Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:- Hospitali za Serikali zimeandaliwa kupata huduma za dawa MSD lakini wakati mwingine baadhi ya dawa zimekuwa hazipatikani MSD na hospitali haziruhusiwi kununua dawa nje ya MSD. Je, Serikali imetoa maelekezo gani pale ambapo MSD wamekuwa hawana baadhi ya dawa hizo zinazohitajika kwa wagonjwa?

Supplementary Question 1

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwanza, niipongeze Wizara hii kwa maana ya MSD kwa kuwa sasa wanatoa dawa za kutosha katika hospitali zetu. Hata hivyo, kwa kuwa hospitali hizi zinapokuwa zinakosa hivi vifaa tiba, kama ambavyo amezungumza kwenye jibu lake la msingi, kwamba wanaruhusu kwenda kununua kwa wazabuni, haoni kwamba kitendo cha kwenda kununua kwa wazabuni bei ni kubwa mara mbili zaidi ya vile vifaa ambavyo wanakwenda kuvinunua kama vile dawa za amoxicillin pamoja na vile vifaa vya theater. Hawaoni kwamba sasa inakuwa ni gharama kubwa zaidi kuwahudumia hao wagonjwa ambao wanaokwenda kwenye hizi hospitali? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, pili, kwa kuwa anasema kwamba mteja apewe ndani ya siku moja ili kwenda kununua kwenye haya maduka ya watu binafsi. Kwa nini isiwe ndani angalau ya wiki moja kuliko ile siku moja ili mtu apate nafasi nzuri ya kuweza kwenda kununua hizo dawa?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza, ni kweli kwamba bei kwenye sekta binafsi zinaweza zikawa kubwa ukilinganisha na bei zilizopo kwenye maghala ya MSD. Sababu ni nyingi, mojawapo ikiwa ni kwamba kwenye MSD kwa sasa kwa sababu tunanunua dawa moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji tumeshusha gharama ya manunuzi ya dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi kwa asilimia takribani 40 na kwa hiyo bei ya dawa MSD iko chini sana ukilinganisha na kwenye sekta binafsi.
Mheshimiwa Spika, lakini kinachosababisha tushindwe ku-take advantage ya bei ya MSD kuwa chini ni kujaribu kuongeza ufanisi kwamba pale ambapo hatuna dawa kwa kiasi fulani tusicheleweshe wananchi kupata huduma ya dawa kwa sababu tu tunataka vituo vyetu vipate dawa kutoka MSD, basi tuwape fursa Halmashauri waende wakanunue dawa kwenye sekta binafsi ili dawa zisikosekane kwa wateja pale kwenye kituo cha kutolea huduma za afya. Haya yalikuwa ni malalamiko ya muda mrefu, kabla hata sisi hatujateuliwa kwenye nafasi hizi malalamiko ya dawa yalikuwa mengi sana na Waheshimiwa Wabunge wengi walitamani Halmashauri zao ziruhusiwe kwenda kununua dawa kwenye sekta binafsi, kwa sababu kisheria hairuhusiwi kabisa lakini tumeamua kufanya maboresho ambayo yanaongeza tija na ufanisi wa MSD ili kuhakikisha tunaharakisha upatikanaji wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya wakati ambapo Halmashauri zina pesa na MSD haina stock ya dawa fulani.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, niwathibitishie na kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge na wananchi wote kwa ujumla kwamba baada ya kuongeza ufanisi wa MSD, kwa sasa upatikanaji wa dawa umeongezeka kwa zaidi ya asilimia 80. Kwenye Halmashauri nyingine ambazo natembelea nakuta upatikanaji wa dawa umekuwa mpaka katika kiwango cha asilimia 90, asilimia 95, dawa zote muhimu zinapatikana.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, tunatoa saa 24 kile kibali cha Out of Stock (OS) kwa sababu tunataka kuongeza ufanisi kama nilivyosema. Kuliko kusema tutoe wiki nzima ndiyo tutoe kile kibali cha Halmashauri kwenda kununua dawa, maana yake tutakuwa tumewachelewesha wananchi kupata dawa kwa wiki nzima.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hii kwenda kwenye 24 hours maana yake tunataka ufanisi uwe ni wa hali ya juu na wananchi wasikose dawa.

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:- Hospitali za Serikali zimeandaliwa kupata huduma za dawa MSD lakini wakati mwingine baadhi ya dawa zimekuwa hazipatikani MSD na hospitali haziruhusiwi kununua dawa nje ya MSD. Je, Serikali imetoa maelekezo gani pale ambapo MSD wamekuwa hawana baadhi ya dawa hizo zinazohitajika kwa wagonjwa?

