Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:- Kwa sasa kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo Jijini Dar es Salaam kimezidiwa uwezo wa kutoa huduma kwa ufanisi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha vituo vingine kikanda ili kuboresha huduma za usafiri wa mabasi yanayoingia na kutoka mikoani?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Kwa maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri inaelekea Serikali haijajipanga kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivyo. Kwa kuwa suala la ujenzi wa kituo cha mabasi cha Mbezi Luis ni la miaka mingi na kwa kuwa msongamano uliokuwepo pale Ubungo umekithiri na haileti sura nzuri kwa sababu sasa hivi nchi yetu inatakiwa iwe na kituo chenye hadhi ya Kimataifa. Swali la kwanza, je, ni lini Serikali iko tayari kuanza kujenga kituo cha mabasi katika maeneo ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyataja kwa maana ya mabasi ya Kusini, Kaskazini na yanayotoka Kanda ya Kati na nchi jirani? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa katika maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba kituo cha mabasi ya Kusini kinatarajiwa kujengwa Kongowe na ukiangalia eneo la Kongowe halina nafasi ambayo watajenga kituo bila kutumia pesa nyingi za Serikali.
Je, atakubaliana na mimi kwamba majibu haya hayako sahihi kwa sababu vikao vimeshaanza kufanywa kati ya Wizara ya Maliasili na Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga? Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kuanza kufanya upembuzi yakinifu katika hilo eneo la Vikindu au Mwanambaya huko Mkuranga? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Zaynabu Matitu Vulu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano imejipanga sana na ndiyo maana nilisema pale awali mipango yoyote lazima ipangwe katika utaratibu sahihi. Wiki iliyopita nilijibu swali la Mheshimiwa Mnyika linalofanana na swali hili. Kinachotokea ni nini? Serikali kupitia Jiji la Dar es Salaam imeweza kupata eneo la Mbezi Luis. Bahati nzuri Kamati yenye kuhusika ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa iliamua kwenda kujihakikishia na imejiridhisha kuwa ni eneo muafaka. Bahati nzuri sasa LAPF wameshakubali uwekezaji wa kituo hicho cha kisasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na hayo kuna mambo ya msingi lazima yafanyike. Wiki iliyopita Jiji pamoja na LAPF na wadau wengine walikaa kikao kujadili ujenzi wa kituo hicho ambao utagharimu takribani shilingi bilioni 28. Walikuwa wanajadili katika hicho kituo cha Mbezi Luis daraja litapita juu au chini kwenda katika kile kituo cha mabasi cha kawaida cha daladala. Hiyo haitoshi, tarehe 19 Mei, Kamati hii itakutana tena kufanya mjadala mpana kuona ni jinsi gani kituo hiki kinaenda kujengwa. Kwa hiyo, ndiyo maana nimesema kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano imejipanga sana na tutahakikisha tunajenga vituo katika Jiji la Dar es Salaam ili kusaidia wananchi waweze kupata usafiri mzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kituo cha watu kutoka Kusini ni kweli, Jiji la Dar es Salaam sasa hivi linafanya tafakari kwa sababu yeye anaangalia mipaka yake. Walivyoangalia eneo lililokuwepo la Kongowe waliona kwamba ni lazima kulipa fidia. Kwa hiyo, kwa mkakati unavyokwenda, kwa mfano Kongowe mbele pale Vikindu kuna eneo kubwa, Serikali itaangalia jinsi gani stand ile itaweza kujengwa pale kwa watu wa Kanda ya Kusini na itahakikisha mipango hii yote inafanyika vizuri. Hata hivyo, agenda hii itaenda awamu kwa awamu lakini lazima tumalize kujenga vituo vyote.
Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba tutaweza kujenga vituo imara kabisa kama tulivyojenga pale Msamvu, Mpanda na maeneo mengine. Lengo kubwa ni wananchi waweze kusafiri vizuri katika nchi yao.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:- Kwa sasa kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo Jijini Dar es Salaam kimezidiwa uwezo wa kutoa huduma kwa ufanisi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha vituo vingine kikanda ili kuboresha huduma za usafiri wa mabasi yanayoingia na kutoka mikoani?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa kuwa kituo cha Mbezi Luis kimeshapata mwekezaji LAPF, Serikali inatuambiaje kuhusu kituo cha Boko na cha Temeke, wamewatafuta akina nani watakaosaidia kujenga vituo hivi kwa haraka ili kuondoa msongamano Dar es Salaam? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bulembo, Mbunge Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishukuru sana
swali la Mheshimiwa Mbunge na ndiyo maana nimesema Mbunge Maalum kwa sababu ana hadhi maalum katika nchi hii kutokana na nafasi zake alizokuwa nazo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa hivi Serikali tumepata wadau wetu wa LAPF tumeanza na kituo kile lakini hata hivyo tunaenda kutafuta wadau wengine kwa ajili ya kujenga kituo kile katika eneo la Boko na kituo cha Kanda ya Kusini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, niwaelekeze wenzetu wa Jiji la Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam na wadau wengine hasa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, ikiwezekana wakae na Halmashauri ya Mkuranga, kwa sababu eneo la kimkakati tayari lipo ambalo halina haja ya kulipa fidia kuona ni jinsi gani tuta-fast track hiki kituo ambacho tunaweza tukakijenga eneo la Mkuranga kwa watu wa Kusini ili wakapata unafuu zaidi.
Kwa hiyo, tunachukua mambo yote haya kwa kushirikisha wadau mbalimbali lengo ikiwa ni kujenga vituo ambavyo vitasaidia suala la usafiri katika nchi yetu.

