Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:- Serikali iliahidi kuweka minara katika Kata ya Sindano, Mchauru, Lipumbiru na Lupaso. Je, ni lini minara hiyo itajengwa ili kuondoa tatizo la kutokuwa na mawasiliano katika maeneo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, ninaomba sasa kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba, TTCL walishalipwa fedha za sola za Kimarekani 94,000 na ilikuwa ni mwaka 2015. Je, Serikali kwa nini haijawasisitiza TTCL kukamilisha kazi hii ambayo imechukua muda mrefu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, miongoni mwa kata ambazo Kampuni ya Viettel ilikuwa imeshinda zabuni mwaka 2015 ni pamoja na kata ya Sindano, lakini hadi sasa kazi hiyo haijafanyika. Je, Mheshimiwa Waziri atalithibitishia Bunge hili kwamba Viettel watakwenda kufanya hiyo kazi?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeisisitiza sana TTCL ikamilishe kazi iliyoianza. Na kama utarudia tena sehemu ambayo nilijibu swali la msingi ni kwamba, kazi hii waliikamilisha, lakini waliikamilisha kwa kutumia teknolojia ya CDMA na sasa wanaondoka katika teknolojia hii ya CDMA kwa sababu teknolojia hii haiwawezeshi wao kuongeza hizi huduma za nyongeza za mobile money na banking kwa hiyo, wanabadilisha mtandao na mtakumbuka kuna wakati hapa Dodoma walizindua ile ya 4G LTE kwa hiyo, sasa wapo katika mpango huo wa kuzindua huo mtandao mpya na hivyo kazi hiyo tutahakikisha inakamilika mapema kama ambavyo wao wameahidi by June, 2017 watakuwa wamefika kule Lupaso na Lipumbiru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu Viettel, ninafahamu Viettel wamekuwa na matatizo kidogo kwa sababu ya mikataba na tunarekebisha kwa sababu, kuna baadhi ya kodi walikuwa wanatarajia wasilipe. Kwa hiyo, wameingiza vifaa vyao vya kuweza kutuletea mawasiliano, lakini vimekwama kidogo kwa sababu ya malipo ya kodi na tutahakikisha hilo linasuluhishwa haraka, wanalipa kodi inayotakiwa, ili hatimaye vifaa hivyo viende vikafanye kazi, vikasimikwe kule kulikokusudiwa.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:- Serikali iliahidi kuweka minara katika Kata ya Sindano, Mchauru, Lipumbiru na Lupaso. Je, ni lini minara hiyo itajengwa ili kuondoa tatizo la kutokuwa na mawasiliano katika maeneo hayo?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuwa, ni Wizara hiyohiyo ya Uchukuzi, ingawa niliomba swali namba 70.
Kwa kuwa mawasiliano ni haki ya kila Mtanzania, lakini
toka nchi imepata uhuru kuna maeneoa ambayo hayajapata mawasiliano, ikiweko kata ya Kala na Ninde. Ni lini Serikali itatimiza wajibu wake wa kupeleka mawasiliano katika hizo kata, ikizingatia ziko pembezoni? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie Serikali ina nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata mawasiliano na ndio sababu kubwa ya kuanzisha huu Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote. Kwa hiyo, mara tutakapopata fedha tutakuja huko ambako Mheshimiwa Aida umekueleza.