Supplementary Question 2

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kumekuwa na tatizo kubwa sana na uhaba mkubwa wa dawa ya morphine kwenye hospitali zetu ambayo inapelekea wagonjwa hususani wa cancer kuteseka na maumivu makali sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu, je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuweka dawa hii ya morphine kwenye list ya dawa muhimu au National Essential Drug List ili ziweze kupatikana kirahisi na kuwaponya maumivu wagonjwa hawa wa cancer? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, kwamba dawa ya morphine iwekwe kwenye Essentials Medicine List ni kitu ambacho katika hali ya sasa ya nchi yetu hatuwezi kukikubali kwa sababu ni katika dawa ambazo ziko controlled na kwamba ili kuzitoa ni lazima kuwe kuna ujuzi fulani unaohitahijika kuwepo katika kituo hicho ndipo mtu aweze kuruhusiwa kutoa dawa hiyo. Ndiyo maana inatolewa kwa kibali maalum, inatunzwa kwa kibali maalum na hatuwezi kubadilisha hilo kwa sababu dawa ya morphine ina madhara kama ikiwa administered na mtu ambaye hata ujuzi wa namna ya kuitunza na namna ya kui-prescribe.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:- Hospitali za Serikali zimeandaliwa kupata huduma za dawa MSD lakini wakati mwingine baadhi ya dawa zimekuwa hazipatikani MSD na hospitali haziruhusiwi kununua dawa nje ya MSD. Je, Serikali imetoa maelekezo gani pale ambapo MSD wamekuwa hawana baadhi ya dawa hizo zinazohitajika kwa wagonjwa?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. GODWIN A. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, hili suala la dawa linaonesha ni tatizo sugu na swali langu ni kwamba ukilinganisha vituo vya afya vya binafsi na hata maduka ya binafsi na MSD, dawa ambazo hazipatikani Serikalini mara nyingi zinapatikana kwenye vituo binafsi.
Mheshimiwa Spika, je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kutuambia ni kwa nini vituo binafsi vinakuwa na dawa zote wakati Serikali inashindwa kuwa nazo na imekuwa ni tatizo sugu, tufanye nini kama nchi?
Mheshimiwa Spika, hapa amezungumzia suala la morphine pamoja na ku-control, lakini ni dawa ambayo kwa kweli inahitajika kwenye vituo vya Serikali kwa sababu watu maskini wanateseka sana. Pamoja na control hizo zote ambazo tunazisema lakini kwa kuzingatia hizo control ni muhimu hizo dawa ziwepo kwenye vituo vyetu. Unatuambia nini kwa sababu kwa kweli hili ni suala sungu na ni aibu kwa Seriali kwa sababu kwanza tunanunua kutoka kwa mtengenezaji, kwa nini hatuna dawa?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mollel...
Mheshimiwa Spika, basi nachangua kujibu lile la kwanza, kwamba kwa nini kwenye baadhi ya vituo vya Serikali hakuna baadhi ya dawa wakati kwenye private zipo.
Mheshimiwa Spika, ukweli ni kama nilivyoeleza kwenye majibu yangu ya msingi lakini pia kwenye maelezo ambayo nimeyatoa kwenye maswali mbalimbali ya nyongeza ambayo yamekuwa yakiulizwa hapa Bungeni ni kwamba huko tunakotoka hali ya upatikanaji wa dawa ilikuwa chini sana na sababu zilikuwa nyingi.
Mheshimiwa Spika, sababu mojawapo ilikuwa ni hiyo ya maoteo kujua mahitaji ya Halmashauri zote nchini kabla mwaka haujaanza na hii ni kwa mujibu wa sheria kwamba inatakiwa kila Halmashauri kufikia Januari ya kila mwaka wawe wameleta maoteo yao ya mahitaji ya dawa MSD na MSD ijipange kununua kadri ambavyo itaweza na kadri ambavyo inajua kwamba mahitaji ya dawa yametathminiwa na Halmashauri husika. Sasa mwaka jana tulikuja kugundua Halmashauri nyingi hazikuwa zikileta maoteo kwa hivyo unakuta Halmashauri wana pesa, halafu MSD ana bajeti ndogo kiasi kwamba hawezi ku-meet mahitaji ya Halmashauri ambao wana pesa zao tayari. Ndiyo maana tukaanzisha hii saa 24 kutoa kibali cha kwenda kununua kwenye private sector.
Mheshimiwa Spika, sababu nyingine ni kwamba dawa nyingi hazipatikani hapa nchini kwenye viwanda na sisi tuna maelekezo ya Mheshimiwa Rais ya kununua dawa moja kwa moja kutoka viwandani na sasa ili tuweze ku-meet hayo maelekezo tulikuwa tunapaswa kufanya mambo yafuatayo; tutanue mtaji wa MSD na ndicho ambacho tumekifanya. Mheshimiwa Rais ametuongezea bajeti ya dawa kutoka shilingi bilioni 31 mwaka juzi mpaka shilingi bilioni 251.5 mwaka jana na mpaka shilingi bilioni 299 mwaka huu. Tatizo la fedha sasa limeanza kupungua kwa hivyo sasa tuna uwezo wa ku- order dawa kadri ambavyo tunaona mahitaj ya nchi yatakuwa katika mwaka husika na kupanga schedule ya supply kila baada ya miezi mitatu itakuwaje.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, baada ya kufanikisha hilo, ndiyo maana nimesema pale awali, mahitaji ya dawa sasa tuna uwezo wa kuya-meet katika nchi kwa wastani wa asilimia 80 na kuna baadhi ya Halmashauri ambazo zina viongozi wazuri ma-DMO wazuri, Wakurugenzi wazuri wanaweza kufika mpaka asilimia 90. (Makofi)
Kwa hiyo, tukisema kuna baadhi ya dawa hazipo Serikalini na kuna baadhi ya dawa zipo kwenye private sector ni kweli, lakini angalau sisi tumehakikisha kwenye ile list ya essential medicines, dawa 138 za muhimu zaidi tunazo na kuna zile tracer medicine 30 tunazo wakati wote. Kwa hiyo, kuongelea kwamba dawa fulani ipo huku private na huku Serikalini haipo linaweza likawa ni suala kidogo relative lakini objectivity yake ni kwamba angalau tuna uhakika makundi yote ya dawa yanapatikana, anti-biotics zipo, anti inflammatories zipo dawa zote essentials zinapatikana kwenye vituo vya kutolea huduma vya Serikali.
Sasa hivi mimi nazunguka sana pengine kuliko Mheshimiwa Mbunge, sijapata malalamiko ya dawa tena takribani mwaka mzima umepita. Nakushukuru.