niishukuru Serikali sasa hivi amani Kibiti inazidi kuimarika. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu, wananchi wa Kibiti wametenga takribani ekari 15 kwa ajili ya ujenzi wa Polisi Kanda Maalum. Je, ni lini watajenga kituo hicho?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayoifanya na kwa kweli amekuwa bega kwa bega kuzileta hoja za wananchi wa Kibiti pamoja na ukanda ule. Nimhakikishie tu, kwa sababu kanda tayari ilishaanza tayari tumeshateua uongozi na uongozi uko kazini kwa hiyo hatua inayofuata ni ujenzi wa jambo hilo na tunalielewa, tunategemea tu kulitekeleza kufuatana na mtiririko wa fedha kwa tutakapokuwa tunapata. (Makofi)

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Askari wa Wilaya ya Bukombe wanazo changamoto nyingi zikiwemo ukosefu wa nyumba za askari. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia nyumba askari hao katika Wilaya ya Bukombe?

Supplementary Question 3

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona na ningependa kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Kahama nyumba za Polisi zina hali mbaya kweli, na nimewahi kuuliza hapa na kumuomba Mheshimiwa Waziri akaniahidi kwamba watatusaidia kukarabatai zile nyumba. Kwanza hazitoshi na zina hali mbaya.
Je, ni lini Mheshimiwa Waziri atakuja kutusaidia kuweza kukarabati nyumba zile ili anglau polisi nao waweze kuishi katika mazingira mazuri? Ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nimshukuru Mheshimiwa Salome kwa kuleta jambo hili. Nilishazungukia Wilaya ya Kahama. Kama tunavyojua Kahama ni moja ya eneo potential sana katika nchi yetu, hata kimakusanyo; kwa hiyo hata vijana wetu wanaokaa kule na wanapokabiliana na changamoto za eneo husika wanatakiwa wawe katika mazingira mazuri. Tunalitambua jambo hilo na kwa sababu limekuwa likiletwa mara kwa mara. Niseme tu kwamba tutalipa kipaumbele, tutalipa uzito ili hadhi za nyumba za askari wetu ziweze kulingana na eneo husika.