Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Tangu mwaka 2014 TANESCO iliweka alama ya X kwenye maeneo ya Kiluvya, Kibaha hadi Chalinze kupisha ujenzi wa kupitisha umeme wa Gridi ya Taifa lakini hadi sasa hakuna fidia iliyolipwa kwa wananchi hao na pia wanashindwa kufanya uendelezaji wa maeneo hayo. Je, ni lini wananchi hao watalipwa fidia stahiki?

Supplementary Question 1

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Pwani, tangu alama ya X zilivyowekwa Serikali haijarudi kutoa mrejesho kwamba kitu gani kinaendelea na wananchi wale kujua tathmini hiyo watalipwa kiasi gani. Je, ni lini watarejesha mrejesho kwa wananchi ili waweze kujua malipo yao yatakuwa kiasi gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Serikali iliweka alama za X mwaka 2015 na sasa hivi tunaelekea 2018. Wananchi wanauliza watalipwa kwa tathmini ile au uthamini utafanywa mwingine? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ameuliza ni lini Serikali itapeleka mrejesho, naomba nimtaarifu muda si mrefu Serikali itapeleka mrejesho wa namna ambavyo malipo haya ya bilioni 21.6 kwa wakazi wa maeneo haya inakojengwa msongo huu wa kilovoti 400. Kwa kuwa mimi na yeye ni Wabunge tunaotoka Mkoa wa Pwani na niwataarifu pia Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Koka na Mheshimiwa Ridhiwani maana nao wamekuwa wakifuatilia, kwa hiyo muda si mrefu tutawapelekea mrejesho na taarifa wataipata. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge ameuliza kwamba kwa kuwa tathmini ilifanyika mwaka 2015 na tunaelekea mwaka 2018, naomba tu nimtaarifu kwamba malipo ya fidia yatalipwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo. Ahsante. (Makofi)

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Tangu mwaka 2014 TANESCO iliweka alama ya X kwenye maeneo ya Kiluvya, Kibaha hadi Chalinze kupisha ujenzi wa kupitisha umeme wa Gridi ya Taifa lakini hadi sasa hakuna fidia iliyolipwa kwa wananchi hao na pia wanashindwa kufanya uendelezaji wa maeneo hayo. Je, ni lini wananchi hao watalipwa fidia stahiki?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Hoja ya kulipa fidia watu wanaopisha mradi wa TANESCO inafanana na watu ambao walichomewa moto mashamba yao wakati wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam katika Kijiji cha Kilangala. Bahati TPDC kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Lindi waliunda Tume ya kwenda kuhakiki yale madai ya kuunguziwa moto mashamba yao mwaka 2013.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari tathmini imeshafanyika na kinachosubiriwa ni kulipwa tu lakini tuliahidiwa wananchi wale wangelipwa mwezi wa Julai. Naomba commitment ya Serikali, ni lini wananchi wa Kilangala watalipwa hizi fedha zao ambazo zilitokana na wao kuchomewa moto mashamba yao? Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni kweli tathmini ilifanyika na naomba nimtaarifu kwamba wananchi wa Kijiji cha Kilangali watalipwa kwa mujibu wa sheria na taratibu. Ahsante.

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Tangu mwaka 2014 TANESCO iliweka alama ya X kwenye maeneo ya Kiluvya, Kibaha hadi Chalinze kupisha ujenzi wa kupitisha umeme wa Gridi ya Taifa lakini hadi sasa hakuna fidia iliyolipwa kwa wananchi hao na pia wanashindwa kufanya uendelezaji wa maeneo hayo. Je, ni lini wananchi hao watalipwa fidia stahiki?

Supplementary Question 3

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami nilitaka nimuulize Mheshimiwa Waziri. Wananchi wa Jimbo la Segerea, Kata ya Kinyerezi, Mtaa wa Kifulu nao pia walitoa maeneo yao kwa ajili ya kuipisha TANESCO na mpaka sasa hivi hawajalipwa tangu Machi, 2016. Nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri ni lini wananchi wa Kinyerezi watalipwa pesa hizo kwa ajili ya maeneo yao waliyotoa?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bonnah Kaluwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tathmini ya maeneo ya Kinyerezi ambapo maeneo yao yametolewa kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa Kinyerezi imekamilika na kiasi cha Sh.10,475,603,000 zinahitajika. Kwa hiyo, naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge na wananchi wake kwamba fidia hii italipwa kwa bajeti zinazokuja. Ahsante.