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:- Serikali iliahidi kuweka minara katika Kata ya Sindano, Mchauru, Lipumbiru na Lupaso. Je, ni lini minara hiyo itajengwa ili kuondoa tatizo la kutokuwa na mawasiliano katika maeneo hayo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo yanayowakumba wakazi wa Lulindi, Masasi, yanafanana kabisa na wakazi wa Wilaya ya Malinyi katika kata za Sufi, Kilosa Mpepo; swali langu, kata hizo ninazozitaja ni kwamba kama alivyosema jibu la msingi Mheshimiwa Waziri, kwamba, kupitia Mfuko wa Fursa ya Mawasiliano kwa Wote (UCAF), wamejenga minara miwili katika Kata ya Ngoeranga na kata ya Sufi, lakini minara hiyo ambayo imejengwa chini ya Tigo haifanyi kazi kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali nangu. Je, ni lini Serikali watarekebisha minara hiyo na vilevile kumalizia Kata zile mbili ambazo hazina mawasiliano kabisa, kata ya Sufi na kata nyingine?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwakikishie kwamba kata hizo mbili alizozieleza ambazo hazina mawasiliano kabisa ikiwa ni pamoja na kata ya Kilosa Mpepo, tutahakikisha kwamba tunazifikishia mawasiliano kwa kadri tutakapopata fedha na maadamu ulishawasilisha hilo mapema Mheshimiwa Mponda nadhani utakumbuka Mheshimiwa Waziri wangu alivyokujibu na nikuthibitishie lie jibu alilokupa Waziri wangu na mimi nitalifuatilia utekelezaji wake.
Mheshimiwa Mponda kuhusiana na kata mbili ambazo…
Alitaja kata nne na nimeongelea kata mbili, kata hizo mbili ambazo Tigo wamejenga minara nitazifuatilia kuhakikisha kwamba minara hiyo inafanya kazi.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:- Serikali iliahidi kuweka minara katika Kata ya Sindano, Mchauru, Lipumbiru na Lupaso. Je, ni lini minara hiyo itajengwa ili kuondoa tatizo la kutokuwa na mawasiliano katika maeneo hayo?

Supplementary Question 4

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali moja dogo la nyongeza.
Kwa kuwa suala la Lulindi linafanana kabisa na tatizo lililoko katika jimbo la Makambako. Makambako kuelekea usawa wa kwenda Mbeya ni kilometa mbili eneo moja linaitwa Majengo hakuna mawasiliano. Kilometa tano kuelekea usawa wa kwenda Njombe kijiji chenye eneo la Kyankena Kiumba hakuna mawasiiano; Kitandililo Mawandea hakuna mawasiliano. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka minara hii ilimawasiliano yaweze kupatikana katika maeneo hayo?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliongea na Mheshimiwa Deo Sanga kutokana na matatizo hayo na matatizo hayo yanatokanana maeneo yenye mteremko kwa hiyo mawasiliano yaliyopo katika eneo hili kuna maeneo ambayo hayana mawasiliano kwa sababu yako chini. Kwa hiyo, tutahakikisha kwamba kwanza kama nilivyokuambia nitapenda nipite hayo maeneo barabara hiyo nikajionee halafu baada ya hapo tuwatake watu wa Mawasiliano kwa Wote wajaribu kurekebisha hayo maeneo ambayo ni ya mteremko tunawezaje kuyapelekea mawasiliano.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:- Serikali iliahidi kuweka minara katika Kata ya Sindano, Mchauru, Lipumbiru na Lupaso. Je, ni lini minara hiyo itajengwa ili kuondoa tatizo la kutokuwa na mawasiliano katika maeneo hayo?

Supplementary Question 5

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali ya nyongeza.
Tatizo la mawasiliano lililopo Lulindi linafanana na
tatizo lililopo katika jimbo la Lupembe Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Katika Halmashauri tuna kata nne ambazo hazina mawasiliano kata za Ninga, Ikondo, Ukalawa na Mfiriga hakuna minara na hakuna mawasiliano, je, ni lini Serikali itajenga minara katika kata hizi ili wananchi waweze kupata mawasiliano kwa kuwa inawaathiri kiuchumi kutokana na kutokuwepo mawasiliano? Naomba majibu ya Serikali. Ahsante sana.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kila kijiji Tanzania kinafikishiwa mawasiliano. Na ndio dhamira ya kuanzisha Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote. Kwa hiyo, nikuhakikishe Mheshimiwa Mbunge tutayafikisha mawasiliano katika maeneo hayo uliyoyataja mara tutakapopata fedha za kutuwezesha kufikisha mawasiliano maeneo haya.