Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Viwanda vingi vya Moshi vilibinafsishwa havifanyi kazi, badala yake vimegeuzwa kuwa maghala ya kuhifadhia bidhaa mbalimbali na vimechakaa sana; aidha mafao ya wafanyakazi waliostaafishwa katika Kiwanda cha Magunia na Kilimanjaro Timber Utilization hayakulipwa inavyostahili na hivyo kuwepo kwa malalamiko ya muda mrefu ya madai yao bila mafanikio:- (a) Je, kwa nini Serikali isivikabidhi viwanda hivyo kwa kampuni nyingine zenye uwezo wa kuviendeleza na hivyo kupunguza tatizo la ajira katika Mji wa Moshi? (b) Je, ni lini madai ya mafao ya wafanyakazi waliostaafishwa katika viwanda hivyo yatalipwa?

Supplementary Question 1

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa majibu ya namna hiyo kuhusu viwanda vya Moshi yamekuwa yakitolewa mara kwa mara katika Bunge lako Tukufu bila utekelezaji; na kwa kuwa ilikuwa ni moja wapo ya ahadi ya Mheshimiwa Rais kwamba kwa muda mfupi sana viwanda vile vingetwaliwa kwa waliovitumia bila utaratibu.
Je, Serikali haioni sasa ni wakati wa kutoa muda halisi kwa maana ya time frame ya lini viwanda hivyo vitatwaliwa kwa watu ambao wameshindwa kuvifanyia kazi katika malengo halisi yaliyokuwa yametarajiwa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa majibu ya Serikali hayaakisi ukweli ulivyo kuhusu wafanyakazi, kwa sababu madai yao ni ya msingi na fedha wanazodai siyo za mikataba ya hiari na wamekuwa wakidai fedha hizo tangu mwaka 1998, na kwa kuwa Serikali haijataka kuwa karibu nao…
NAIBU SPIKA: Naomba uulize swali tafadhali!
MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Je, ni lini sasa Serikali itakuwa tayari kuanza kufuatilia ukweli wa madai hayo na kuwa karibu na hao wafanyakazi ili waweze kutoa ufafanuzi unaoridhisha wafanyakazi hao kuondoa manung’uniko yao? Ahsante sana.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na (b) suala la maslahi ya wafanyakazi ni lako wewe, ni langu mimi. Wewe kama Mwakilishi wao na mimi kama Kiongozi wa Serikali, mimi na wewe tuwasiliane tutakwenda wote mpaka Moshi tuwaone hao watu tuzungumze nao tutakwenda kwa Msajili wa Hazina, tutaweza kujua mbichi na mbivu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali (a) Mheshimiwa Rais amezungumza bayana, na mimi nimekuwa nikizungumza mara nyingi kuhusu viwanda ambavyo havifanyi kazi. Jambo moja ambalo tunapaswa kulielewa kuna suala la kisheria kuhusu hivi viwanda vilivyobinafsishwa, kwa hiyo, tunajitahidi kufuata hizo sheria kusudi tuvitwae kisheria kusiwepo migongano. Nia yetu nikuona hivyo viwanda vinafanya kazi haraka sana, hatutaki kwenda mahakamani. Kwa hiyo, viwanda hivyo vitatwaliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na jitihada za kuvitwaa tunawafuata wale watu ni Watanzania wenzetu tunawauliza kitu gani kilichowasibu? Sababu nyingine zina mantiki na kuna baadhi ya viwanda vimeshaleta proposal namna gani vitaweza kufufuliwa. Tumewapa wataalam watu, wataalam wa Wizara yangu wawasaidie hao waliovichukua, hasa wale Watanzania wazawa tuweze kuona wanatoa bidhaa tulizotegemea.
Moja ya sababu ni kwamba soko tulilokuwemo lilikuwa linaleta bidhaa ambazo lilikuwa linafanya viwanda vyetu nchini visiwe competitive hilo suala ni historia Mheshimiwa Rais na Waziri wa Fedha wamelisulihisha bidhaa zinaingia kwa kulipa kodi na bidhaa standard. Kwa hiyo, viwanda vya Watanzania waliopewa vitafanyakazi na hiyo ni kazi yangu tulishughulikie mnisaidie Waheshimiwa Wabunge.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Viwanda vingi vya Moshi vilibinafsishwa havifanyi kazi, badala yake vimegeuzwa kuwa maghala ya kuhifadhia bidhaa mbalimbali na vimechakaa sana; aidha mafao ya wafanyakazi waliostaafishwa katika Kiwanda cha Magunia na Kilimanjaro Timber Utilization hayakulipwa inavyostahili na hivyo kuwepo kwa malalamiko ya muda mrefu ya madai yao bila mafanikio:- (a) Je, kwa nini Serikali isivikabidhi viwanda hivyo kwa kampuni nyingine zenye uwezo wa kuviendeleza na hivyo kupunguza tatizo la ajira katika Mji wa Moshi? (b) Je, ni lini madai ya mafao ya wafanyakazi waliostaafishwa katika viwanda hivyo yatalipwa?

