Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kabla sijaruhusu swali langu kujibiwa naomba marekebisho madogo kwenye majina yangu yaliyo kwenye majibu ya Waziri. Jina langu Samson halina (iiI kule mwisho na jina langu Bilago halina N katikati halisomeki Bilango linasomeka Bilago. MHE. KASUKU S. BILAGO aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya wastaafu kutolipwa mafao yao baada ya kustaafu:- (a) Je, kuanzia Januari hadi Disemba, 2015 ni watumishi wangapi wa umma wamestaafu utumishi? (b) Je, kati ya hao ni wangapi wamelipwa mafao yao? (c) Kama kuna ambao hawajalipwa, je, ni kwa sababu gani?

Supplementary Question 1

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu yaliyotolewa na Wizara ambayo hayakidhi viwango.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna wastaafu zaidi ya idadi iliyotolewa na hasa walimu, hata Jimboni kwangu Buyungu idadi kubwa ya walimu waliostaafu inaweza ikaakisi idadi ya watumishi walistaafu katika nchi hii. Sababu zilizotolewa za wastaafu hao kutolipwa moja kubwa ni kukosa fedha kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ambayo Serikali haijataja.
Swali la kwanza, naomba Serikali ikiri ni lini italipa wastaafu wote kwa kupeleka fedha kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ili wasiendelee kuteseka sambamba na kuwarudisha nyumbani kwao mara baada ya kustaafu? (Makofi)
Swali la pili, wapo wastaafu wa aina mbili, wapo wanaolipwa pensheni na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na wapo wanaolipwa pensheni na Hazina. Wale wa Mifuko wa Hifadhi ya Jamii wanapata monthly pension wale wahazina wanalipwa kwa miezi mitatu (quaterly pension) hali hii inawasumbua na kuwatesa wastaafu wetu. Naomba wastaafu wote walipwe monthly pension kama ilivyo kwenye mkataba wa kazi. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naomba uulize swali, naona unaleta ombi.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Swali la pili dogo, ni lini Serikali itaanza kuwalipa wastaafu wote pensheni ya kila mwezi badala ya miezi mitatu? Ahsante!

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kumhakikishia data nilizompatia ni za kweli na za uhakika, kwa hiyo naomba aamini hao ndiyo wastaafu ambao tunajua wamestaafu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili sababu nilizozitaja ndizo zinazosababisha wastaafu hao wachelewe kulipwa siyo upelekaji wa fedha. Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwenye Mifuko hii ili waweze kulipwa wastaafu hawa na hizi sababu nilizozileta ndizo ambazo tunazifahamu kama Serikali na Mifuko yote imeendelea kupokea fedha kutoka Serikalini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, wastaafu wanaolipwa Hazina kulipwa kwa miezi mitatu mitatu. Naomba nilieleze Bunge lako Tukufu kwamba uamuzi wa Serikali kuelekea kulipa miezi mitatu mitatu lilifikiwa baada ya maombi ya wastaafu hawa kuomba walipwe miezi mitatu mitatu. Kama itaonekana sasa wataomba tena walipwe mwezi moja moja, Serikali haioni ugumu wowote kurejea kule tulikotoka.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kabla sijaruhusu swali langu kujibiwa naomba marekebisho madogo kwenye majina yangu yaliyo kwenye majibu ya Waziri. Jina langu Samson halina (iiI kule mwisho na jina langu Bilago halina N katikati halisomeki Bilango linasomeka Bilago. MHE. KASUKU S. BILAGO aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya wastaafu kutolipwa mafao yao baada ya kustaafu:- (a) Je, kuanzia Januari hadi Disemba, 2015 ni watumishi wangapi wa umma wamestaafu utumishi? (b) Je, kati ya hao ni wangapi wamelipwa mafao yao? (c) Kama kuna ambao hawajalipwa, je, ni kwa sababu gani?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona, nina swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, wastaafu ambao wanapitia Mfuko PSPF hivi karibuni Serikali iliongeza kiwango, lakini wastaafu hawa wanakuwa hawalipwi kwa wakati na kwa kiwango ambacho Serikali ilitangaza.
Je, ni lini sasa Serikali itaanza kuwalipa wastaafu hawa kwa kiwango sahihi na kwa wakati muafaka?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu tatizo hili lilkuwepo PSPF, lakini kuanzia Disemba 2015 mpaka leo wastaafu hao wamekuwa wakilipwa pesa zao inavyostahili. Kuanzia Disemba hiyo tumeanza kulipa hao wastaafu shilingi 100,000/= kama ambavyo Serikali iliongeza kiwango hiki kupitia Mfuko wa PSPF na arrears zao mpaka kufikia mwisho wa mwezi huu wa nne wote watakuwa wamelipwa zile arrears za kutoka Julai hadi Disemba.

Name

Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kabla sijaruhusu swali langu kujibiwa naomba marekebisho madogo kwenye majina yangu yaliyo kwenye majibu ya Waziri. Jina langu Samson halina (iiI kule mwisho na jina langu Bilago halina N katikati halisomeki Bilango linasomeka Bilago. MHE. KASUKU S. BILAGO aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya wastaafu kutolipwa mafao yao baada ya kustaafu:- (a) Je, kuanzia Januari hadi Disemba, 2015 ni watumishi wangapi wa umma wamestaafu utumishi? (b) Je, kati ya hao ni wangapi wamelipwa mafao yao? (c) Kama kuna ambao hawajalipwa, je, ni kwa sababu gani?

Supplementary Question 3

MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Mheshmiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali imekuwa na tabia tata ya kuchukua fedha kwenye Mashirika ya Umma kama NSSF, LAPF na Mashirika mengine na kutokuzirudisha kwa wakati, ama kuwekeza katika miradi mfu kama mradi wa Machinga Complex na miradi mingine ambayo imekuwa haina tija Serikalini.
Ni lini Serikali itakoma mchezo huu wa kuchukua fedha ambazo zinawaathiri wachangiaji?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali imekuwa ikichukua fedha na hii ikifuata taratibu zote na Mifuko hii kuingia katika Mikataba ili Mifuko hii iweze kuwekeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali itasitisha utaratibu huu, siamini sana kwamba ni sahihi sana Serikali kusitisha, kama Mifuko inaweza kuwekeza na wakaingia katika mikataba ambayo tunaita ni Win Win Situation kati ya Serikali na Mifuko naamini ni sehemu nzuri ya uwekezaji kwa mifuko yetu hii. Kwa hiyo, naomba tuendele kufanya hivyo.