Name

Halima Ali Mohammed

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:- Kwa sasa kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo Jijini Dar es Salaam kimezidiwa uwezo wa kutoa huduma kwa ufanisi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha vituo vingine kikanda ili kuboresha huduma za usafiri wa mabasi yanayoingia na kutoka mikoani?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA ALI MOHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimuulize suala moja Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali inatilia mkazo suala la kukusanya mapato kwa njia ya kielektroniki. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri ana mpango gani wa kuhakikisha katika kituo cha Ubungo wanakusanya mapato kwa njia ya kielektroniki wakati abiria wakiingia na wakati magari yakitoka? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme tumetoa maelekezo kwamba siyo maeneo ya vituo vya mabasi pekee isipokuwa maeneo yote, utaratibu wa Serikali ni kwamba tunaenda kukusanya mapato yote kwa njia ya kielektroniki.
Naomba nisisitize sana na nimuelekeze Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam ambapo eneo lile lipo, kama kuna upungufu kwamba sehemu zingine wamekusanya kwa njia ya kielektroniki na nyingine hawajakusanya washughulikie changamoto hiyo. Naomba niagize na mimi najua kwamba hilo zoezi limeshaanza katika Jiji la Dar es Salaam, kwamba ili kuziba mianya yote ile ya upotevu wa fedha, mifumo yote ya ukusanyaji wa mapato ya Serikali katika vituo ya mabasi, hospitali na maeneo mengine ni kwa kutumia mifumo ya kielektroniki na si vinginevyo.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:- Kwa sasa kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo Jijini Dar es Salaam kimezidiwa uwezo wa kutoa huduma kwa ufanisi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha vituo vingine kikanda ili kuboresha huduma za usafiri wa mabasi yanayoingia na kutoka mikoani?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amejibu kuhusiana na ujenzi wa kituo cha mabasi ya Kusini katika eneo la Jimbo la Mkuranga; na kwa kuwa uratibu wa zoezi zima la ujenzi wa kituo cha mabasi ya Kusini linasimamiwa pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kuhakikisha wanashirikiana vema, Wizara ya TAMISEMI, Maliasili na nyingine zinazohusika kuhakikisha kituo hiki cha mabasi ya Kusini kinapatikana kwa haraka katika eneo la Wilaya ya Mkuranga hasa maeneo ya msitu ule wa Vikindu? (Makofi)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba ujenzi wa vituo hivi vya mabasi ni uwekezaji mkubwa sana na ni vyanzo vikubwa vya mapato kwenye Halmashauri zetu. Ukizingatia Sheria ya Fedha ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa, huwezi kwa namna yoyote ile ukafanya mradi kwenye mamlaka ya Serikali ya Mtaa husika na mradi ule ukawa na wadau wengi nje ya utaratibu wa kuibua na kutekeleza mradi ule kutoka kwenye Halmashauri husika.
Kwa hiyo, kwa kuzingatia dhana ya ugatuaji wa madaraka (D by D), katika kusimamia sisi kama TAMISEMI tutajaribu sana kuhakikisha kwamba miradi hii ya vituo vya mabasi itafanywa na mamlaka za Serikali za Mitaa husika kwa kushirikiana na wadau wowote whether ni PPP au kwa kushirikiana na taasisi zetu za Mifuko ya Jamii, kwa vyovyote vile lakini mwenye mradi na mmiliki wa mradi atakuwa ni Halmashauri husika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kumueleza kwamba sisi kama Serikali kwa kushirikiana na TAMISEMI na Wizara ya Maliasili tutakuwa tu ni facilitator lakini pia kuwaondolea vikwazo ili waweze kutekeleza mradi huo. Hii naisema ni kwa maeneo yote, kwa Mbezi Luis lakini pia kwa Boko, utaratibu utakuwa ni huo huo.(Makofi)