Supplementary Question 2

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana pia kuniruhusu na mimi niulize swali la pili la nyongeza.
Mheshimiwa Waziri wa viwanda na Biashara amejibu majibu mazuri sana, kwa ujumla lakini ningependa na mimi kujua kwamba suala la viwanda vilivyobinafsishwa limekikumba kiwanda chetu cha Nyuzi cha Tabora. Ningependa Mheshimiwa Waziri aniambie ana mkakati gani hasa wa Kiwanda cha Nyuzi Tabora ambacho kilikuwa kinasaidia wakulima wote wa Pamba katika Kanda ya Ziwa Magharibi? Ahsante sana.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanda cha Nyuzi Tabora mmiliki wa Kiwanda hicho ameshaitika wito kwa Msajili wa Hazina, madai yake yeye anasema nyuzi zake hazina soko.
Kwa hiyo, tunashirikiana naye ili tuweze kupata soko la nyuzi zake lakini tuweze kuona kiwanda kile kinafanya kazi. Nyuzi zake zilikuwa zinakosa soko, mtu anakuambia kiwanda hiki nyuzi hazina soko na hayo niliyowaeleza bidhaa kutoka nje ndiyo mojawapo ya mambo yaliyokuwa yanatuumiza. Kwa hiyo, tuko nae bega kwa bega, wataalam wanafanyia kazi, na nitakuja kuleta mrejesho kwa watu wa Tabora ili kusudi kiwanda chenu kiweze kufanya kazi vizuri.

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Viwanda vingi vya Moshi vilibinafsishwa havifanyi kazi, badala yake vimegeuzwa kuwa maghala ya kuhifadhia bidhaa mbalimbali na vimechakaa sana; aidha mafao ya wafanyakazi waliostaafishwa katika Kiwanda cha Magunia na Kilimanjaro Timber Utilization hayakulipwa inavyostahili na hivyo kuwepo kwa malalamiko ya muda mrefu ya madai yao bila mafanikio:- (a) Je, kwa nini Serikali isivikabidhi viwanda hivyo kwa kampuni nyingine zenye uwezo wa kuviendeleza na hivyo kupunguza tatizo la ajira katika Mji wa Moshi? (b) Je, ni lini madai ya mafao ya wafanyakazi waliostaafishwa katika viwanda hivyo yatalipwa?

Supplementary Question 3

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa swali la Mheshimiwa Raphael Japhary linafanana na hali ilivyo Moshi Vijijini, kuna kiwanda kilifunguliwa mwaka 1975 na Mwalimu Nyerere na kiwanda kile ni cha ngozi hakikupata mwekezaji mpaka leo, na kimepangishwa kwa shilingi 20,000 kwa mwezi. Naomba Waziri aniambie ni lini atakuwa tayari kwenda kuona hiyo hali nakuchukua hiyo hatua zinazoyostahiki?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Antony Komu, Waziri Kivuli wa Viwanda Biashara na Uwekezaji kuhusu kiwanda chake cha mwaka 1975 Moshi ambacho hakukitaja jina. Kwa kweli nitakudanganya nikisema ninakijua kwa sababu hukukitaja jina, niko tayari wewe unipeleke unionyeshe kiwanda tukitafutie majawabu.

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Viwanda vingi vya Moshi vilibinafsishwa havifanyi kazi, badala yake vimegeuzwa kuwa maghala ya kuhifadhia bidhaa mbalimbali na vimechakaa sana; aidha mafao ya wafanyakazi waliostaafishwa katika Kiwanda cha Magunia na Kilimanjaro Timber Utilization hayakulipwa inavyostahili na hivyo kuwepo kwa malalamiko ya muda mrefu ya madai yao bila mafanikio:- (a) Je, kwa nini Serikali isivikabidhi viwanda hivyo kwa kampuni nyingine zenye uwezo wa kuviendeleza na hivyo kupunguza tatizo la ajira katika Mji wa Moshi? (b) Je, ni lini madai ya mafao ya wafanyakazi waliostaafishwa katika viwanda hivyo yatalipwa?

Supplementary Question 4

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa Mwanza tuna Kiwanda cha Tanneries ambacho sasa kimegeuzwa kuwa chuo.
Je, Serikali ina mpango gani wa kukirudisha hicho kiwanda ili kiweze kufanya kazi iliyokusudiwa?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Mwanza kuhusu kiwanda cha Mwanza TANNERIES, ambacho kimegeuzwa kuwa chuo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Katibu Mkuu anayeshughulikia Biashara na Uwekezaji Profesa Mkenda, alikuwa Mwanza wiki iliyopita, kile kiwanda kitaendelea kuwa Chuo na tunalenga kuwafundisha wananchi namna ya kutengeneza nguo, ni Technical School ni VETA ambayo itasaidia watu wa nguo, lakini kando na eneo hilo, kuna Kiwanda cha Ngozi, hicho ndicho tatizo mtu aliyepewa amekigeuza hifadhi ya makatapila na matrekta tunataka kifanyekazi. Kwa hiyo, chuo kitaendelea kufanyakazi tunawafundisha vijana, wanakwenda kwenye viwanda vyao vidogo vidogo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo ni huyo mtu ambaye kiwanda cha Ngozi cha Mwanza amekigeuza hifadhi na kuja Mwanza tarehe 30 na nitakwenda kushughulikia, tarehe 30 mwezi huu.