Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

KITETO Z. KOSHUMA (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Wavuvi wa Wilaya ya Rorya wanaovua katika Ziwa Victoria wamekuwa wakitekwa, kunyang’anywa nyavu zao pamoja na injini za boti. Aidha, majambazi wanaofanya vitendo hivyo hutumia silaha nzito na inasemekana ni wanajeshi kutoka Uganda. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongea na Serikali ya Uganda ili kukomesha uvamizi huo?

Supplementary Question 1

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na majibu ya Serikali, imesema kwamba hawana ushahidi na Serikali ina mkono mrefu, je, ni kwa nini Mheshimiwa Waziri katika Wizara yake wasiweke mkakati wa operation maalum ili kuweze kuwakamata wahalifu hawa ambao wamekuwa wakizorotesha uchumi wa wavuvi? Hilo ni swali la kwanza.
Swali la pili, kwa kuwa wavuvi wengi Kanda Ziwa wakiwemo wavuvi wa Mkoa wa Mwanza na mikoa ya jirani kama vile Kagera ikiwepo Kata ya Kerebe ambayo iko Bukoba, Ukerewe pamoja na Kalebezo na Kayenze wamekuwa wakiteseka sana na uporaji wa mali zao, hizi bodi pamoja na samaki, suala ambalo limekuwa likizorotesha sana uchumi wa wavuvi, je, ni lini sasa Serikali itatimiza ahadi yake ambayo imekuwa ikiahidi kwa takribani miaka kumi sasa ya ununua boti ambazo zinaweza zikafanya doria ili kuwakamata hawa wahalifu ambao wanawapora wavuvi mali zao? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na mkakati, mkakati upo na kuna mahitaji ya task force ambayo inahusisha wadau mbalimbali na majukumu yake makubwa ni kukabiliana na uhalifu katika maeneo ya majini. Kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi kwamba mikakati hiyo ikiwemo katika eneo ambalo anazungumzia Mheshimiwa Mbunge ya Ziwa Victoria, tulipeleka hiyo timu na tukaweza kubaini upungufu kadhaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wenyewe ambao umeelekezwa ni kwamba kuna umuhimu wa kuweza kupata boti zaidi zenye uwezo mkubwa zaidi kwa ajili ya kukabiliana na uhalifu huo. Ndiyo maana nikamweleza katika jibu la msingi kwamba Serikali inafanya jitihada kuweza kupata boti hizo za kisasa ili kuweza kudhibiti hali hiyo. Kuhusiana na kwamba wahalifu hawa wanatoka ndani au nje; ndiyo maana nimemwambia kwamba tunashirikiana na nchi jirani ili kuweza kuwabaini na kuwachukulia hatua za kisheria kupitia Wizara yetu ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

KITETO Z. KOSHUMA (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Wavuvi wa Wilaya ya Rorya wanaovua katika Ziwa Victoria wamekuwa wakitekwa, kunyang’anywa nyavu zao pamoja na injini za boti. Aidha, majambazi wanaofanya vitendo hivyo hutumia silaha nzito na inasemekana ni wanajeshi kutoka Uganda. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongea na Serikali ya Uganda ili kukomesha uvamizi huo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, kuna mambo mengine Serikali haitakiwi hata iyaseme, kwa sababu yanaitia Serikali aibu. Wavuvi wanasema wanawafahamu, ni Waganda. Sasa ni kitu rahisi, kwa nini Serikali isikae na wavuvi, wavuvi wakasaidia kuwa- identify hawa watu? (Makofi)

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Selasini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa hizi kwamba kuna majambazi kutoka mje ya nchi wanavamia wavuvi huko ziwani, hata mimi nimepata kuzisikia, lakini baada ya kufanya verification kwa kuongea na wavuvi wenyewe, mimi naongea nao wengi tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuongea na wavuvi wenyewe hasa katika visiwa vya huku Mara, kilichothibitika ni kwamba ni Watanzania hawa hawa ambao wanajifanya kwamba ni wageni wanapoenda kwenye visiwa jirani kwa kujifanya wanaongea lugha ambayo kama siyo Kiswahili sawa sawa. Ajenda ya kwamba ni majambazi kutoka sijui nchi za jirani, siyo sahihi. Hawa watu wanafahamika na tumeshatoa taarifa kwa uongozi wa Mkoa wa Mwanza wawatafute kwa sababu at least identity zao sasa zinafahamika. (Makofi)