Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:- Je, Serikali inatumiaje fedha za Mfuko wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi (Adaptation Fund) zinazotolewa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi?

Supplementary Question 1

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuangalia mpango wa kitaifa ambao ulikuwa umeweka vipaumbele 13 ambao ni National Adaptation Program of Action kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi Serikali iliweka vipaumbele 13 ambavyo vya kwanza vilihusu masuala ya maji pamoja na kilimo, lakini katika utekelezaji Serikali hela iliyopata imeweka katika ujengaji wa ukuta katika barabara ya Ocean Road na miundombinu mingine katika maeneo ya Dar-es-Salaam. Sasa Serikali haioni kwamba, inaruka vipaumbele vyake ambavyo iliviweka mwanzo na inakwamisha sasa kuhakikisha kwamba, nchi inakuwa na uwezo wa kuwa na uhakika wa suala zima la usalama wa chakula katika kuangalia hilo suala la vipaumbele?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala lingine ni katika suala zima la NEMC ambalo lilichaguliwa na Makamu wa Rais, ili kuweza kupata hii ithibati. Imechukua sasa miaka mitano kupata hii accreditation na NEMC hawajaweza kupata. Tunavyopata pesa kupitia Multinational Implementation Entities Serikali inakatwa asilimia 10 na hizo taasisi kwa hiyo, NEMC ilivyopata hizo hela tulikatwa asilimia 10 kwa hiyo, inapunguza hela ambazo zingesaidia katika utekelezaji wa miradi ya kuweza kupunguza kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Serikali ina mkakati gani na lini hasa kwa sababu, NEMC imeshachukua miaka mitano, Serikali sasa ni lini itakamilisha mchakato mzima na kukamilisha vigezo vyote, ili hatimaye Serikali iweze kuwa inapata hela zake moja kwa moja? (Makofi)

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, linahusu Serikali ilikuwa imeweka vipaumbele 13, lakini Serikali ikaamua kuchukua mradi ule wa Dar-es-Salaam kuhakikisha kwamba, wanaokoa fukwe zetu na kutekeleza shughuli zile ambazo zinahusu kutengeneza mifereji ya maji ya mvua na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba, vipaumbele vyote ni muhimu, lakini pia tunaangalia katika vipaumbele vile, ukiacha pembeni kipaumbele ambacho tumeshaanza kukifanyia kazi, huwezi ukasema kwamba, hakina umuhimu kuliko hiyo ya kilimo. Hata hivyo, niseme tu kwamba, kama anavyojua katika ombi mradi huu una sehemu ya pili ambayo sasa hivi Serikali inaifanyia kazi. Suala la kusema kwamba labda NEMC imechukua muda mrefu, sasa miaka mitano kufanya process ya kupata usajili, ili iweze yenyewe moja kwa moja kuomba sehemu ya pili ya fedha hizi, kwa sababu najua kwamba ilikuwa inatakiwa iwe milioni kumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimwambie tu Mheshimiwa Peneza kwamba tayari NEMC imeshapita vile vigezo vyote ambavyo vilikuwa vimewekwa na hivi karibuni itaanza sasa yenyewe. Itapata usajili na kuanza kuomba ile sehemu ya pili ya fedha ambazo zinatakiwa kuokoa mazingira yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile nimwambie tu kwamba, NEMC baada ya kupata huu usajili itaanza sasa kuangalia hivi vipaumbele ambavyo yeye amevizungumzia; kuhusu mambo ya kilimo. Vile vile labda nimwambie kwamba licha ya Serikali kutumia Mfuko huu wa Adaptation Fund tuna Mifuko mingine ambayo pia inaangalia masuala ya kilimo na umwagiliaji. Kwa hiyo, labda nimhakikishie tu kwamba, baada ya NEMC kupewa usajili ambao tayari imeshapita katika vigezo vile, sasa hivi tunasubiri wapewe hiyo barua ya accreditation ili waweze kuianza hii process ya kuchukua hizi hela milioni tano.