Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Katika Tarafa ya Kamsamba kuna Shule ya Sekondari ya Wazazi inayomilikiwa na Jumuiya ya Wazazi ya CCM ni muda mrefu sasa shule hiyo haitumiki na haina mwanafunzi hata mmoja na hivyo kufanya majengo yake kuharibika. Je, kwa nini Serikali ya Awamu ya Tano isirudishe shule hiyo kwa wananchi ili waweze kuitumikia au kubadili matumizi na kuwa Chuo cha Ufundi?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kukubali kwamba watafanya mazungumzo na mmiliki ambaye ni Chama cha Mapinduzi, shule hii ni muda mrefu sana imefungwa, karibu miaka kumi hamna mwanafunzi anayesoma pale. Ni kwa nini msione sasa ni wakati muafaka wa kuirudisha kwa wananchi ili tuweze kuitumia?
Mheshimiwa Spika, ombi letu la pili, tunaomba shule hii tuitumie kwa ajili ya kidato cha tano kwa sababu Halmashauri ya Wilaya Momba haina shule ya kidato cha tano? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema shule hii inamilikiwa na Chama cha Mapinduzi kupitia Jumuiya yake ya Wazazi. Kwanza naishukuru Jumuiya ya Wazazi kwa sababu imefanya intervention kubwa kwa nchi hii kujenga shule mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa kweli naomba niweke katika kumbukumbu kwamba Jumuiya ya Wazazi kupitia Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, alitusaidia sana kupatikana kwa Shule ya Umumwani, ambayo Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo alikuja kutukabidhi pale na juzi nimeenda kule Kagera watoto wanasoma pale. Kwa hiyo, tunaishukuru sana jumuiya hiyo kwa kazi kubwa sana inayofanya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kama Serikali, hatuwezi kuirudisha tu hivi hivi, isipokuwa kuna utaratibu wa negotiation, pale Jumuiya ya Wazazi itakapoona inafaa, kwa sababu jukumu lake kubwa ni kuwasomesha watoto wa Tanzania kwa mbinu muafaka, basi inawezekana tukaongea na Mwenyekiti pale ambaye nadhani ni Mjumbe wa Kamati Kuu, aangalie nini cha kufanya, aidha kuiboresha mwenyewe ili ichukue watoto ama kuangalia utaratibu kama alivyotusaidia kule Umumwani kwa lengo la kuwasaidia Watanzania. Hili siyo jambo baya sana.
Mheshimiwa Spika, katika suala zima la kuifanya shule hii iwe ya Kidato cha Tano na cha Sita, nadhani hili ni wazo zuri na Jumuiya ya Wazazi pale watakapoona, aidha wenyewe kuifanya na kuiboresha miundombinu yake iwe ya kidato cha tano na cha sita kwa Tanzania, ama kuirudisha Serikalini. Mwenyekiti wa jumuiya hiyo yuko humu, atatuelekeza nini tufanye kwa muktadha wa kusaidia wanafunzi na watoto wa Tanzania.
Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Katika Tarafa ya Kamsamba kuna Shule ya Sekondari ya Wazazi inayomilikiwa na Jumuiya ya Wazazi ya CCM ni muda mrefu sasa shule hiyo haitumiki na haina mwanafunzi hata mmoja na hivyo kufanya majengo yake kuharibika. Je, kwa nini Serikali ya Awamu ya Tano isirudishe shule hiyo kwa wananchi ili waweze kuitumikia au kubadili matumizi na kuwa Chuo cha Ufundi?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLA M. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Kabla sijauliza swali, naomba unipe nafasi kidogo niseme maneno mawili kidogo.
Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Silinde kama ameona mali za Chama cha Mapinduzi zinaweza kuja kuombwa Bungeni, nafikiri ni dalili nzuri kwamba naye anaelekea kuja CCM, karibu sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu linasema hivi, maombi haya yanayoletwa kwa ajili ya Shule ya Jumuiya ya Wazazi, Wizara naomba iniambie; je, kwa nini msishirikiane na Mbunge mkaimarisha shule nzuri ya Julius Nyerere ambayo inaonekana imeharibika, haifai, haina huduma nzuri, mpaka mwende kutafuta mali za CCM? (Kicheko/Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, nadhani Mheshimiwa Alhaji Bulembo alikuwa anatoa ushauri na mimi napenda kumpongeza sana kwa juhudi kubwa anayofanya katika shughuli zake.
Mheshimiwa Spika, nadhani ushauri huu kama Serikali tumeupokea, kwa sababu Mheshimiwa Alhaji Bulembo wewe ni mlezi wa watoto na ndiyo maana umeamua kujenga shule hizi na kuzisimamia. Kwa hiyo, tutakachokifanya ni kuboresha maeneo mbalimbali ili watoto wetu waweze kusoma kwa kadiri iwezekanavyo.